Ndugu.Kwenye uchumi kuna kitu kinaitwa multiplier effect, kwanini iwe ndege na sio bandari, hoteli za kitalii, treni, kampuni ya TTCL nk. kwa mfano serikali imechukua asilimia 35 zilizokuwa zinamilikiwa na Bhatti ambao ni wamiliki wa Airtel waliokuwa wakiwa sehemu ya umiliki wa TTCL je ununuzi wa hizo hisa uliogharimu zaidi ya billioni 15 unakusaidiaje,
Kwa kesi ya ATCL pamoja na ukweli kuwa si watanzaniawengi wenye uwezo wa kupanda ndege hii haiondoi ukweli kuna faida kama wananchi tutaipata kwa mfano faida ya moja kwa moja miezi 2 kabla ya hizi ndege kuja shirika la ATCL lilitangaza nafasi za ajira takribani 18. japo sio wewe au bibi yako tayari kuna watanzania takribani 18 ambao watanufaika moja kwa moja, hawa watu watapata vipato ambavyo vitaendesha maisha yao yao ya kila siku na jamaa zao, fedha zao zotakuwa chanzo kwa wengine kupata riziki hiyo moja.
Kwa kuwa shirika ni la serikali, tunatarajia kupata kodi ambayo hulipwa na kila abiria anayesafiri, na kila ndege inapotua katika uwanja wa ndege kuna ada inalipia, kupitia hiyo serikali itapata fedha ambazo zitatumika kuagiza dawana bidhaa muhimu kama mafuta ambayo yanaleta bidhaa kwako na bibi yako. hiyo mbili
ya tatu kupitia sekta ya anga kuimarika kutapelekea sekta nyengine kama ya utalii kukuwa na hivyo kuongeza mapato ya kuja kujenga hiyo barabara, badala ya watalii kushukia nchini kenya na kupanda usafiri mwengine sasa watakuwa wanakuja moja kwa moja jambo litakalowapunguzia usumbufu na kuwavutia kuja kwa wingi, lakini pia sekta ya biashara za kimataifa itaimarika kwa kuwa na usafiri wa uhakika ambao wafanyabiashara wengi huzingatia katika kuhakikisha wanafanya biashara kwa wakati ili kuokoa gharama zinazoweza kuongezeka kwa kuwa na mfumo mbovu wa usafiri wa anga. hili litatupelekea kuongeza akiba ya kutosha ya fedha za kigeni ambazo zitasaidia katika manunuzi ya bidhaa na huduma nje ya nchi na kuimarisha shilingi yetu
Umeongea hoja nzuri ya multiplier effect lakini kwa ununuzi wa ndege the strength of multiplier effect ni ndogo sana ukilinganisha na sectors zeingine ulizotaja!
Kwa mfano, umetaja hatimae ATCL inaweza kuajiri wafanyakazi 18 kutokana na investment ya 61bn plus! Kwenye uchumi huko huko kuna kitu kinaitwa opportunity cost! Multiplier effect ya ununuzi wa ndege 2 itakuwa economically viable endapo no best alternative na hapa concentration ikiwa kwenye hiyo hiyo hoja yako ya multiplier effect.
Ona sasa, multiplier effect yako imeanzia kwa wafanyakazi 18... and it's true, itaanzia hapo! Kinyumee chake, tuchukue sekta moja wapo ya ulizotaja... bandari. Assume pametokea upanuzi. Kwanza kabla ya kuajiri hao wafanyakazi 18; kwenye upanuzi wa bandari utaanza na ununuzi wa sement, nondo, misumari na makororokoro mengine! Hivyo ndivyo hiyo 61 billion itakavyoanza kuwa multiplied kwamba viwanda vyote hivyo vita-pool in revenues from hizo 61bn. Baaada ya hapo, kutakuwa na magari kadhaa yatakayosafirisha hivyo vifaa kwenda bandarini... magari yatakuwa yamejazwa mafuta hapa na pale... mulitiplier effect inaendelea hapo!! Vifaa navyo vitakuwa vimepakiwa kwenye magari na vibarua ambao nao watalipwa ujira na kwenda kula mama lishe, kununua maji ya kunywa, kununua sigara n.k... hiyo ndiyo multiplier effect! Vifaa hivyo vikifika bandarini vitapakuliwa tena na vibarua na kutokea yale yale ambayo yalitokea viwandani... hiyo ndiyo multiplier effect!
Hapo bado hata ujenzi haujaanza lakini angalia 61 billion investment ilivyoathiri economic activities positively!
Ujenzi ukishaanza, hapo tena kutakuwa na vibarua, wauza vyakula, wauza maji n.k! Hiyo ndiyo multiplier effect. Ujenzi ukishakamalika ndo watu wanaanza kufikiria suala la wafanyakazi wa kudumu wakati hiyo 61 billion imeshakuwa reflected in the economy from day one! Na kama itakuwa umejenga container terminal, hapa tena tunatarajia vibarua wa kumwaga, tunatarajia magari yakayoleta na kufuata mizigo ambayo nayo yatakuwa na madereva na matingo... magari ambayo nayo yatakuwa yameshakunywa mafuta ya kutosha na hivyo kuendeleza biashara za wauza mafuta ambao nao watakuwa wanahakikisha ajira za wafanyakazi wao... mlongo mlongo ni mrefu!
Now tell me kwenye hizo ndege katika taifa ambalo lina limited resources ambazo, from economic point of view, hapo unatakiwa ku-invest kwenye the best alternative!