Mbona linaelezeka kirahisi tu. Katika hali ya tukio hilo kuna uwezekano mkubwa kuwa kulikuwapo purukushani ya kujaribu kuzuia au kunyang'anyana hiyo silaha baada ya kumpiga mama mkwe. Purukushani hiyo inaweza kuelezea hiyo risasi ya begani. Baada ya huyo mwananume kupata tena udhibiti wa silaha yake, ndio akapata nafasi ya kumshambulia Ufoo na kudhani ameshawauwa wote wawili. Baada ya hapo, akajipiga risasi chini ya kidevu ili kujimaliza. Kama polisi wapo makini, sio kazi ngumu sana kubaini ni silaha ngapi/gani zilitumika katika tukio hilo. Hata hivyo, Ufoo anabaki kuwa shahidi muhimu sana katika tukio hili. Na ni kweli pia kuwa kuna uwezekano wa kuwepo kwa mambo mengi tu yaliyojificha kuhusiana na kadhia hii.