Ni nani aliyemtuma Prof. Mruma na ni lini?

Ni nani aliyemtuma Prof. Mruma na ni lini?

Acha kuwa kichwa cha kuku mjomba ,,vyombo vya usalama siku zote huwa na plan za miaka hata kumi au ishirini ,mbele tafuta anayejua maswala ya kupenyezwa kidogo moja 2 3 ,utaelewa na hilo ni jambo la kawaida sema hauyajuii,,, na kama magu akisema kamtuma hajakosea kwa kua magu ndio boss wa usalam ,,,so sioni cha kushangaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizo plan za miaka ishirini kwa mtindo uliotokea leo ni plan za hovyo dunia.Mossad,kb na cia hawawezi fanya,hii inaweza tokea tz pekee.
 
Hivi inawezekanaje mtu asaini mkataba mbovu kisa katumwa upelelezi
 
Sasa kama ndio hivyo hakuna mantiki ya kuwepo kwa intelijensia,yaani yeye kasaini akijua yupo kazini ilihali anajua serikali inapata hasara na hicho alichokisaini anajua kitalipa shida taifa.Hivi ni bora kuzuia hasara au ni kusaini ukijua utapata hasara ili baadaye uje hudai fidia
Huo ni mtazamo wako na unahaki zote za kufikiri unavyodhani ila pale unapoamini fikira zako ndo sahihi hapo ndo makosa

Sidhani kama alisaini mikataba zaidi ya gharama za kuendesha mgodi! Yeye kama mwenyekiti wa Bodi akiwa pale kama mtafuta taarifa namna bodi ilivyo na uozo, atawezaje kuanza kupingana na bodi kabla hajatimiza malengo!?

Hatuna budi kukubali hao waliopewa zawadi za mawe ya ALMASI ilifikia hatua wakawa wazinguaji! Mambo kama haya tunayoyaona sidhani kama ni mageni kwa baadhi ya watu serikalini!!!

Waliyajua ili hawakuwa na wakuyasemea!! Na wao wasingeweza kuyasema hadharani kwa sababu hawakuwa na fursa hiyo

Naungana na Bashe aliposema Kinga ziondolewe kwa baadhi ya viongozi maana sio rahisi Waziri kusaini mkataba ulioandaliwa nje ya nchi na wawekezaji wenyewe tena huko huko kwao bila system ya usalama kujua na kiongozi mwenyewe wa nchi asijue!!!

Hawa wote wanaotajwa tajwa na kuambiwa wapishe uchunguzi, ni kafala tu!

Ningekuwa mimi ndo Rais, wala nisingemgusa yeyeto!! Ningewaita ofisi ya AG na wahusika wa mikataba hiyo wanieleze kinaga ubaga then madongo yangehamia kwa hao waliokuwa TOP LEADERS kwanini waliyaruhusu!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwahiyo alitumwa muda wooote huo madini yanatoroshwa wala hayazuiliwi yy bado anatumikia?? Matrilioni yanapotea aliyetumwa anakusanya "data"???? Hahahaaaaa....Lissu yukowapi atufafanulie haya
 
Kwetu ukishakuwa mkubwa(MTU mzima) hatutegemei useme uongo . Tunatazamia yote utakayosema ni kweli tena kweli tupu. Ndio sababu ukimkuta Mtoto akitenda makosa tunawajibu wa kumrudi.na hakuna anayelalamika kwa sababu tunaamini ktk kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ripoti ya zungu inataja makosa yapi ya huyu shushu mruma?,
 
Na chenge alitumwa jamani, hata simba chawene sema wao hawakurudisha majbu
 
kwahiyo alitumwa muda wooote huo madini yanatoroshwa wala hayazuiliwi yy bado anatumikia?? Matrilioni yanapotea aliyetumwa anakusanya "data"???? Hahahaaaaa....Lissu yukowapi atufafanulie haya
Wamemtumbua lissu mapma kabla hajawajibu. Kinachofata ni sheria kupitishwa kwa hati ya dharula kabla lisu hajarud bungeni.

[emoji124]‍♂️naenda zimbobo.
 
Matendo na jinsi alivyoshughulika na mambo mbalimbali kuhusu suala la Almasi, Profesa Mruma hana sifa ya kuitwa shushushu bali ni mzembe wa kiwango cha juu na anafanya sisi kama jamii tuhoji weledi wa wasomi wetu linapokuja suala la uelewa wa nini cha kufanya na kutokufanya kulingana na wakati.

Mruma ni sehemu ya tatizo na wala hawezi kuwa shushushu.
 
Matendo na jinsi alivyoshughulika na mambo mbalimbali kuhusu suala la Almasi, Profesa Mruma hana sifa ya kuitwa shushushu bali ni mzembe wa kiwango cha juu na anafanya sisi kama jamii tuhoji weledi wa wasomi wetu linapokuja suala la uelewa wa nini cha kufanya na kutokufanya kulingana na wakati.

Mruma ni sehemu ya tatizo na wala hawezi kuwa shushushu.
Ni fisadi mwenye vyeti vya uprofesa lakini hajitambui
 
Back
Top Bottom