Ni muhimu kwa Mashirika na Kampuni mbalimbali kulinda Data za Wateja wao

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
bycv.png

Sheria ya #UlinziWaData ambayo bado haipo nchini Tanzania ina umuhimu mkubwa kwasababu itasaidia kulinda data za mteja kama zifuatazo;

Majina ya Watu(Wateja kama ni kwenye Kampuni ya biashara), Anuani za Posta na Makazi za Wananchi ambao na Wateja wa Makampuni ya biashara

Barua pepe za watu, hii inajumuisha mawasiliano yote yanayaofanyika kwa njia ya barua pepe na kufanikishwa chini ya uwezeshaji wa mtoa huduma



MTEJA ANA HAKI YA KULINDIWA DATA ZAKE ZA KIBENKI NA AFYA

tcrf.png

Sheria ya ulinzi wa data Tanzania inahitajika ili kulinda haki ya kila Mtanzania ya kulindiwa taarifa zake, iliyoidhinishwa katika ibara ya 16 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa za Kibenki na miamala yote inayofanyika kupitia Taasisi za Fedha. Sheria ya ulinzi wa data itazitaka Kampuni husika kuhakikisha taarifa za wateja wao zinatunzwa

Taarifa za afya za Watu, taarifa hizi hukusanywa na Taasisi mbalimbali zinazotoa huduma ya afya pamoja na mashirika yanayotoa Bima za Afya
 
Hii Sheria ingekuwepo nchini, nadhan ingeshakua imefutwa na JPM(RIP)...rejea udukuzi wa mawasiliaano Kwa wasaidizi wake.ivi alikuwa anapataje huo mda ??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom