Ni kwanini Rais Samia anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume ya Majaji kumchunguza Biswalo Mganga, aliyekuwa DPP?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Zipo tuhuma nzito Sana zinazomkabili aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga, kuhusiana na kile kinachoitwa "plea bargaining" mtindo uliobuniwa wakati wa utawala wa awamu ya 5, ambapo watuhumiwa "waliobambikiwa" makosa, wakati wa utawala wa awamu ya 5, "walilazinishwa" kukiri makosa na hivyo kukamuliwa mabilioni ya pesa, ambapo inadaiwa kuwa mabilioni hayo hayakufikishwa kwenye hazina ya Taifa hili na badala yake ziliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake!

Hizi ni tuhuma nzito Sana kumkabili mtumishi wa Umma, tena mwenye hadhi ya ujaji, Biswalo Mganga, ambapo anadaiwa kuwa Kati ya shilingi bilioni 51, alizokusanya kwa njia hiyo ya "plea bargainining" mabilioni mengi, hakuyafikisha hazina, kwa mujibu wa taarifa ya CAG, Charles Kicheere, na badala yake, mabilioni hayo yanasemekana, yaliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake.

Watuhumiwa hao waliobambikiziwa Kesi, Ili hatimaye walazimishwe kukiri makosa hayo wanayotuhumiwa nayo na baadaye "wakamuliwe" mabilioni hayo ya pesa, wametoa wito kwa Rais wetu, aweze kuunda Tume ya Majaji, kuchunguza tuhuma hizi nzito, wakati huo huo akimsimamisha Kazi ya ujaji, aliyomteua mapema mwaka jana.

Ni utaratibu wa kawaida sana, unaotumika Katika nchi za Jumuiya ya Madola, ambayo nchi yetu ipo, ambapo tunalazimika kufuata.

Swali kubwa ninalojiuliza, ni kwanini hadi hivi sasa, Rais Samia, anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo ya Majaji, ambayo itatafuta ukweli wa kujua kama tuhuma hizo ni za kweli au la?

Ni vyema Rais Samia, akatambua kuwa kushikwa kwake na "kigugumizi" cha kuunda Tume hiyo ya Majaji,, kutatoa tafsiri kwa wananchi wengi kuwa, yeye Rais ana mpango wa kumwewekea kinga dhidi ya tuhuma anazokabiliwa nazo huyo aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga.

Vile vile itatoa tafsiri kuwa kuna baadhi ya watu hapa nchini, hususani viongozi waandamizi wa Serikali hii ya CCM, wanapewa kinga ya "impunity" ya kutoshtakiwa, hata kama wamefanya makosa makubwa ya jinai, jambo ambalo halitendi haki kwa wananchi, kwa kuwa Katiba yetu inaeleza wazi kuwa wananchi wote, wapo sawa mbele ya sheria.
 
Hiyo ni integrated system... Ni mfumo wenye chain ya wengi, kutaka kumgusa mmoja ni kutaka kuuchezesha mfumo wote.. Nani atakubali?
Mshana Jr
Sasa kama Rais ataendelea kushikwa na "kigugumizi" cha kuunda Tume ya Majaji, wananchi tutabaini kuwa kumbe wote hao viongozi wa CCM, wapo kwenye mkumbo mmoja, wa kutaka kuendelea kutuibia sisi watanzania! Full Stop
 
Elewa kwanza sheria ya plea bargaining ndio uje kulalamika hapa.

Maana unaweza leta lawama out of ignorance.
Haya wewe kada wa CCM, tueleweshe, jinsi hiyo sheriia ya "plea bargaining" inavyofanya Kazi.

Hata hivyo hapa hatuongelei namna sheria hiyo inavyofanya Kazi, bali tunaongelea, namna hayo mabilioni yaliyokusanywa na yalivyotafunwa na huyo Biswalo Mganga na washirika wake, kinyume cha utaratibu
 
Mshana Jr
Sasa kama Rais ataendelea kushikwa na "kigugumizi" cha kuunda Tume ya Majaji, wananchi tutabaini kuwa kumbe wote hao viongozi wa CCM, wapo kwenye mkumbo mmoja, wa kutaka kuendelea kutuibia sisi watanzania! Full Stop
Unajua Mystery kuna siasa na kuna uhalisia.. Siasa ziko majukwaani na ahadi nyingi tamutamu ili kuipoza jamii.. Lakini ukija kwenye uhalisia unachanwa live unaambiwa kabisa ZILE NI SIASA TUU LAKINI HILI HALIWEZEKANI
 
