News Alert: Dr. Maua na wazalendo wafanya kweli tena!

Tunayefanya naye kazi anatutia sana moyo. Maana haagalii saa wala nini ni mzigo tu. Ukichelewa kumpa update anakupigia kwanza wewe. Ana ku-update kazi ulizompa amefikia wapi kisha na yeye andemand umefikia wapi. Sometime ni vigumu kwenda na speed yake lakini tunaenda vizuri mpaka sasa.

Sasa kama kuna wivu basi ngoja tuwasikie . . .

Laiti hata asilimia 30 ya wateule wangekuwa kama yeye, tungepiga hatua....
 
Havina ubaya....
Cheki hapo mbele jinsi vilivyochongoka....

Kuna tatizo gani kuchongoka?
Yaani unashindwa kuangalia kitu muhimu kilichokuwa kinafanyika hapo wee unakalia kuangalia mavazi. Utasema sana lakini hiyo haitasababisha misaada kutokuendelea kutolewa. Big up TPN, Jamiiforums, Mwanakijiji, Michuzi na Watanzania wengine mlioguswa na matatizo ya wenzetu.
 
Bado tunasafari ndefu.. we are about to make a great leap. Siku moja tunaweza kujikuta kuhitaji msaada wa Red Cross. Sasa tuwasaidie mapema kabla hatujajiuliza "wako wapi"?
 
Wana JF naomba kujuwa kwa wale tulio nje ya nchi(Tanzania) michango(misaada)yetu tuipitishie wapi.
 
Kuna tatizo gani kuchongoka?
Yaani unashindwa kuangalia kitu muhimu kilichokuwa kinafanyika hapo wee unakalia kuangalia mavazi. Utasema sana lakini hiyo haitasababisha misaada kutokuendelea kutolewa. Big up TPN, Jamiiforums, Mwanakijiji, Michuzi na Watanzania wengine mlioguswa na matatizo ya wenzetu.

Ulikuwa ni utani tu. Sasa kama unaona nimekosea basi niwieni radhi.
 
Bado tunasafari ndefu.. we are about to make a great leap. Siku moja tunaweza kujikuta kuhitaji msaada wa Red Cross. Sasa tuwasaidie mapema kabla hatujajiuliza "wako wapi"?

Mkuu Mwanakijiji nadhani hili suala la Kuchangia Red Cross lingekuwa Endelevu especially kwa Nchi kama yetu ifikie mahala Red Cross iwe na Uwezo wa kutoa msaada wa Kiutu On time, na hili litawezekana tu kama watakuwa na Fund ambayo iko tayari katika account yao
 
Hafla ya Kukabidhi Misaada ya Wahanga Wa Mafuriko iliyokusanywa na TPN; Jamiiforums na Michuzi Blog kwa Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Tarehe 30-01-2010 katika ofisi za Chama Cha Msalaba Mwekundu; Masaki jijini Dar Es Salaam.


attachment.php


Rais wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN); Mzalendo Sanctus Mtsimbe; akitoa maelezo ya misaada iliyokusanywa katika awamu ya pili ya Kampeni kwa ajili ya kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko. Pichani ni misaada mbalimbali ambayo ilikusanywa na Wadau mbalimbali.



attachment.php



Mlezi wa TPN Mzalendo Maua Dfatari (kati); Mkurugenzi wa Maafa wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo na Rais wa TPN Mzalendo Sanctus Mtsimbe wakiteta jambo kabla ya hafla ya kukabidhi misaada katika Makao Makuu ya Chama Chama Msalaba Mwekundu; Masaki; Dar Es Salaam




attachment.php



Mlezi wa TPN Mzalendo Dr. Maua Dfatari (kati) akitoa maelezo kuhusiana na kampeni kwa; Mkurugenzi wa Maafa wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo (Kulia) katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Chama Chama Msalaba Mwekundu; Masaki; Dar Es Salaam. Mzalendo Daftari aliweka wazi kuwa Kampeni yetu ni ya Kukisaidia na Kukiwezesha Chama cha Msalaba Mwekundu Red Cross na haina uhusiano wowote na kampeni ya Red Alert inayoendeshwa na Vodacom ambayo hata hivyo wameiga kutoka TPN na Wadau wake baada ya wao kudokezwa kuwa tutaendesha kampeni ya jinsi hiyo. Alisema TPN imefurahi kuwa imetoa changamoto na sasa wadau mbalimbali wanasaidia na kuendesha kampeni kuwasaidia wahanga ingawa ilikuwa ni jambo jema kuunganisha nguvu kwani wote lengo letu ni moja. Aliasa kuwa Muhimu kuliko vyote ni kuhakikisha kuwa misaada inafika kwa walengwa. Kampeni yetu inaendelea kwa kutuma SMS yenye neon TPN kwenda namba 15522.



