Mmea Jr
JF-Expert Member
- May 20, 2016
- 551
- 1,222
Okay habari zenu wakuu ??. Natumaini wote mnafurahia kuuona mwaka 2024 . Na wale tunaokimbiza na ada tusijali wakuu tutatoboa tu .
Sawa tusipoteze muda leo ngoja niwapeni kisa fulani ambacho nimewahi kukutana nacho hapo nyuma katika mambo ya biashara .
Mkoa ninaoishi ni miongoni mwa mikoa yenye wafugaji wazuri sana wa mbuzi katoliki( nguruwe ) na walaji wakutosha . Sasa bwana katika kujitafuta mwenzenu nikaona ngoja nijaribu hii biashara ya kuuza mbuzi katoriki maana jamaa yangu fulani yeye alikuwa kafungua gori pande za katikakati ya mji na aliniambia hii biashara inalipa sana plus kunifundisha mbinu mbali mbali za kuibia wateja ilimradi tu mwisho wa siku itokee faida . Huyu jamaa huamini kwenye biashara yeyeto ile ukiona faida inakuja tu basi ujue kuna sehemu unakosea yeye usema " siku zote faida inabidi itafutwe faida haiji yenyewe "
Basi bwana nikatafuta sehemu na mimi nikajenga banda langu nunua ndizi mzuzu , katakata kachumbari , agiza nyama ya mbuzi katoliki (nilianza na kilo 7 ) . Mafuta ya kupikia lita 3 plus kabati fulani kubwa tu la vioo kwa ajili ya kuhifadhia nyama ili isiguswe guswe na nzi . Ili kipunguza gharama za kuendeshea nikachukua mkaa kwenye lita 10 ( wale waishio sehemu zinazochoma mkaa nadhani watanielewa hapa vizuri ).
Lakini pia nikapata wazo kwamba ili nipate maokoto ya kutosha vizuri kukang'aa nyama ya nguruwe pekee na kuuzia watu inaweza isinipe faida sana nikajisema " hata ikitokea mteja anataka kitimoto nitamuuzia tu " hivyo nikatafuta mzani . Yes, lakini kauli ya jamaa yangu ikanijia kichani. " faida haiji tu lazima uitafute " basi nikamcheki jamaa na kumpa wazo langu , mimi huyo kwenye simu " halo master sasa nimeona badala ya kuuza nyama pekee yake nimeonelea si vibaya pia nikawa nauza pia kwa kupimisha ili niwateke wateja wote wa mbuzi katoliki wa hili eneo " jamaa huyo anajibu sasa " safii sana master unaakili sana na ndiyo maana kila siku mimi huwa nakwambia wewe ni kichwa cha biashara ila sasa hebu lete huo mzani nikifundishe kitu " .
Basi bwana mimi huyo na mzani mbaka kwa kiongozi wangu wa biashara tukaenda kwa mshikaji wake ukaurekebisha vizuri mzani " lengo, ni ili mzani uwe unawaibia kidogo wateja ( wale wanaofanya biashara za kipima pima watakuwa wananielewa vizuri hapa juu ya huu uhuni ). Basi bwana siku hazigandi biashara ikaanza .
Siku ya kwanza nilipiga maokoto vizuri kwani nilisukuma kama kilo 5 hivi plus watu kibao kuulizia ulizia ( moyoni nikajisema mambo si haya ) siku ya pili sukuma kilo zote 7 , ya tatu sukuma kilo 5 tena . Nikajisea " sasa hii biashara nshaijua vizuri hapa ili nikimbizane vizuri na hawa wateja ngoja nilete kilo 10 sasa, eehh hili eneo linataka kilo 10 " . Baada ya kuleta kilo 10 siyo mbaya nilisukuma kama kilo 6 hivi.
Lakini sasa balaa lilianza wiki ya pili toka nianze biashara eneo lile . Uwezi amini jumatatu ya wiki ya pili toka nilipoanzisha kijiwe nikiwa nimeweka kilo kumi kwenye kabati langu la kuhifadhia nyama . Alikuja bibi mmoja akipiga "" hodi hodi mwanangu , mimi sijambo bibi shikamoo bibi marihaba mwanangu . Mimi karibu bibi asante . Mwanangu nilikuwa naulizia kama nyama ipo ??."