Waliofaidi yale mabilioni ni wale waliotengeneza huo mfumo. Si kama ofisi yake awamu ya 5 hajui waliokuwa wanufaikaji wa ule mfumo, usikute naye alihusika ndiomana anasita kuunda hiyo tume.
Ndiyo maana tunamshinikiza Rais Samia aunde Tume hiyo ya Majaji, kwa kuwa siyo "fair" kwa nchi hii moja, baadhi ya watu waruhusiwe kutafuna mabilioni ya pesa, kama vile wapo "above law" wakati wananchi wengine wanasulubiwa na wamehukumiwa Mahakamani kwa wizi wa kuku tu!🥺
 
Wakerewe na wajita, huwa Wana vitabia fulani hivi, na Biswalo ni WA huko huko, na hivyo vitabia anavyo, bahati mbaya aliruhusiwa kufanya anavyotaka. Sasa changanya vitabia hivyo, pamoja na Uhuru aliopewa na JPM, it was dangerous.
 
Mshana Jr
Sasa kama Rais ataendelea kushikwa na "kigugumizi" cha kuunda Tume ya Majaji, wananchi tutabaini kuwa kumbe wote hao viongozi wa CCM, wapo kwenye mkumbo mmoja, wa kutaka kuendelea kutuibia sisi watanzania! Full Stop
Mkuu mbona una jibu tayari, na pia kuna mchango muhimu hapo kuwa hii ni systems, means huwezi to just pick one person!,na elewa ni fedha ya serikali inayoendesha chama cha ccm,unafikiri budget ya mwezi ya mishahara ya watumishi wa ccm ni kiasi gani?,je ccm waneshawahi kusema sources of their income?,katiba mpya ndio jibu maana political parties vitalazimika kutangaza sources zao za mapato!,kuna mtu alitugeuza mazuzu
 
Zipo tuhuma nzito Sana zinazomkabili aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga, kuhusiana na kile kinachoitwa "plea bargaining" mtindo uliobuniwa wakati wa utawala wa awamu ya 5, ambapo watuhumiwa "waliobambikiwa" makosa, wakati wa utawala wa awamu ya 5, "walilazinishwa" kukiri makosa na hivyo kukamuliwa mabilioni ya pesa
Hili la watuhuhumiwa kubambikiwa kesi, na kukamuliwa, karma imeisha lishughulikia
, ambapo inadaiwa kuwa mabilioni hayo hayakufikishwa kwenye hazina ya Taifa hili na badala yake ziliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake!
Mkuu Mystery , maadam ni inadaiwa, then acha tuu idaiwe, ila pesa za plea bargain zililipwa kwa maandishi tena kupitia a control number, pesa hizo ziliingia serikalini na pesa ukiisha ingia serikalini, haiwezi kutoka bila maandishi!. Hivyo maandishi ya every cent yapo!.
Hizi ni tuhuma nzito Sana kumkabili mtumishi wa Umma, tena mwenye hadhi ya ujaji, Biswalo Mganga, ambapo anadaiwa kuwa Kati ya shilingi bilioni 51, alizokusanya kwa njia hiyo ya "plea bargainining" mabilioni mengi, hakuyafikisha hazina, kwa mujibu wa taarifa ya CAG, Charles Kicheere, na badala yake, mabilioni hayo yanasemekana, yaliishia kwenye mifuko ya Biswalo Mganga na washirika wake.
Fedha kukusanywa na kutofikishwa kwenye mfuko mkuu wa hazina, haina maana ndio zimetafunwa!, ni utaratibu tuu ndio haukufuatwa, hivyo CAG hakuziona ila sio lazima kila fedha ambazo CAG hakuziona ni zimetafunwa!. Enzi za CAG Prof. Asad kuna 1.5B hazikuonekana!. Mbona hakusimamishwa mtu kupisha uchunguzi?. Tulinunua ndege kwa cash cash kwa kuchota kutoko mfuko mkuu hazina na kulipa tulikolipa bila kufuata utaratibu!, mbona hamkuomba uchunguzi?.
Watuhumiwa hao waliobambikiziwa Kesi, Ili hatimaye walazimishwe kukiri makosa hayo wanayotuhumiwa nayo na baadaye "wakamuliwe" mabilioni hayo ya pesa, wametoa wito kwa Rais wetu, aweze kuunda Tume ya Majaji, kuchunguza tuhuma hizi nzito, wakati huo huo akimsimamisha Kazi ya ujaji, aliyomteua mapema mwaka jana.
Tume ya nini kuchunguza nini wakati maandishi yote ya makisanyo hayo yapo na matumizi yapo?.
Ni utaratibu wa kawaida sana, unaotumika Katika nchi za Jumuiya ya Madola, ambayo nchi yetu ipo, ambapo tunalazimika kufuata.

