Ndoa yangu ipo ICU !dah

Ndoa yangu ipo ICU !dah

Mkuu pole sana....unavyoandika na maneno yako inaonekana unaumia vya kutosha....

Ndoa ngumu sana....but till when utaishi na haya maumivu kwa kudanganya unafuraha... binafsi ningekuwa mimi ili kupata uthibitisho nngechunguza mienendo yake vizuri... Kama ni spyware ningeweka kwa simu yake ili siku umfumanie vizuri na ukimfumania unakuwa mpole unamshukuru then unabeba wanako unaondoka nap..... Umri unamchanganya huyo nyumbu anaishi Maisha ya mtandaoni akifika tu 32 atakutafuta mkuu but pole sana mkuu
 
Mwanamke akishakwambia muachane hutakiwi kuendelea nae.
Huyo umaemuita mkeo ni dhahiri anamegwa kisela na Masela hapo Moro. Mpotezee mazima angalia watoto vinginevyo utaletewa UKIMWI uanze kumeza njugu-karanga kwa maisha yako yote yaliyobaki hapa duniani
 
Mkuu ufunge kwa ajili ya kupata relief
Pole sana! Fanya maombi ya kufunga kwa siku 3 ukiomba Mungu akuwezeshe kufanya maamuzi sahihi. Baada ya hapo fuata kile kitakachokupa amani ya moyo. Yawezakuwa kubaki na huyo mwanamke au kumwacha.
Ya asiye jali hisia za mwenz wake
 
BROTHER POLE SAAANA! NA MUNGU AKUTANGULIE....

NACHOWEZA SEMA JUU YA HILO NI KWAMBA..... UNATAKIWA KUTAMBUA VIZURI NAFASI YAKO NA WAJIBU WAKO KAMA MWANAUME KADRI YA MAAGIZO YA MUNGU....... NAFIKIRI UMEJISHUSHA SANAA KTK HILO.... MWANAMKE WAKO WA NDOA ANAINGIA KTK UASHERATI/UZINZI NA BADO UNAMVUMILIA, ISITOSHE AMESHAKUONESHA KILA ISHARA KUWA HANA HAJA NA WW ILA UNAKOMAA NAE..... WANAWAKE WANA UWEZO MKUBWA WA KUMCONTROL MWANAUME KIMWEMKO AMBAYO NDIO SECTOR KUU YA MAISHA.......NDIO MANA PIA WANAUME TUNAKUFA HARAKA.....

MWANAUME NI KICHWA KWA MAANA YA KIONGOZI, SS UKISHAONA HAYUPO TAYARI TENA KUONGOZWA PAMOJA NA JITIHADA ZA MSINGI BASI UJUE KABISA HUYO SI TAIFA LAKO TENAAA...

USHAURI WANGU:

1)
KAMA UNA IMAN THABITI KABISA KWA MUNGU MUUMBA KILA KITU, STICK IN PRAYERS KWA IMAN KABSAAA NA WALA USIJIHUSISHE NA NJIA ZAKE KABSA..... MPE UHURU ILA ULALE NAE KAMA DADA YAKO AU HAMA CHUMBA....... THEN MAJIBU UTAYAPATA SOON.

2)
ACHANA NAE CHUKUA WANAO LEA BAADA YA KUJADILI JAMBO HLO NA WAZAZ NA WADAU WENGINE WA NDOA YENU ILI UISHI KWA AMAN FROM THERE..........

NOTE:
UVUMILIVU BAADA YA JITIHADA UNA KIKOMO CHAKE...... UKIZIDI UTAKUFA MAPEMA SANA BROTHER.

MAISHA YAKO NA WAJIBU WAKO HAPA DUNIAN KADIRI YA UUMBAJI WA MUNGU NI MUHIMU SANA ZAID YA MTU AU KITU....................................... . SO BROTHER I WISH U ALL THE BEST.
 
Binafsi nipo kwenye ndoa takribani miaka mine na tumebarikiwa watoto wawili. Changamoto zilianza mke alipohamishwa kikazi mwaka juzi kutoka Dar kwenda Morogoro.

Kutokana na ukaribu nikawa najituma sana kutwa kwenda halafu isitoshe huyu mtoto wa pili alikua mwaka mmoja. Umbali ukasababisha mimi niwe mnywaji kidogo kuondoa upweke kuliko niwe nachepuka. Nikawa napunguza safari za kwenda weekend na yeye akazidisha mahusiano ya simu na mfanyakazi mwenzie(sijui kama walitembea ila nilijua wana uhusiano baada ya kunasa chat maana ilifika kipindi anajua weekend nalala ndo anakua busy kwa simu wakiongea na huyo mpaka nilivyombana na chats aka admit wanamahusiano via simu na huyo mtu yupo Dar).

