Ndugu wa 'mume' wa Ufoo waja na mapya

Ndugu wa 'mume' wa Ufoo waja na mapya

Marehemu kajipiga risasi mbili? Eti moja begani na nyingine kidevuni. Kama Polisi wetu wangekuwa sio wavivu wa kuchunguza,hapo kulikuwa na neno jipya na la kustua.

mama ake kapigwa risasi 5 very strangee
 
data unachanganyikiwa na nini sasa
Ngoja nimsaidie data...kachanganyikiwa na hizi habari gongana...mpaka zinatia hasira
We haupati hasira kuona leo hl kesho lile na pengine hakuna ukweli kati ya hayo yote...
 
Nimeipenda analysis yako mkuu. That is how a Great Thinker should look like!
Ninasikitishwa sana na vyombo vya habari vya Tanzania. Kwangu mimi nilipongeza hatua ya serikali ya hivi karibuni ya kuyafungua magazeti mawili ( sio mwana halisi) kwa matarajio kwamba wana habari wetu watafika sehemu waache "ukasuku"

kwa namna habari ya Ufoo inavyotangazwa, tunakubaliana kwamba ni mtu "maarufu". ndio sababu vyombvopvyote vya habari kwa muda wa zaidi ya wiki moja vimekuwa vikishindana "kutafuta" habari yake. Jambo la kushangaza vyombo vyote( naamaanisha vyote) vimeshindwa kwenda hatua zaidi na kubaki kuimba kama kasuku yale yanayosemwa na watu fulani. Mara polisi, msimaji wa Moi, ndugu wa ufoo au shemeji wa ufoo! tena kwa yale ambayo hao wasemaji wanataka yaandikwe!

kwanini vyombo vyetu vya habari vinavyoitwa huru (hata hizi Blog) vuimeshindwa kufika sehemu na kutueleza zaidi ya ngonjera ambazo zimekuwa zikielezwa nma hao wanaokaririwa navyo.

1. inaelezwa kuwa huyo anayedaiwa kuwa muuaji alitoka Sudan ya kusini na kwenda moja kwa moja kilimanjaro kuzungumza na mama yake kabla ya kurejea dar es salaam: waandishi wetu kwanini wamehsindwa kufanya jitihada za kumwuliza huyo mama ni kitu gani hasa kilichokuwa kinamtatiza mtoto wake? na alikwenda kwake kufanya nini?

2. inaelezwa kuwa baada ya kufika dar es salaaam, wawili hao walikuwa katika gari moja wakielekea nyumbani kwao ufoo na kuwa ufoo alimpigia simu mama yake kuwa aondoke nyumbani kwani huyo mzazi mwenzie angeweza kumfanyia kitu kibaya: waandishi wetu kwanini hatuwezi kuhoji ilikuwaje huyu aliyekuwa akiendesha gari apige simu kumwleza mama yake kuwa kuna hatari na huku akiendelea kuendesha gari kuelekea katika hatari yenyewe?

3. ndugu mmoja ndani ya nyumba ya akina ufoo amekaririwa akisema kuwa alimwleza mwenzake kwenda kuangalia huko sebuleni kuna nini wakati yeye akiendelea kubaki chumbani: waandishi, ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na watu watatu, kulingana na taarifa za huyu jamaa ambaye pia alisema mzazi mwenzake na ufoo alijipiga risasi na kufa na ninyi mkadandia hivyo je inawezekanaje mtu ajipige risasi begani halafu aji[pige kidebvuni, au ndio habari za utawala wa MOI ulotoa ttaarifa za uchunguzi wa kifo cha Dr Robert Auoko kuwa alijipiga risasi akafa halafu akachoma moto mwil wake?

4. kwa nini mmeammua kufanya ubaguzi wa waziwazi kwa mzazi mwenzake na ufoo kuonekan mkosaji ( kwa kuua) ilihali hamtaki kutwambia CHANZO HASA cha mzozo huo ni kitu gani? tunaelezwa kuwa huyo mzazi mweziwe na ufoo alikuwa pia mwana habari akiwa pia amepitia ITV kwanini kumbagua, au kwa sababu ufoo hushika mafungu ya mshiko kwa wanahabari wanaokwenda kwenye ziara za vyama vya siasa. Igunga!.

5. Nilikuwa najiuliza siku nyingi malengo ya wahariri wa ITV kupenda kumtumia zaidi Ufoo saro katika safari za wanasiasa hasa chadema, ingawa siku hizi kumekuwa na mabadiliko kuwa ni kutokana na weledi wake mkubwa zaidi katika siasa au kuna sababu nyingine, na katikakufanya hivyo walikuwa wakiangalia ambacho kingeweza kujitokeza?

