mkunga wa jadi
JF-Expert Member
- Jul 21, 2025
- 208
- 431
Unaweza kujiuliza Uingereza ipo wapi na inafanya nini, katika huu mgogoro mkubwa wa dunia, mwisho wa siku ukagundua kwamba “power” ya Uingereza ipo Google na magazetini.
Wakati Juha anaivamia Ukraine, Rais Macron alikuwa ni kiongozi wa kwanza duniani kulaani uvamizi ule, kusimama na Ukraine na kuagiza vikwazo vichukuliwe dunia nzima dhidi ya Urusi.
Uingereza sijui walikuwa bado wamelala fofofo.
Rais Macron, ambaye nyuklia zake ni za Ufaransa, tofauti na nyuklia za Uingereza ambazo rimoti ipo Marekani, Macron mpaka sasa ni kiongozi pekee duniani kutangaza vita na Juha.
Uingereza bado wapo katika usingizi mzito.
Kiongozi mkuu wa mazungumzo ya amani Ukraine kwa sasa ni Rais Emmanuel Macron. Misele mingi ya Rais Zelenskyy Ulaya ni hapa Paris ambapo analala mara kwa mara. Paris imekuwa Kyiv yake ya pili. Uingereza sijui wako wapi katika hili.
Wakati Juha na Trump wanapanga dili la kwenda kugawana Ukraine kule Alaska, kiongozi pekee duniani aliyepinga hilo dili ni Rais Macron. Akasema mazungumzo ya amani ya Ukraine hayawezi kufanyika bila uwepo wa Rais wa Ukraine ambaye Juha hajawahi kumtambua kisa kafyeka majeshi yake zaidi ya milioni moja Ukraine. Kikao kilifanyika Alaska lakini agenda ikabadilishwa, kufuatia moto wa Macron.
Bado namtafuta Uingereza katika hili.
Baada ya hicho kikao cha mchongo cha Alaska, Rais pekee duniani aliyepinga Rais Zelenskyy kupewa feedback ya kikao kwa simu, kama vile Ukraine sio nchi yake, alikuwa ni Macron.
Rais Macron ndiye alilazimisha kikao cha pili White House kati ya Trump na Zelenskyy na hakuishia hapo. Akaona ili yasitokee yale ya mwezi February kati ya Trump na Zelenskyy, akakusanya viongozi wote Ulaya kutoka Uingereza, Ujerumani, Italy, EU, etc. Wakaongozana wote White House kumpa kampani Zelenskyy.
Jamani, naanza kumtafuta Uingereza kwa tochi.
Ndani ya kikao hicho, Rais Macron akapendekeza nchi zote 32 za NATO zipeleke majeshi nchini Ukraine.
Jana dili limekamilika, Rais Macron amezikusanya nchi zote za Ulaya hapa Paris, nchi 26 kati ya nchi 31 zimeweka saini kupeleka majeshi ya ardhi, ya majini na ya angani huko Ukraine. Juha tayari ameanza kulia baada ya azimio hilo la Paris.
Hatimaye tochi yangu imezima chaji… Uingereza simuoni na siwezi kumuona tena.
Kuna watu humu, baada ya ku Google, wanakwambia eti “Uingereza ndio nchi kubwa kijeshi Ulaya.” Nguvu ya Uingereza mnaweza kuniambia ipo wapi katika yote niliyozungumza hapa?
Google hiyo hiyo inatufahamisha kwamba jeshi la Congo ni la 8 Afrika, jeshi la Rwanda ni la 42. Wakati dunia nzima imeuona ukweli hapo Congo.
Huwa nawadharau sana watu wanaofanya tafiti zao kupitia Google/Wikipedia, sijui nawachukuliaje yaani.
Wakati Juha anaivamia Ukraine, Rais Macron alikuwa ni kiongozi wa kwanza duniani kulaani uvamizi ule, kusimama na Ukraine na kuagiza vikwazo vichukuliwe dunia nzima dhidi ya Urusi.
Uingereza sijui walikuwa bado wamelala fofofo.
Rais Macron, ambaye nyuklia zake ni za Ufaransa, tofauti na nyuklia za Uingereza ambazo rimoti ipo Marekani, Macron mpaka sasa ni kiongozi pekee duniani kutangaza vita na Juha.
Uingereza bado wapo katika usingizi mzito.
Kiongozi mkuu wa mazungumzo ya amani Ukraine kwa sasa ni Rais Emmanuel Macron. Misele mingi ya Rais Zelenskyy Ulaya ni hapa Paris ambapo analala mara kwa mara. Paris imekuwa Kyiv yake ya pili. Uingereza sijui wako wapi katika hili.
Wakati Juha na Trump wanapanga dili la kwenda kugawana Ukraine kule Alaska, kiongozi pekee duniani aliyepinga hilo dili ni Rais Macron. Akasema mazungumzo ya amani ya Ukraine hayawezi kufanyika bila uwepo wa Rais wa Ukraine ambaye Juha hajawahi kumtambua kisa kafyeka majeshi yake zaidi ya milioni moja Ukraine. Kikao kilifanyika Alaska lakini agenda ikabadilishwa, kufuatia moto wa Macron.
Bado namtafuta Uingereza katika hili.
Baada ya hicho kikao cha mchongo cha Alaska, Rais pekee duniani aliyepinga Rais Zelenskyy kupewa feedback ya kikao kwa simu, kama vile Ukraine sio nchi yake, alikuwa ni Macron.
Rais Macron ndiye alilazimisha kikao cha pili White House kati ya Trump na Zelenskyy na hakuishia hapo. Akaona ili yasitokee yale ya mwezi February kati ya Trump na Zelenskyy, akakusanya viongozi wote Ulaya kutoka Uingereza, Ujerumani, Italy, EU, etc. Wakaongozana wote White House kumpa kampani Zelenskyy.
Jamani, naanza kumtafuta Uingereza kwa tochi.
Ndani ya kikao hicho, Rais Macron akapendekeza nchi zote 32 za NATO zipeleke majeshi nchini Ukraine.
Jana dili limekamilika, Rais Macron amezikusanya nchi zote za Ulaya hapa Paris, nchi 26 kati ya nchi 31 zimeweka saini kupeleka majeshi ya ardhi, ya majini na ya angani huko Ukraine. Juha tayari ameanza kulia baada ya azimio hilo la Paris.
Hatimaye tochi yangu imezima chaji… Uingereza simuoni na siwezi kumuona tena.
Kuna watu humu, baada ya ku Google, wanakwambia eti “Uingereza ndio nchi kubwa kijeshi Ulaya.” Nguvu ya Uingereza mnaweza kuniambia ipo wapi katika yote niliyozungumza hapa?
Google hiyo hiyo inatufahamisha kwamba jeshi la Congo ni la 8 Afrika, jeshi la Rwanda ni la 42. Wakati dunia nzima imeuona ukweli hapo Congo.
Huwa nawadharau sana watu wanaofanya tafiti zao kupitia Google/Wikipedia, sijui nawachukuliaje yaani.