Ni kwanini Rais Samia anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume ya Majaji kumchunguza Biswalo Mganga, aliyekuwa DPP?

Hahaaa unajitahidi sana kukitetea chama!.

Sijui kwanini hawakuoni, au bado wanakupima. Keep it up!.

Sasa anatetea nini Hapo na kakuambia simple fact. Kasome kwanza. Acha kuwa na mambo ya Vyama Vyama kwenye mijadala ya kimantiki.
 
Ukweli ni huu HORSE POWER ...wote waliokuwa viongozi wa juu katika serikali ya Magufuli bado wapo, wengine wao katika nyadhifa za juu zaidi Serikalini, Mahakamani na Bungeni. Tena Bungeni ndio usiseme, wapo kwa asilimia 99%.

Magufuli aliwaagiza watu kutekeleza matakwa yake hata pale yalipopishana na Katiba ya nchi. Watekelezaji hao wote bado wapo na wengine wamepandishwa vyeo. Hizi zote ni katika jitihada za kulindana ambayo ni sera kuu ya CCM.

Kumbuka kazi iendeleeee!
Mag3
Hapa Solution ni kupata Katiba mpya, tena ile Rasimu ya Jaji Warioba, ambayo ndiyo maoni ya wananchi
 
Zipo tuhuma nzito Sana zinazomkabili aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga, kuhusiana na kile kinachoitwa "plea bargaining" mtindo uliobuniwa wakati wa utawala wa awamu ya 5, ambapo watuhumiwa "waliobambikiwa" makosa, wakati wa utawala wa awamu ya 5, "walilazinishwa" kukiri makosa na hivyo kukamuliwa mabilioni ya pesa, ambapo inadaiwa kuwa mabilioni hayo hayakufikishwa kwenye hazina ya Taifa hili na badala yake ziliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake!

Hizi ni tuhuma nzito Sana kumkabili mtumishi wa Umma, tena mwenye hadhi ya ujaji, Biswalo Mganga, ambapo anadaiwa kuwa Kati ya shilingi bilioni 51, alizokusanya kwa njia hiyo ya "plea bargainining" mabilioni mengi, hakuyafikisha hazina, kwa mujibu wa taarifa ya CAG, Charles Kicheere, na badala yake, mabilioni hayo yanasemekana, yaliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake.

Watuhumiwa hao waliobambikiziwa Kesi, Ili hatimaye walazimishwe kukiri makosa hayo wanayotuhumiwa nayo na baadaye "wakamuliwe" mabilioni hayo ya pesa, wametoa wito kwa Rais wetu, aweze kuunda Tume ya Majaji, kuchunguza tuhuma hizi nzito, wakati huo huo akimsimamisha Kazi ya ujaji, aliyomteua mapema mwaka jana.

Ni utaratibu wa kawaida sana, unaotumika Katika nchi za Jumuiya ya Madola, ambayo nchi yetu ipo, ambapo tunalazimika kufuata.

Swali kubwa ninalojiuliza, ni kwanini hadi hivi sasa, Rais Samia, anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo ya Majaji, ambayo itatafuta ukweli wa kujua kama tuhuma hizo ni za kweli au la?

Ni vyema Rais Samia, akatambua kuwa kushikwa kwake na "kigugumizi" cha kuunda Tume hiyo ya Majaji,, kutatoa tafsiri kwa wananchi wengi kuwa, yeye Rais ana mpango wa kumwewekea kinga dhidi ya tuhuma anazokabiliwa nazo huyo aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga.

Vile vile itatoa tafsiri kuwa kuna baadhi ya watu hapa nchini, hususani viongozi waandamizi wa Serikali hii ya CCM, wanapewa kinga ya "impunity" ya kutoshtakiwa, hata kama wamefanya makosa makubwa ya jinai, jambo ambalo halitendi haki kwa wananchi, kwa kuwa Katiba yetu inaeleza wazi kuwa wananchi wote, wapo sawa mbele ya sheria.
Huyu anasiri nyingi. Si faida kwa Serikali kumfungulia mashtaka. Ni hatari kwa serikali yenyewe.
 
Zipo tuhuma nzito Sana zinazomkabili aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga, kuhusiana na kile kinachoitwa "plea bargaining" mtindo uliobuniwa wakati wa utawala wa awamu ya 5, ambapo watuhumiwa "waliobambikiwa" makosa, wakati wa utawala wa awamu ya 5, "walilazinishwa" kukiri makosa na hivyo kukamuliwa mabilioni ya pesa, ambapo inadaiwa kuwa mabilioni hayo hayakufikishwa kwenye hazina ya Taifa hili na badala yake ziliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake!

Hizi ni tuhuma nzito Sana kumkabili mtumishi wa Umma, tena mwenye hadhi ya ujaji, Biswalo Mganga, ambapo anadaiwa kuwa Kati ya shilingi bilioni 51, alizokusanya kwa njia hiyo ya "plea bargainining" mabilioni mengi, hakuyafikisha hazina, kwa mujibu wa taarifa ya CAG, Charles Kicheere, na badala yake, mabilioni hayo yanasemekana, yaliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake.

Watuhumiwa hao waliobambikiziwa Kesi, Ili hatimaye walazimishwe kukiri makosa hayo wanayotuhumiwa nayo na baadaye "wakamuliwe" mabilioni hayo ya pesa, wametoa wito kwa Rais wetu, aweze kuunda Tume ya Majaji, kuchunguza tuhuma hizi nzito, wakati huo huo akimsimamisha Kazi ya ujaji, aliyomteua mapema mwaka jana.