Mmmhh mimi nikaguna nakujiuliza swali inamaana nyama yote hii kwenye kabati bibi haioni ??. Nikahitimisha kwa kujisemea mmhh japo wote tutazeka ila uzee mbaya sanaa. Oky bibi nyama ipo yakutosha kabisa kwani ulikuwa unaitaji kiasi gani bibi yangu ??. Bibi hapana nilikuja kwanza kuulizia kama ipo . Nakuondoka zake , nikiwatafakari kilichotokea tena kwenye saa sita vijana wawili kwa mbali wakiwa wanapita " oyii mwanangu,,,,,,,,,, vipi ?? Mie oiiii!! oiiii !!! oiiiii!!! poa wakuu vipi leo huna mzigo nini ?? Eehh nikayarudisha macho chap sandukuni kujilidhisha kama nyama ipo au haipo maana sielewi kwanini watu wananiuliza vile .. kucheki mzigo upo sasa kwanini naulizwa vile ??. Mzigo hupo tena wakutoshaaaa wazee huku nikitumia kidole changu kuwaoneshea mali iliyopo kabatini . Hinakwelee usiwaze jombaa tukipata mafekechee basi tutakuja kuchangamsha kijiwe . Amani amani wazee ntafurahi sana mkija.
Okay kumalizia tu wiki ile ilienda vile kwa kuulizwa kama nyama ipo na hata kwenye kuuza nyama ningeuza sanaa ni kilo 3 tu . Wiki ya tatu nilipoona hali imezidikuwa tete na tayari nimeshaingiliwa na hasara nusu ya mtaji wangu . Nikajisemea " bora nusu shari kuliko shari kamili acha nifikirie biashara nyingine huenda walimwengu wa huu mtaa hawajaipenda biashara niifanyayo nikafunga na kwasasa nipo nauza mafuta ya kupikia mtaa mwingine wale wote wenye connection nzuri ya wapi ntapata mafuta kwa bei chee tuchekiane nilipo dumu 80, 000/= ( huku tunapima kwa kilo na siyo kwa lita ) na lita moja wengi tunafanya 4500/=. Kwasasa
Sawa tusipoteze muda leo ngoja niwapeni kisa fulani ambacho nimewahi kukutana nacho hapo nyuma katika mambo ya biashara .
Mkoa ninaoishi ni miongoni mwa mikoa yenye wafugaji wazuri sana wa mbuzi katoliki( nguruwe ) na walaji wakutosha . Sasa bwana katika kujitafuta mwenzenu nikaona ngoja nijaribu hii biashara ya kuuza mbuzi katoriki maana jamaa yangu fulani yeye alikuwa kafungua gori pande za katikakati ya mji na aliniambia hii biashara inalipa sana plus kunifundisha mbinu mbali mbali za kuibia wateja ilimradi tu mwisho wa siku itokee faida . Huyu jamaa huamini kwenye biashara yeyeto ile ukiona faida inakuja tu basi ujue kuna sehemu unakosea yeye usema " siku zote faida inabidi itafutwe faida haiji yenyewe "
Basi bwana nikatafuta sehemu na mimi nikajenga banda langu nunua ndizi mzuzu , katakata kachumbari , agiza nyama ya mbuzi katoliki (nilianza na kilo 7 ) . Mafuta ya kupikia lita 3 plus kabati fulani kubwa tu la vioo kwa ajili ya kuhifadhia nyama ili isiguswe guswe na nzi . Ili kipunguza gharama za kuendeshea nikachukua mkaa kwenye lita 10 ( wale waishio sehemu zinazochoma mkaa nadhani watanielewa hapa vizuri ).
