Ni biashara gani ambayo huelewi faida wanapata vipi?

Sio kila biashara unayoona ndiyo biashara inayouzwa hapo wengine wanazugia tu mfano sinza kino unakuta mtu Ana frem ya laki mbili dukani Kuna t-shirt kumi na viatu pair kumi kumbe mwenzio anajiuzia zake bange na madawa we unakaa kuwaza anapaje faida.faida hipo ndiyo Mana biashara haifungwi
 
JAMIIFORUMS
-Mnalipa kodi
-Mnalipa pango,maji,umeme
-Mnanunua mitambo
-Mnalipa mishahara na viinua migongo.
-Mnanunua vifaa,mnafanya marekebisho
-Hamfanyi matangazo
-Mnalipia gharama za kesi mahakamani
-Mnalipia server,vibali.
Mr. Melo, mnatengenezaje faida.
Hawa nao JFs pia siwaelewi.

Hata matangazo hawafanyi.

Sisi kujiinga ni Bure😂😂😂
 
Japo mwenyewe nafanya biashara ya uwakala lakini sioni faida najiuliza wenzangu wanapataje faida 😀😀😀 vicommission vidogo dogo sijui sh 20, 30... kodi ya frame 150,000/= × 6 unategemea itarudi vipi?
Nikisikia Comision za Miamala nashangaa sana zile kazi wanaozifanya.

Mwezi mzima mtu anapata kamisheni ya Laki tatu. Hapao kajumlisha mitandao kama mitatu.
 
Hiyo ni miaka ya kuanzia 2015 ndiyo majengo yakawa matupu but maghorofa bado yanajengwa barabara hizo hizo
Bagamoyo road uchumi umeanza kushuka awamu ya tano.
Yaani ni miaka hii tu unakuta Apartment na office space zimeandikwa mabao yaatangazo.

Zamani ulikuwa kupata sehemu ya biashara ni mbinde.

Siku hizi huwatafuti madalali wao ndio wanakutafuta.
 
Japo mwenyewe nafanya biashara ya uwakala lakini sioni faida najiuliza wenzangu wanapataje faida 😀😀😀 vicommission vidogo dogo sijui sh 20, 30... kodi ya frame 150,000/= × 6 unategemea itarudi vipi?
Hapo hujakutana na Kaka tapeli 😂😂😂.
Ila uwakala unalipa Kama una mtaji mkubwa na location yenye mzunguko mkubwa wa watu.
 
Wavuvi wa samaki yaani kuanzia Tanga, Pwani, Lindi, Mtwara ... maisha yao yapo ka hayapoo

Hawasii / hawapandi / hawafugii ... wao ni kuvuna tu
Hawa usiwahesabu kabisa, ni watu wana pesa kiasi ya kwamba akiwa na akili ya kujiongeza huwa wanasogea mbali mno. Hapa nawaongelea wanaomiliki hivyo vidau, ila kwa wavuvi wenyewe huwa ni kusukuma maisha tu
 
Duka la vyupi, duka la jumla ye ananunua elf 9 anauza elf 10...means faida buku.
Kodi laki na nusu kwa mwezi, muuzaji mshahara laki na nusu bado kula nauli. 🤔
Evelyn buku mbona kubwa sana, kuna watu wanafanya biashara faida kwa bidhaa sh. 200. Na mambo yanaenda tu.
Mzunguko ukiwa mkubwa inalipa
Mfano vinywaji vya jumla hakuna faida ya buku. Ni 200,300,500. Ila wanauza mpaka katoni 1000 kwa siku.
Sasa fanya 200*1000.
Mchawi mtaji tu na eneo zuri
 
Back
Top Bottom