Ni utaratibu wa kawaida sana, unaotumika Katika nchi za Jumuiya ya Madola, ambayo nchi yetu ipo, ambapo tunalazimika kufuata.

Swali kubwa ninalojiuliza, ni kwanini hadi hivi sasa, Rais Samia, anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo ya Majaji, ambayo itatafuta ukweli wa kujua kama tuhuma hizo ni za kweli au la?

Ni vyema Rais Samia, akatambua kuwa kushikwa kwake na "kigugumizi" cha kuunda Tume hiyo ya Majaji,, kutatoa tafsiri kwa wananchi wengi kuwa, yeye Rais ana mpango wa kumwewekea kinga dhidi ya tuhuma anazokabiliwa nazo huyo aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga.

Vile vile itatoa tafsiri kuwa kuna baadhi ya watu hapa nchini, hususani viongozi waandamizi wa Serikali hii ya CCM, wanapewa kinga ya "impunity" ya kutoshtakiwa, hata kama wamefanya makosa makubwa ya jinai, jambo ambalo halitendi haki kwa wananchi, kwa kuwa Katiba yetu inaeleza wazi kuwa wananchi wote, wapo sawa mbele ya sheria.
Tanzania wasomi ni wachache ukimtoa utampata wapi mwingine? Huoni hata mawaziri wanajirudia rudia hatuna nafasi ya kutengeneza nguvu kazi mpa
 
Huyu anasiri nyingi. Si faida kwa Serikali kumfungulia mashtaka. Ni hatari kwa serikali yenyewe.
Zawadi Ngoda
Kuna msemo wa kiswahili unaosema,.. mficha ficha maradhi, mwisho kilio kitamwumbua...........

Kama Hawa CCM, wanaona hiyo ndiyo njia muafaka, watambue kwamba na sisi wananchi, tumebaini ukwapuaji mkubwa wa mabilioni ya shilingi, unavyofanywa na Serikali hii ya CCM

Kwa hiyo solution pekee ni kuwaondoa jumla jumla, hao wakwapuaji, kwenye sanduku la kura, muda ukiwadia.
Time will tell
 
Tanzania wasomi ni wachache ukimtoa utampata wapi mwingine? Huoni hata mawaziri wanajirudia rudia hatuna nafasi ya kutengeneza nguvu kazi mpa
Hizo nafasi kujirudia rudia, siyo k sababu watanzania wasomi hawapo, la hasha, bali inatokana na mfumo wa kiutawaka wa CCM, ambao wanaogopa kuweka sura mpya zenye kutaka kuleta mageuzi kisiasa na kiuchumi
 
Elewa kwanza sheria ya plea bargaining ndio uje kulalamika hapa.

Maana unaweza leta lawama out of ignorance.
Nikusaidie wewe bush lawyer. Sheria Ile ilitungwa na kufanya kazi kabla ya kuwekewa kanuni zake na hapo ndipo kwenye utata! Uwe unatafiti kabla ya kupata hewani!
 
Mna mawazo ya kijinga! Na utoto mwingi. Tume ya nini na wakati mijizi kama Kabendera na akina sethi walishikishwa adabu. Umesahau mara hii Tegeta escrow wajinga nyie
Una umri Gani? Kama ni under 30yrs basi hujui lolote kuhusu tegeta escrow na nani wamiliki halali! Unakumbuka Kikwete alisema Nini juu ya pesa zile kuwa ni Mali ya nani na kwanini alisema vile mbele ya wazee wa Dar? Au basi tuache TU.
 
Nikusaidie wewe bush lawyer. Sheria Ile ilitungwa na kufanya kazi kabla ya kuwekewa kanuni zake na hapo ndipo kwenye utata! Uwe unatafiti kabla ya kupata hewani!
Bora unemfafanulia ukweli huyo jamaa🤝
 
Elewa kwanza sheria ya plea bargaining ndio uje kulalamika hapa.

Maana unaweza leta lawama out of ignorance.

Kwamba hiyo sheria inapeleka hela kwa watu binafsi, hakili ya hovyo sana hiii
 
Mshana Jr
Sasa kama Rais ataendelea kushikwa na "kigugumizi" cha kuunda Tume ya Majaji, wananchi tutabaini kuwa kumbe wote hao viongozi wa CCM, wapo kwenye mkumbo mmoja, wa kutaka kuendelea kutuibia sisi watanzania! Full Stop

Mkuu iwapo nchi itapinduliwa, au chama kingine kuingia madarakani hilo linaweza kufanyika. Lakini CCM iliyoko madarakani kwa maagizo ya Magufuli usitegemee hilo.
 
Ilitungwa lini ?
Tatizo ni muda au content??

Maana kuna watu hapa kama mleta mada tatizo lake sio sheria bali ni nani kaitunga ndio maana hata wewe umeuliza imetungwa lini?

Malengo hapa ni kutafuta kila njia mradi Magufuli atachafuliwa.
 
Mna mawazo ya kijinga! Na utoto mwingi. Tume ya nini na wakati mijizi kama Kabendera na akina sethi walishikishwa adabu. Umesahau mara hii Tegeta escrow wajinga nyie

Mijizi inapaswa kupelekwa mahakamani ili ichukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria, na sio kuporwa fedha zao na genge la Magufuli kwa kichaka cha kupambana na wezi. Sasa pesa zilizokusanywa haifahamiki nyingine ziko wapi. Huwezi kupambana na majizi kwa ujizi.
 
Back
Top Bottom