Lakini pia nikapata wazo kwamba ili nipate maokoto ya kutosha vizuri kukang'aa nyama ya nguruwe pekee na kuuzia watu inaweza isinipe faida sana nikajisema " hata ikitokea mteja anataka kitimoto nitamuuzia tu " hivyo nikatafuta mzani . Yes, lakini kauli ya jamaa yangu ikanijia kichani. " faida haiji tu lazima uitafute " basi nikamcheki jamaa na kumpa wazo langu , mimi huyo kwenye simu " halo master sasa nimeona badala ya kuuza nyama pekee yake nimeonelea si vibaya pia nikawa nauza pia kwa kupimisha ili niwateke wateja wote wa mbuzi katoliki wa hili eneo " jamaa huyo anajibu sasa " safii sana master unaakili sana na ndiyo maana kila siku mimi huwa nakwambia wewe ni kichwa cha biashara ila sasa hebu lete huo mzani nikifundishe kitu " .
Basi bwana mimi huyo na mzani mbaka kwa kiongozi wangu wa biashara tukaenda kwa mshikaji wake ukaurekebisha vizuri mzani " lengo, ni ili mzani uwe unawaibia kidogo wateja ( wale wanaofanya biashara za kipima pima watakuwa wananielewa vizuri hapa juu ya huu uhuni ). Basi bwana siku hazigandi biashara ikaanza .
Siku ya kwanza nilipiga maokoto vizuri kwani nilisukuma kama kilo 5 hivi plus watu kibao kuulizia ulizia ( moyoni nikajisema mambo si haya ) siku ya pili sukuma kilo zote 7 , ya tatu sukuma kilo 5 tena . Nikajisea " sasa hii biashara nshaijua vizuri hapa ili nikimbizane vizuri na hawa wateja ngoja nilete kilo 10 sasa, eehh hili eneo linataka kilo 10 " . Baada ya kuleta kilo 10 siyo mbaya nilisukuma kama kilo 6 hivi.
Lakini sasa balaa lilianza wiki ya pili toka nianze biashara eneo lile . Uwezi amini jumatatu ya wiki ya pili toka nilipoanzisha kijiwe nikiwa nimeweka kilo kumi kwenye kabati langu la kuhifadhia nyama . Alikuja bibi mmoja akipiga "" hodi hodi mwanangu , mimi sijambo bibi shikamoo bibi marihaba mwanangu . Mimi karibu bibi asante . Mwanangu nilikuwa naulizia kama nyama ipo ??."
Mmmhh mimi nikaguna nakujiuliza swali inamaana nyama yote hii kwenye kabati bibi haioni ??. Nikahitimisha kwa kujisemea mmhh japo wote tutazeka ila uzee mbaya sanaa. Oky bibi nyama ipo yakutosha kabisa kwani ulikuwa unaitaji kiasi gani bibi yangu ??. Bibi hapana nilikuja kwanza kuulizia kama ipo . Nakuondoka zake , nikiwatafakari kilichotokea tena kwenye saa sita vijana wawili kwa mbali wakiwa wanapita " oyii mwanangu,,,,,,,,,, vipi ?? Mie oiiii!! oiiii !!! oiiiii!!! poa wakuu vipi leo huna mzigo nini ?? Eehh nikayarudisha macho chap sandukuni kujilidhisha kama nyama ipo au haipo maana sielewi kwanini watu wananiuliza vile .. kucheki mzigo upo sasa kwanini naulizwa vile ??. Mzigo hupo tena wakutoshaaaa wazee huku nikitumia kidole changu kuwaoneshea mali iliyopo kabatini . Hinakwelee usiwaze jombaa tukipata mafekechee basi tutakuja kuchangamsha kijiwe . Amani amani wazee ntafurahi sana mkija.
Okay kumalizia tu wiki ile ilienda vile kwa kuulizwa kama nyama ipo na hata kwenye kuuza nyama ningeuza sanaa ni kilo 3 tu . Wiki ya tatu nilipoona hali imezidikuwa tete na tayari nimeshaingiliwa na hasara nusu ya mtaji wangu . Nikajisemea " bora nusu shari kuliko shari kamili acha nifikirie biashara nyingine huenda walimwengu wa huu mtaa hawajaipenda biashara niifanyayo nikafunga na kwasasa nipo nauza mafuta ya kupikia mtaa mwingine wale wote wenye connection nzuri ya wapi ntapata mafuta kwa bei chee tuchekiane nilipo dumu 80, 000/= ( huku tunapima kwa kilo na siyo kwa lita ) na lita moja wengi tunafanya 4500/=. Kwasasa