NHC: Hatujamuonea Mbowe

Hivi kwa nini nyumba nyingi za NHC wapangaji wake wa kudumu ni Wahindi na watu wenye uraia pacha.
 
Iloo shirika mbowe tuu ndo anadaiwa. Kama sio swala la kisiasa na wengine ambao hawalipi wawe ndani ya ccm au nje ya ccm wafungiwe pia.
 
Kama hadaiwi kweli ajitokeze kwa mbwembwe kwenye media kujibu,walewale wezi wakikaa bungeni wanashambulia taasisi za umma kumbe nao wanachangia kuzfilisi,Kibaraka Lissu ajitokeze sasa anye kama haujaanikwa mkataba wa hilo pango,bado sasa tunaenda kwenye swala la ukwepaji kodi kwenye hiyo kampuni na kina Protea hotel ndio atashikwa na kichomi,
 
Duh! Kumbe ni kwa sababu ya kupambana na Magufuli!? ina maana asingepambana naye basi NHC wasingetumika kisiasa!!! Kweli nduli wa visasi katinga nchini!
Je Mbowe anadaiwa kodi au hadaiwi??
Yeye ndo kila siku anatukana kufa kwa mashirika ya umma kumbe naye ndo mmoja wa wauaji wake wakuu.
 
Ukiishia kuandika hivyo huwezi kueleweka, hebu tuwekee in details ni namna gani hakufuata masharti-utuwekee mkataba baina ya hizo pande mbili na namna ulivyokuwa ukitekelezwa hadi kutokea yaliyotokea!
We hushangai kuwa Mbowe kakaa kimya sana??
NHC washatoa deatails za madeni.
Sasa ni zamu ya Mbowe kusema alilipa lini na wapi.
 
Hata kwa Lugumi na wakwapuaji wa UDA akina Salma na Ridhwan Kikwete hakuna siasa uchwara anatenda wajibu wake wa kujitoa sadaka ili kupambana na mafisadi.

Hakuna siasa hapo NHC wanafanya kazi Yao afu magu ajatajwa hata kidgo hapo
 
View attachment 391870
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limeeleza kuwa, hatua ya kufungia Kampuni ya Mbowe Hotels Limited (MHL) ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa si ya kisiasa,*anaandika Pendo Omary.

Leo NHC kupitia wakala wake Fosters Auctioneers (Sio Action Mark) wamevamia jengo lililopo kampuni hiyo katika makutano ya Mitaa ya Mkwepu na Indira Gandhi (Makunganya) jijini Dar es Salaam na kuchukua vifaa vya kampuni hiyo katika upande wa uzalishaji gazeti.

Hatua hiyo inatokana na madai kwamba, NHC inadai kampuni hiyo jumla ya Sh. 1.3 Bilion na kwamba, bado hazijalipwa mpaka sasa licha ya kutoa muda stahili wa kulipwa deni hilo.

Ndani ya kampuni ya MHL kuna Kampuni ya Free Media inayozalisha Gazeti la Tanzania Daima la kila siku.

Japhet Mwasenga, Meneja wa Kitengo cha Ukusanyaji Madeni katika Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) amesema, kuondolewa kwa kampuni ya Mbowe katika jengo hilo hakuhusiani na masuala ya kisiasa.

Mwasenga amewaambia waandishi wa habari leo mapema asubuhi wakati NHC ikisimamia shughuli ya uondoshaji vifaa kwenye jengo hilo kuwa “hiki kinachofanyia sio siasa. Hili sio suala la Mbowe peke yake. Ni suala la kiutendaji, pamoja na kwamba wadaiwa wako wengi, tumeamua kuanza na Mbowe.

“Tumefuata taratibu zote kumwondosha mpangaji wetu. Alishapewa taarifa na sisi kama taasisi ya umma, tuliendelea kumvumilia kwa muda mrefu lakini leo tumefika mwisho,” amesema Mwasenga.

Joshua Mwaituka, Mkurugenzi wa Kampuni ya udalali ya Fosters Auctioneers inayosimamia shughuli ya uondoshaji vifaa katika nyumba hiyo amesema, vifaa vyote vilivyondolewa vitahifadhiwa na kampuni hiyo mpaka hapo deni hilo litakapolipwa.

Source:
Mwanahalisi Online
Kwanini iwe sept mosi?
 
Wakuu salaaa

Huyu mkurugenzi ni jipu na ili sakata la mbowe ni kujikomba kwa wakuu wake lakini unajua nini unakifanya ,umekifanya na unaendelea kukifanya hapo NHC!!

Umeshindwa kujenga Nyumba angalau ya milioni 30,40,50 kwenye uongozi wako

Umeshindwa kuzikarabati Nyumba za NHC ingawa kodi unapokea kila siku!!

Kuna pesa za kodi za pango hazilipwi TRA Bali mnaziweka mfukoni !!!

Njoo kwanza mtuambie
Mikataba wa NHC na Ile foundation ya mke wa Kikwete mlipojenga magorofa ya Dodoma mliingiaje kwanini shirika LA Nyumba la taifa waingizwe watu wachache kumiliki share kama nani wao ?

Niko na mengi lakini ushauri hapa nataka Rais magufuli amchunguze huyu bwana ni jipu !!
 
Kodi anapokea kila siku kutoka wapi kama akina Mbowe wapangaji hawalipi kodi. Mlipeni hizo bilion then mtoe malalamiko kua hajengi nyumba
 
Mbowe alipe deni full stop.

Hela zote alizouza chama ametumia kuprinti t shirt za UKUTA ,huku akijua UKUTA haupo.!!

Waosha miguu wake mmeanza kutetea kwa ngonjera zisizo na kichwa wala miguu
 
Mmeanza majungu badala ya kumchangia Mwenyekiti alipe deni.

Mkizubaa hatua inayofuata ni kupiga mnada mali zake.
 
Back
Top Bottom