6 waandishi wetu habari ikitoka kwenye gazeti la mwananchi ukurasa wa mbele itakuwa hivyo hivyo katika magezeti mengine bila kufanya kazi ya ziada, hata kwenda kwa watalaamu wa saikolojia kutoa ushauri wao wa nini kinaweza kufanyika kwa mtu ambaye anajikuta katika hali kama ya huyo mzazi mwenzake na ufoo.

vinginevyo niwape pole waliokutwa na janga hilo nikiwatakia wapumzike kwa amani( waliofariki) na kupona kwa haraka wale wanouguza majeraha pamoja na waliopatwa msongo wa mawazo. lakini waanndishi wetu mmeshindwa katika hili na mengine mengi kiasi imefika wakati hata humu ndani watu wana fahamu kitu wanaishia kueleza ile mimba au ile nyumba.

Ndio sababu ni rahisi zaidi kupata habari ya tanzania kutokea marekani kuliko kutokea Tanzania.
 
kazi kweli kweli. polisi nao watakuja na theory ya ajabu ajabu. Kosa la marehemu
 
Wote mnabwabwaja hamna idea yoyote na uchunguzi ngoja wataalam wafanye kazi yao na investigation itatoka tu
 
Mh,Ufoo kweli yamekukuta.uchunguzi wa polisi uwe wa kweli,kama Ana kesi ya kujibu apandishwe kizimbani na iwe funzo kwa wengine.

unadhani ufoo atasema ukweli wote? Hawezi maana Mushi amefariki hakuna atakayempinga tena na hakuna shuhuda mwingine.
 
Love ..!stupid undesirable feeling , yet we can't run away from it or let it go...!
 
Asilimia 99.9 ya wanaotaka kujiua kwa bunduki au bastola huwa wanaji renga kichwani. Na si mradi kichwani bali ni aidha juu kidogo ya sikio la kulia au kushoto,au chini ya kidevu. Lengo la kufanya hivi huwa wanataka risasi i/zikatishe uhai wao kwa haraka. Huyu aliyejirenga kwanza sijui mkononi nia take ulikua nini? Mwingine humu kasema eti alijipiga moja sikioni nyingine chini ya kidevu ha!,waulize wataalamu dunia nzima watakuambia hilo ndio kabisaa huwa haliwezekani. Only the truth will set you free so as Great Thinkers lets do Sherlock .H. thing here!
 
si kuna waliokimbilia darini?wataeleza aliyeanza kupiga risasi ni nani
Hivi dali ya hiyo nyumba ina ngazi kabisa za kupandia!!!?

Maana ninavyoelewa mimi nyumba nyingi za mjini zina ceiling boards. Halafu kwenye ceiling board inaweza kuachwa sehemu moja tu ambayo unaweza kuifungua kuingia juu dalini (mara nyingi hii huwa sebuleni), na ili kuifikia ni lazima uweke ngazi hapo.

Je hao vijana waliitoa wapi ngazi ya kupanda haraka haraka huku purukushani ikiendelea?

Je huko "walikokuwa wamejificha" kulkuwa na access ya kupanda dalini?

Maswali ni mengi sana....!

Hao vijana ni moja ya mashahidi muhimu sana katika hili sakata.
 
Hivi kwanini tusiangalie kwa mtazamo huu...kwani haiwezi kuwa jamaa baada ya wa kuwashoot wote akataka kujiua yeye kwa kujipiga risasi ya moyo ndio maana alijipiga kwenye bega la kushoto baada yakuona hajafanikiwa huko ndio maana akaamua kuamia kidevuni...mi naona ni possible
kwan wewe uwezi kujipiga risas ya mkono baadaye ya kichwa?
 
inachukua sekunde zisizopungua 3 paka 10 kama risasi imeingia sensitive area kama brain to make it cease functioning so majibu unayo mkuu.
Pili from the chin to the brain hapo kuikuta risasi kwenye ubongo tena kwa risasi ya bastola ni ngum kidogo mkuu sanasana iwe imepoison tu.nafikiri majibu unayo hapa mkuu

Learning never ends!!!!!

Lakini angekiwa na.capacity na ujasiri wa say kujipiga twice!!!!!

Mum cud only get one lethal shot and the injured wud be dead by now!!!!!

Was he gud enough to get himself two pins???!!!
 
Bila FBI au CIA, kazi bure. Wanatakiwa wafanye uchunguzi watu walio shiba.
 
Vibibi kama hivi hujifanya vinasalii we kutwa mara 3 kanisani kama dozi but vinajawa na dhulma mioyoni
 
ukweli anao ufoo,hatutakaa kamwe tujue exactly kilichotokea kwenye ile nyumba kibamba
 
Katika Bastola zinazomilikiwa kihalali,
% kubwa zinatumika kwenye issue za malovee zaidi kuliko kuulia majambazi, shame on you owners!!!
 
Kujipiga risasi sehemu mbili kwa anaetaka kujiua sio rahisi,nadhani wamemmachame huyo.
 
Back
Top Bottom