Siku moja nikaenda Moro ghafla nikakuta anachat nae bado na isitoshe kuna mwingine wa Moro; nilimdunda hatari. Tukasuluhishwa na familia baada ya hapo kila tukikwaruzana kidogo anakimbilia kusisitiza tuachane yaani ndo ukawa wimbo.

Sasa nikaona kuondoa usumbufu na yeye kuhamia Dar aligoma kwa kusema maisha nafuu Moro nikatafuta kazi Moro nikahamia(nilipata kazi half the pay ya Dar) ila nilimweleza la msingi tuwe pamoja tuweze nusuru ndoa.

Sasa tangu tumeamua kukaa pamoja mambo hayajawa mepesi. Mimi na-cover basic needs kama kawaida yangu na napambana na biashara ila mwenzangu amekuwa amepotea kabisa kimapenzi. Tangu mwaka huu tunaweza kuwa tumesex si zaida ya mara 15 am sure maana mwenzangu hayupo kabisa anaona nimembana sana.

Kila kitu anatupia lawama nivomdundaga na matatizo ya nyuma. Nimejitahid kumpa space sana ila naona kitu kidogo anakimbilia kutaka talaka.

Sasa kilichonipelekea kuandika uzi huu ni majuzi nilimwambia naenda Dar maana alikua yupo moody sikujua ni sababu yangu au lah. Nikamwambia tu nina safari ya Dar week nzima; aisee alifurahii sana.

Safari ilikuwa ya siku mbili nikarejea jioni nikamtafuta kwenye simu akawa hapokei alivyotoka kibaruani. Jirani yetu ni mfanyakaz mwenzie akarudi tukapishana nikamuuliza vipi shoga yako akasema tumeachana amesema anapita sokoni mara moja (nikaona very rare kutorudi na shoga yake).

Wife akanitumia meseji akasema ametoka outing na shoga zake. Nikasema fine mimi nikanyuti nje mtaa wa pili kuona nani angerudi nae.

Kuna gari ikaja ikapaki kwa jirani ikakaa dakika kama 15 akashuka halafu gari ikaondoka. Alivyoingia ndani nami nikamfwata kwa nyuma
akashtuka sana. Nikamuuliza nani akasema rafiki yake tu walienda pata wine.

Nikamwambia naomba uwe makini tu kuna maradhi. Kama tumefikia huko naomba basi uwe na amani ufanye yako na si hapa kwangu na isitoshe tuna watoto wadogo usilete jazba kwenye haya mambo(maana tulivoingia ndani akaanza kuwaka kama simuamini alivyosema yupo outing nikamweleza outing sio issue ishu umetoka huko mkaweka kambi kwenye gari mie nawaona tu mnapiga story hamkumaliza huko outing)

Nimegundua hana mapenz kwa sasa na nimevumilia sana vituko vyake ila nawaza niwashirikishe wazazi wake na wadhamini wetu nataka niwachukue wanangu nirudi Dar nimpe nafasi tu.

Mkewangu ananiuma sana kila nikikumbuka nilivyompata, mahusiano yetu nk. Yeye ndo alikuwa kipaumbele kunitia sana moyo pale nilipokwama au kusita jambo(hii naandika kwa majonzi sana)

Umri wake haujazidi 30 bado na kuna muda naamini alingia ndoani akiwa mdogo sijui kuna mambo hajafanya? Ila mimi ni mtu wa kuwa huru sana namwambiaga nishirikishe nikupe kibali sina hiyana wala nini cha msingi ni imani tu kwamba hatavuka mipaka.

Suala la uwezo sijalitilia uzito maana yeye binafsi ana kazi na mshahara wake kwakweli huwa simgusiagi hata kidogo anafanya atakavyo. Mimi nina nyumba Dar ndo nimepangisha kuja kuishi naye huku. In short majukumu yangu nayajua na nayamudu.

Suala la kitandani lilikuwa zuri tu sote tunafurahi nk. Mwaka huu lilianza kususasua penzi la kubembeleza yeye ata enjoy ila mpaka nimemuandaa nimemconvince mbona shughuli.

Kwa upande wangu sio mnywaji sana na anajua. Nikinywa tu wine nikiwa nae ntajitahid kumueleza kiu yangu juu ya mambo ambayo hanitimizii hapo nae atarukia "si uniache"bas mkibishana atasema mlevi tatizo.

Weekend ndo tunakaa na kujadili mambo ila mara chache sana maana katikati ya wiki akirudi home yeye kachoka ni kula kulala tu.

Mimi ni mwanadamu pia naweza kuwa na mapungufuyangu ila all i know kuachilia mbali kila jambo nimekuwa nikijitahid kuomba msamaha ninapokosea nk.

Ndugu zangu ndo wanaona nimekamatwa kwelikweli ila nakuwa najitahid niishi ki maadili maana mke mwenyewe mmoja.