attachment.php

Rais wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN); Mzalendo Sanctus Mtsimbe; akitoa maelezo ya misaada iliyokusanywa katika awamu ya pili ya Kampeni kwa ajili ya kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko. Pichani ni misaada mbalimbali ambayo ilikusanywa na Wadau mbalimbali. Mz. Mtsimbe alisema hadi sasa zaidi ya watu 1880 wanachangia katika kampeni ya SMS. Vitu vilivyokabidhiwa ni pamoja na ndoo; magodoro; miswaki na dawa za miswaki; sabuni; vyandarua; mablanketi; maji ya kunywa; Nguo mbalimabli za kike, kiume,watoto, Mataulo, mashati, Suruali; Viatu na Madawa ya vyooni vyote vikiwa na dhamani ya TZS Million 5.






attachment.php


Mkurugenzi Mtendaji wa CAPS Limited na Mdau wa TPN Mzalendo Peter Marealle akikabidhi madawa ya choo kwa Mlezi wa TPN kwa ajili ya matumizi ya vyo vya Wahanga wa Mafuriko. Dawa hizi zinaua wadudu wote na harufu mbaya na hivyo kuzuia uwezekano wa magonjwa ya Kuhara na kipindupindu. Madawa hayo yana dhamani ya Zaidi ya TZS Millioni 1.3.





tunashukuru walau imefika.
 
Mkuu Mwanakijiji nadhani hili suala la Kuchangia Red Cross lingekuwa Endelevu especially kwa Nchi kama yetu ifikie mahala Red Cross iwe na Uwezo wa kutoa msaada wa Kiutu On time, na hili litawezekana tu kama watakuwa na Fund ambayo iko tayari katika account yao

ndege ya uchumi.. that is what I want on my part to do. lakini Red Cross siyo shirika la biashara ni lazima wapewe uwezo fulani. Na karibu sehemu zote duniani hutegemea michango ya watu, taasisi na vyanzo mbalimbali. Au unafikiria mkuu akaunti yao itatoa pesa wapi? Kwangu idea ya kutegemea wajomba zetu inanitisha sana siku moja.

Ningekuwa na uwezo ningeifanya Red Cross kuwa a parliamentary chartered entity na kila mwaka or so inapewa uwezo funding ya mambo ya maafa (say, 5 billion TS) kwa kuanzia na kupewa unhindered access to relief resources. Tutafika tu; kuna kitu tunakifikiria kukifanya kikiiva nina uhakika kitafanya juhudi zetu hizi kuwa endelevu zaidi.
 
ndege ya uchumi.. that is what I want on my part to do. lakini Red Cross siyo shirika la biashara ni lazima wapewe uwezo fulani. Na karibu sehemu zote duniani hutegemea michango ya watu, taasisi na vyanzo mbalimbali. Au unafikiria mkuu akaunti yao itatoa pesa wapi? Kwangu idea ya kutegemea wajomba zetu inanitisha sana siku moja.

Ningekuwa na uwezo ningeifanya Red Cross kuwa a parliamentary chartered entity na kila mwaka or so inapewa uwezo funding ya mambo ya maafa (say, 5 billion TS) kwa kuanzia na kupewa unhindered access to relief resources. Tutafika tu; kuna kitu tunakifikiria kukifanya kikiiva nina uhakika kitafanya juhudi zetu hizi kuwa endelevu zaidi.

My full support. A private motion to our parliament can do.
 
ndege ya uchumi.. that is what I want on my part to do. lakini Red Cross siyo shirika la biashara ni lazima wapewe uwezo fulani. Na karibu sehemu zote duniani hutegemea michango ya watu, taasisi na vyanzo mbalimbali. Au unafikiria mkuu akaunti yao itatoa pesa wapi? Kwangu idea ya kutegemea wajomba zetu inanitisha sana siku moja.

Ningekuwa na uwezo ningeifanya Red Cross kuwa a parliamentary chartered entity na kila mwaka or so inapewa uwezo funding ya mambo ya maafa (say, 5 billion TS) kwa kuanzia na kupewa unhindered access to relief resources. Tutafika tu; kuna kitu tunakifikiria kukifanya kikiiva nina uhakika kitafanya juhudi zetu hizi kuwa endelevu zaidi.
Mwanakijiji,
Red Cross hii ya Adam Kimbisa?
 
Hafla ya Kukabidhi Misaada ya Wahanga Wa Mafuriko iliyokusanywa na TPN; Jamiiforums na Michuzi Blog kwa Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Tarehe 30-01-2010 katika ofisi za Chama Cha Msalaba Mwekundu; Masaki jijini Dar Es Salaam.



attachment.php


Rais wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN); Mzalendo Sanctus Mtsimbe; akitoa maelezo ya misaada iliyokusanywa katika awamu ya pili ya Kampeni kwa ajili ya kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko. Pichani ni misaada mbalimbali ambayo ilikusanywa na Wadau mbalimbali.