Swali kubwa ninalojiuliza, ni kwanini hadi hivi sasa, Rais Samia, anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo ya Majaji, ambayo itatafuta ukweli wa kujua kama tuhuma hizo ni za kweli au la?
Niliwahi kushauri, kama JPM, aliyafanya yote aliyoyafanya na hatukumpangia, basi na Samia tusimpangie!.
Ni vyema Rais Samia, akatambua kuwa kushikwa kwake na "kigugumizi" cha kuunda Tume hiyo ya Majaji,, kutatoa tafsiri kwa wananchi wengi kuwa, yeye Rais ana mpango wa kumwewekea kinga dhidi ya tuhuma anazokabiliwa nazo huyo aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga.
Kumefanyika mangapi ndivyo sivyo na hamkuomba uchunguzi, why hili?, nilidhani labda sasa ndio mngeomba uchunguzi wa shambulizi la Lissu ndio ufanyike!, mnaomba uchunguzi wa kitu very systematic kama fedha zilizolipwa kwa control number?. Acheni hizo!.
Vile vile itatoa tafsiri kuwa kuna baadhi ya watu hapa nchini, hususani viongozi waandamizi wa Serikali hii ya CCM, wanapewa kinga ya "impunity" ya kutoshtakiwa, hata kama wamefanya makosa makubwa ya jinai, jambo ambalo halitendi haki kwa wananchi, kwa kuwa Katiba yetu inaeleza wazi kuwa wananchi wote, wapo sawa mbele ya sheria.
Usichanganye tuhuma na makosa, hizi ni tuhuma tuu, maadam ni Mama mwenyewe kaamua kuzichunguza bila kupangiwa na yeyote, mwacheni Mama afanye kazi, tuhuma zikithibitishwa, hatua stahiki zitachukuliwa!.

Mungu ibariki Tanzania,
Kazi iendelee...
P
 
Hili la watuhuhumiwa kubambikiwa kesi, na kukamuliwa, karma imeisha lishughulikia

Mkuu Mystery , maadam ni inadaiwa, then acha tuu idaiwe, ila pesa za plea bargain zililipwa kwa maandishi tena kupitia a control number, pesa hizo ziliingia serikalini na pesa ukiisha ingia serikalini, haiwezi kutoka bila maandishi!. Hivyo maandishi ya every cent yapo!.

Fedha kukusanywa na kutofikishwa kwenye mfuko mkuu wa hazina, haina maana ndio zimetafunwa!, ni utaratibu tuu ndio haukufuatwa, hivyo CAG hakuziona ila sio lazima kila fedha ambazo CAG hakuziona ni zimetafunwa!. Enzi za CAG Prof. Asad kuna 1.5B hazikuonekana!. Mbona hakusimamishwa mtu kupisha uchunguzi?. Tulinunua ndege kwa cash cash kwa kuchota kutoko mfuko mkuu hazina na kulipa tulikolipa bila kufuata utaratibu!, mbona hamkuomba uchunguzi?.

Tume ya nini kuchunguza nini wakati maandishi yote ya makisanyo hayo yapo na matumizi yapo?.

Niliwahi kushauri, kama JPM, aliyafanya yote aliyoyafanya na hatukumpangia, basi na Samia tusimpangie!.

Kumefanyika mangapi ndivyo sivyo na hamkuomba uchunguzi, why hili?, nilidhani labda sasa ndio mngeomba uchunguzi wa shambulizi la Lissu ndio ufanyike!, mnaomba uchunguzi wa kitu very systematic kama fedha zilizolipwa kwa control number?. Acheni hizo!.