Nimesali sana mpaka nimeona kama ni watoto hata nikisema nimpotezee nitahitaji kuwaona wanangu ambapo itapelekea nimwone labda na yeye kitu ambacho mda mwingi kinaniwia ngumu kuvunja familia. Ila nikisema nibebe watoto(namjua kwa sasa majibu yake atasema nenda nao tu la msingi tuachaneee nk) nitabeba ila nataka niombe nisingependa kusikia pua yake na wakwe ndo watakua gia ya kuwaona. Ninataka full right ya wanangu nina uwezo wa kuwalea vizuri. Yani naumia sana ila naona ndo best option kwa sasa.

Naomba ushauri wenu wakuu
Pole sana kiongozi, umejitahidi sana lakini mwenzio kesharuka mdudu mbaya. Wewe umesema unasali, yeye pia anafanya hivyo?
 
We jamaa utakufa siku si zako, mwanamke hakutaki tena huyo bro. JIONGEZE au dalili zote bado huzioni?? Mkeo anagongwa na washkaji wengine na bila shaka atakua nao zaidi ya mmoja na kwa sasa haoni kama una umuhimu wowote kwake yaani kwa kifupi anakuona kama distraction tu kwake na mwanamke akifikia hatua hiyo hutakiwi kuendelea kujishikiza kwake na kama ukikomaa madhara yake yatakua makubwa zaidi ya haya. Unampenda ni sawa na wala hiyo si dhambi lakini isiwe pia kigezo cha kujimaliza mwenyewe, hao watoto usiwatumia kama kigezo cha kuficha udhaifu wako kwa huyo mkeo cha msingi we chukua watoto na ondoka kaanze maisha mapya tena usimwambie wapi unaelekea wala usiongee nae chochote kuhusu mipango yako na maisha yako baada ya kutengana nae we toa talaka na kamilisha taratibu zote za kisheri (usiangalie zitakugharimu nini hayo ni madude ya duniani na utayaacha humu) nenda kaanze upya kuliko kuendelea kuteswa na mtu ambaye mapenzi ya nje yamempofusha hata asijue kama anakutesa. MOVE ON NIGGA KUANZA UPYA SI UJINGA
 
Huyo mwanamke keshaliwa huko nje, mwanamke yupo tofauti na mwanaume kama sio malaya hawezi fanya mapenzi na mtu asiempenda kwaio kama keshatoa papa huyo keshampenda huyo wa nje kwaio anaona wewe ni kauzibe mwanamke akiwa na hawara hashindwi kukuua ili afaidi vizuri na hawara yake...niamini mimi
 
1) Mtafute anayekumegea umueleze ukweli kama ataridhia muachie aendeleze gurudumu.
2)kaa kiume usilie lie utapigwa makofi one day .
3) Ita wazazi plus viongozi wa dini msuluishe ikishindikana bwaga manyanga we sio wa kwanza kuachwa
 
Ila kweli dunia ina mengi, pole sana ndg yangu kwa magumu unayopitia, according to you, kama ni kusali ulishasali sana juu ya ndoa yako, kama ni msamaha ndio usiseme, huenda hata pale ambapo alikosea yeye msamaha uliomba wewe.

Binafsi bado naamini karata ya mwisho unayo wewe mwenyewe, maana hadi unaandika haya hapa hadharani mwanaume, natumai umepitia umepitia mengi magumu zaidi ya hayo uliyoandika.
 
Unajua nn kaka japo sijaoa. But nikwambie let her go.
Let her go man.. it doesnt worth it kuish na mtu ambar haoni dhamani yako.
Nikwambie tu ukiona mwanamke amefika mahali anadai tuachane.. thats it.. means ameshapata rebound huko nje.. so haoni umuhimu wako ndugu yangu.

My bet is kuna company mbovu inamuharibu, au bwana wa nje ana mzuzua na starehe zimemkamata.
Itisha kikao cha wazazi kama mlivyopanga, ili wazazi wamsikie mwenyewe kwa kauli yake kuwa hakutaki. After that kuwa na amani, chukua wanao nenda kawalee..

Trust atakuja one day. Tena ataanza kutuma ndugu kuja kuomba msamaha.
Aliniambia wewe saiz ndo wakumjua mungu
(Pindi namwambia tuombeane mema na mioyo yakufuta majonz niliyomsababishia kwenye kipigo)
 
Unacho experience kinaitwa emotional numbness. Nimeshawahi kupitia hii hali yaan hufeel chochote kabisa unatemveza dyu dyu tu. Hata ikitokea mwanamke anakupenda hufeel chochote.
Hii hali huisha baada ya muda fulani. Japo huchukua muda mrefu.
Nimshaur brother aondokea kabla hii hali haijampata maana ikija atatembeza dudu kila mwanamke anaepita mbele yake which is not a goo thing
kaka simama kama mwanaume, mimi nimevunja juzi tu hapa na toto la kizuru, sasa hivi yaani kwangu ni mwendo wa mbupu, nalala mbele hakuna mapenzi moyoni mwangu
 
Back
Top Bottom