attachment.php



Mlezi wa TPN Mzalendo Maua Dfatari (kati); Mkurugenzi wa Maafa wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo na Rais wa TPN Mzalendo Sanctus Mtsimbe wakiteta jambo kabla ya hafla ya kukabidhi misaada katika Makao Makuu ya Chama Chama Msalaba Mwekundu; Masaki; Dar Es Salaam




attachment.php



Mlezi wa TPN Mzalendo Dr. Maua Dfatari (kati) akitoa maelezo kuhusiana na kampeni kwa; Mkurugenzi wa Maafa wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo (Kulia) katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Chama Chama Msalaba Mwekundu; Masaki; Dar Es Salaam. Mzalendo Daftari aliweka wazi kuwa Kampeni yetu ni ya Kukisaidia na Kukiwezesha Chama cha Msalaba Mwekundu Red Cross na haina uhusiano wowote na kampeni ya Red Alert inayoendeshwa na Vodacom ambayo hata hivyo wameiga kutoka TPN na Wadau wake baada ya wao kudokezwa kuwa tutaendesha kampeni ya jinsi hiyo. Alisema TPN imefurahi kuwa imetoa changamoto na sasa wadau mbalimbali wanasaidia na kuendesha kampeni kuwasaidia wahanga ingawa ilikuwa ni jambo jema kuunganisha nguvu kwani wote lengo letu ni moja. Aliasa kuwa Muhimu kuliko vyote ni kuhakikisha kuwa misaada inafika kwa walengwa. Kampeni yetu inaendelea kwa kutuma SMS yenye neon TPN kwenda namba 15522.



attachment.php

Rais wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN); Mzalendo Sanctus Mtsimbe; akitoa maelezo ya misaada iliyokusanywa katika awamu ya pili ya Kampeni kwa ajili ya kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko. Pichani ni misaada mbalimbali ambayo ilikusanywa na Wadau mbalimbali. Mz. Mtsimbe alisema hadi sasa zaidi ya watu 1880 wanachangia katika kampeni ya SMS. Vitu vilivyokabidhiwa ni pamoja na ndoo; magodoro; miswaki na dawa za miswaki; sabuni; vyandarua; mablanketi; maji ya kunywa; Nguo mbalimabli za kike, kiume,watoto, Mataulo, mashati, Suruali; Viatu na Madawa ya vyooni vyote vikiwa na dhamani ya TZS Million 5.






attachment.php



Mkurugenzi Mtendaji wa CAPS Limited na Mdau wa TPN Mzalendo Peter Marealle akikabidhi madawa ya choo kwa Mlezi wa TPN kwa ajili ya matumizi ya vyo vya Wahanga wa Mafuriko. Dawa hizi zinaua wadudu wote na harufu mbaya na hivyo kuzuia uwezekano wa magonjwa ya Kuhara na kipindupindu. Madawa hayo yana dhamani ya Zaidi ya TZS Millioni 1.3.

Asante sana Mkuu kwa taarifa lakini hasa kwa kufafanua kuhusu Dk Maua Daftari kwamba ni mlezi wa TPN..niliposoma taarifa toka kwa Mwanakijiji I was asking myself why her yeye ni nani kwenye hii harambee mpaka yeye ndo akabidhi hiyo michango but nilivyosoma kwenye post yako chini ya Mwanakijiji nikapata jibu la swali langu.
 
Asante sana Mkuu kwa taarifa lakini hasa kwa kufafanua kuhusu Dk Maua Daftari kwamba ni mlezi wa TPN..niliposoma taarifa toka kwa Mwanakijiji I was asking myself why her yeye ni nani kwenye hii harambee mpaka yeye ndo akabidhi hiyo michango but nilivyosoma kwenye post yako chini ya Mwanakijiji nikapata jibu la swali langu.

GS tuko pamoja.

Ukipenda unaweza kuwa Mwanachama wa TPN. Karibu sana.
 
GS tuko pamoja.

Ukipenda unaweza kuwa Mwanachama wa TPN. Karibu sana.

Mimi ni mwanachama wa TPN but mwanachama mfu...nasubiri mpaka niwe na umri kama wako ndo nitakuwa active...teh teh teh..nipo kwenye mailing list yenu na huwa napata updated several times
 
Mimi ni mwanachama wa TPN but mwanachama mfu...nasubiri mpaka niwe na umri kama wako ndo nitakuwa active...teh teh teh..nipo kwenye mailing list yenu na huwa napata updated several times

Haaa haaa, OK GS; I am proud to see you at JF ingawa inasikitisha kuwa ni mwanachama mfu.

Nimeona GS ni Mgombea Mbunge Mtarajiwa. Tunakutakia kila la heri.
 
niseme nini miye; ninawashukuru kwa moyo wa dhati wote mliojitolea na mnaoendelea kujitolea. Unajua misaada inahitajika zaidi baada ya kamera na waandishi kuondoka kama tunavyoona kule Haiti. Linapotokea janga watu wanashtuka mara moja na kukimbia kusaidia lakini baada ya muda emotionally watu hawawezi kuendelea kuwa katika "high" for too long.

Matokeo yake ndio watu wanaanza kuzembea na kuchoka, na watu wengine hupoteza maisha baada ya janga lenyewe kutokana na matatizo yanayokuja baadaye. Hii ndiyo sababu ya kufanya kampeni hii kuwa more sustainable badala ya haraka ya wiki moja halafu tunajiondokezea.

Kama mambo yanaenda vizuri tunatarajia kufanya angalau awamu nyingine mbili au tatu hadi ifikapo mwisho wa harambee hii.

Matarajio yangu tutafikia Tsh milioni 300 hivi hivi!
 
Back
Top Bottom