Usichanganye tuhuma na makosa, hizi ni tuhuma tuu, maadam ni Mama mwenyewe kaamua kuzichunguza bila kupangiwa na yeyote, mwacheni Mama afanye kazi, tuhuma zikithibitishwa, hatua stahiki zitachukuliwa!.

Mungu ibariki Tanzania,
Kazi iendelee...
P
Paskali sometimes una majibu amazing sana, yani pesa zimekusanywa halafu hazijaonekana kwenye mfuko wa hazina unasema hazijatafunwa!.

Hope zitakuwa mawinguni, ngoja nitoke hapo nje nikaangalie juu naweza kuziona zikipepea.
 
Hili la watuhuhumiwa kubambikiwa kesi, na kukamuliwa, karma imeisha lishughulikia

Mkuu Mystery , maadam ni inadaiwa, then acha tuu idaiwe, ila pesa za plea bargain zililipwa kwa maandishi tena kupitia a control number, pesa hizo ziliingia serikalini na pesa ukiisha ingia serikalini, haiwezi kutoka bila maandishi!. Hivyo maandishi ya every cent yapo!.

Fedha kukusanywa na kutofikishwa kwenye mfuko mkuu wa hazina, haina maana ndio zimetafunwa!, ni utaratibu tuu ndio haukufuatwa, hivyo CAG hakuziona ila sio lazima kila fedha ambazo CAG hakuziona ni zimetafunwa!. Enzi za CAG Prof. Asad kuna 1.5B hazikuonekana!. Mbona hakusimamishwa mtu kupisha uchunguzi?. Tulinunua ndege kwa cash cash kwa kuchota kutoko mfuko mkuu hazina na kulipa tulikolipa bila kufuata utaratibu!, mbona hamkuomba uchunguzi?.

Tume ya nini kuchunguza nini wakati maandishi yote ya makisanyo hayo yapo na matumizi yapo?.

Niliwahi kushauri, kama JPM, aliyafanya yote aliyoyafanya na hatukumpangia, basi na Samia tusimpangie!.

Kumefanyika mangapi ndivyo sivyo na hamkuomba uchunguzi, why hili?, nilidhani labda sasa ndio mngeomba uchunguzi wa shambulizi la Lissu ndio ufanyike!, mnaomba uchunguzi wa kitu very systematic kama fedha zilizolipwa kwa control number?. Acheni hizo!.

Usichanganye tuhuma na makosa, hizi ni tuhuma tuu, maadam ni Mama mwenyewe kaamua kuzichunguza bila kupangiwa na yeyote, mwacheni Mama afanye kazi, tuhuma zikithibitishwa, hatua stahiki zitachukuliwa!.

Mungu ibariki Tanzania,
Kazi iendelee...
P
Kama wapuuzi kama Mystery hawatakuelewa, basi tu. Mchango wako uheshimike
 
Kama wapuuzi kama Mystery hawatakuelewa, basi tu. Mchango wako uheshimike
Sasa upuuzi wangu uko wapi?

Nilichosema Mimi ni kuwa tunamuomba Rais wetu aunde Tume ya Majaji kuchunguza tuhuma hizo, kama utaratibu wa nchi za Jumuiya ya Madola, inavyofanya.

Ninachojiuliza, ni kwanini Rais wetu anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo ya Majaji??
 
Sasa upuuzi wangu uko wapi?

Nilichosema Mimi ni kuwa tunamuomba Rais wetu aunde Tume ya Majaji kuchunguza tuhuma hizo.

Ninachojiuliza, ni kwanini Rais wetu anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo ya Majaji??
Mna mawazo ya kijinga! Na utoto mwingi. Tume ya nini na wakati mijizi kama Kabendera na akina sethi walishikishwa adabu. Umesahau mara hii Tegeta escrow wajinga nyie
 
Mna mawazo ya kijinga! Na utoto mwingi. Tume ya nini na wakati mijizi kama Kabendera na akina sethi walishikishwa adabu. Umesahau mara hii Tegeta escrow wajinga nyie
Unawezaje kusema kuwa akina Kabendera, walikuwa wezi?

Ndiyo maana tunasema iundwe Tume ya Majaji Ili ukweli ubainike.

Sasa ni kwanini Rais Samia, hataki kuunda hiyo Tume ya Majaji?
 
Back
Top Bottom