Pamputi
JF-Expert Member
- Apr 22, 2016
- 982
- 724
NHC wanataka kodi tu mengne umeongeza wewe mkuuTutasikia mengi mwaka huu, inaweza fikia ukitaka nyumba za NHC unaulizwa chama gani, Tanzania ni yetu sote
NHC wanataka kodi tu mengne umeongeza wewe mkuuTutasikia mengi mwaka huu, inaweza fikia ukitaka nyumba za NHC unaulizwa chama gani, Tanzania ni yetu sote
Duh! Kumbe ni kwa sababu ya kupambana na Magufuli!? ina maana asingepambana naye basi NHC wasingetumika kisiasa!!! Kweli nduli wa visasi katinga nchini!
Mpaka inafika B mlikua wapi?NHC ni jipu
Kwani ulitaka waenze na nani?Tunaishi katika jamii ambayo bado ni duni kivitendo na kifikra. Kwa vitendo kama hivi ni vigumu sana nchi hii kupata maendeleo. Tunaongelea nchi ya viwanda, hivyo viwanda vitajengwa na wanachama wa CCM pekee yao? Maana siamini kwa mtu ambaye siyo mfuasi wa CCM kama anaweza kufanya uwekezaji mkubwa usiohamishika kwa kipindi hiki kutokana na hofu inayojengwa.
Ni mjinga pekee yake atakayeamini kuwa limefanyika hili bila ya sababu za kisiasa maana hata maelezo yenyewe yapo wazi kuwa, 'tumeanzia na Mbowe ....', sababu za kuanzia na Mbowe hazikuelezwa.
Hiyo sentensi iko sawa kwasababu wameanza na kioo cha jamii...Sentensi yenye ukakasi wa kisiasa ni
"Wadaiwa wapo wengi, ila tumeamua kuanza na Mbowe"
View attachment 391870
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limeeleza kuwa, hatua ya kufungia Kampuni ya Mbowe Hotels Limited (MHL) ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa si ya kisiasa,*anaandika Pendo Omary.
Leo NHC kupitia wakala wake Fosters Auctioneers (Sio Action Mark) wamevamia jengo lililopo kampuni hiyo katika makutano ya Mitaa ya Mkwepu na Indira Gandhi (Makunganya) jijini Dar es Salaam na kuchukua vifaa vya kampuni hiyo katika upande wa uzalishaji gazeti.
Hatua hiyo inatokana na madai kwamba, NHC inadai kampuni hiyo jumla ya Sh. 1.3 Bilion na kwamba, bado hazijalipwa mpaka sasa licha ya kutoa muda stahili wa kulipwa deni hilo.
Ndani ya kampuni ya MHL kuna Kampuni ya Free Media inayozalisha Gazeti la Tanzania Daima la kila siku.
Japhet Mwasenga, Meneja wa Kitengo cha Ukusanyaji Madeni katika Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) amesema, kuondolewa kwa kampuni ya Mbowe katika jengo hilo hakuhusiani na masuala ya kisiasa.
Mwasenga amewaambia waandishi wa habari leo mapema asubuhi wakati NHC ikisimamia shughuli ya uondoshaji vifaa kwenye jengo hilo kuwa “hiki kinachofanyia sio siasa. Hili sio suala la Mbowe peke yake. Ni suala la kiutendaji, pamoja na kwamba wadaiwa wako wengi, tumeamua kuanza na Mbowe.
“Tumefuata taratibu zote kumwondosha mpangaji wetu. Alishapewa taarifa na sisi kama taasisi ya umma, tuliendelea kumvumilia kwa muda mrefu lakini leo tumefika mwisho,” amesema Mwasenga.
Joshua Mwaituka, Mkurugenzi wa Kampuni ya udalali ya Fosters Auctioneers inayosimamia shughuli ya uondoshaji vifaa katika nyumba hiyo amesema, vifaa vyote vilivyondolewa vitahifadhiwa na kampuni hiyo mpaka hapo deni hilo litakapolipwa.
Source: Mwanahalisi Online
Umejuaje kama hao wengine sio vioo wa jamii ..?!Hiyo sentensi iko sawa kwasababu wameanza na kioo cha jamii...
Alipe deni la pango na sio kutetea upuuzi kwa mgongo wa siasa...kama alipewa notisi kwa nini hakulipa...hii tabia yake ya udeni sugu hata NSSF anawasumbua...ngoja kesi ziishe mahakamani.Duh! Kumbe ni kwa sababu ya kupambana na Magufuli!? ina maana asingepambana naye basi NHC wasingetumika kisiasa!!! Kweli nduli wa visasi katinga nchini!
Umeota?Kwa Magufuli kila goti litapigwa.
Hata wakwepa kodi Chadema waliofukuzwa Leo billicanas ipo siku watatubu na kuachana na wizi wa kuwaibia watanzania.
Nashikwa kichefu chefu ufanisi wa watedaji wetu wansfanya kazi kwa mazoea kweli hadi inafikia B,halafu nakumbuka kaka yangu Mbowe maneno yake katika VililiMpaka inafika B mlikua wapi?NHC ni jipu
Wewe mwenyewe umewekezwa tu hapo ulipo. Unfukuze una nyumba wewe unayomiliki? Ushaacha kulala mitaroni na kwenye makorido ya wahindi?
Mbowe ni mdaiwa sugu!"Pamoja na kwamba wadaiwa wapo wengi, tumeamua kuanza na Mbowe"
Halafu anakataa hili sio suala la kisiasa.
Kwanini Mbowe?
Visasi vya mwendokasi hivo
Kwani ulitaka adaiwe lini? Umesoma habari vyema? Alipewa notisi ..Mbona mnajitetea sana ? Si kodi hajalipa na mnaweza pia kuthibitisha hilo ,Kelele za nini ? Mara hatujamuonea ,oh sio swala la kisiasa ,hata kama sio la kisiasa ,mmekosea timing huwezi kuniaminisha shinikizo la kisiasa halijatumika wakati ambao nchi ilikuwa kwenye homa ya Ukuta Mbowe akiwa ndio Captain