Ndani ya CHADEMA: CCM anaingia, CCM anatoka

Of course kwa mfumo wa siasa na uchaguzi uliopo sasa, ni vigumu kwa chama tofauti na CCM kushika dola! Utashindanaje na chama dola kweli?

CCM kama ina ubavu, iache mazingira ya ushindani yawe fair na transparent! Halafu tuone kama unaweza kusema ulivyosema.
licha ya hivyo ukweli unabaki, chadema haipendwi kama mnavyodhani humi ktk mitandao ya kijamii.
 
Usiogope, nimesema ni wajinga tu wanaofikiri chadema hii itashika dola, wewe unaamini na kufikiri hivyo, kwa hiyo upo kwenye kundi la niliosema hapa.
Usitoke povu.
Uki argue na mpumbavu mara nyingi silaha yake ni kukupandisha hasira ili akushushe mlingane then lecture yake ikuingie...nakutakia maisha marefu ili ushuhudie kiama cha chama cha babu yako ambacho kimekosa sera na viongozi wake wamefilisika kifikra wakitegemea kauli za kimahaba tu kwa aliyewateua ili waendelee kujaza matumbo yao!
 
Nilisikia kuwa CDM kinaendeshwa kama corporate entity - kibiashara.

Sasa katika mikakati yao (short-term na long-term) ya kudhika dola, pengine hizi transactions tunazoziona ni sehemu yake tu.

Pengine CDM inawakaribisha wanaotoka CCM. Baada ya kuwapika vizuri wanawaachilia warudi CCM kutimiza mikakati hiyo mikakati yao.

There might be some genius in this madness.
 
Ni mjinga tu anayefikiri chadema hii ya sasa itakuja shika nchi, wameongeza flava tu ktk chaguzi kuisindikiza sisiemu.

Kuwa mkweli; hakuna CHADEMA ya wakati wowote ule inayoweza kuachiwa ishike nchi. Haikutokea huko nyuma wala haitatokea nyakati zijazo hata CHADEMA ikiwa na umaarufu mara dufu ya iliyokuwa nao enzi za Dr. Slaa. Kauli ya Bulembo ndiyo sahihi Mpaka keshokutwa.
 
Haki kweli kabisa....

ukimrudisha Dokta Slaa leo kwa Ufalme huu unaotawala. Asingefanya Lolote la maana.
Mark my words...heri tumwache auze Supermaket uko canada. Manake ya huko yanaweza mshinda anytime..tena Sijui kwanini watu wanamkumbuka quiter aliekimbia changamoto?!!.

Yule alikua dhahifu kuliko Lowasa. Ndio maana alishindwa Siasa.
Huwezi kua Imara kisha akaja mtu mgeni nyumbani kwako akakutoa. Kisha ukaendeleea kujiita kuwa wewe ni Imara.?!!its absurd!!.

Dk. Slaa, Ameshindwa kilakitu katika maisha yake:-
1. Upadre..Kanisa katoliki lipo palepale bila dokta slaa.

2. CCM:-/tena ndio imekua mbaya kuliko ya JK.
3. CDM tena imekua inaogopwa na chama Tawala kuliko Ya enzi zake ikiwa na wabunge wengi na rekodi kubwa kuliko zote katika matokeo ya Uraisi tangu vyama vingi vianzishwe... Kelele za kuondoka kwake hazikuzuia watanzania kuwaunga mkono wapinzani.


Nitasema Kweli Daima.
Fitina kwangu Mwiko..
Siitashangaa nikisikia Dokta slaa akikimba na kuacha supermarket kwa madai hakukua na haki katika bei za mauzo na wateja huko Canada ameshindwa kuelewana na meneja. Kwa umri ule anything can happen.

Alishindwa kuthibitisha kua Kanisa katoliki lilihongwa na shahidi yake akawa mshenga Gwajima. Gwajima alimkatalia na akapiga double manifestation. Na akamwambia kama yeye slaa ni Mwanaume, ajibu. Slaa alipoona hali mbaya akakimbia bila kutolea ufafanuzi maelezo ya Gwajima.

Juzi gwajima alipokamatwa na serikali kwa kutajwa kwenye sakata la madawa ya kulevya. Slaa akaamua kumtumia slamu za Pole Gwajima. Na kujikomba kua anamfahamu gwajima wanamuonea. Nashangaa hakuna chombo cha habari kilichoonyesha doubt maneno yake...
Jinsi ninvyomuelezea nazidi kuona haina maana kumwita dokta... Aitwe slaa tu. Ndio jina linalomfaa.
Anaogopa hata kumpa Pole tindu lisu..yule ni puppets. Nuff said..
Hizi story za Gwajima sielewi hata zina uhusiano gani na nilichozungumza Slaa,Zitto walikuwa puppet but walikuwa na mchango mkubwa kwenye upinzani kuliko hawa kina Sumaye au Lowasa
Sishangai now mchango wa Dr Slaa hauonekani but alifanya kazi kubwa sana ndio maana hata huyo Mbowe unayemsifia hajawahi kumponda Dr Slaa,
 
Nilisikia kuwa CDM kinaendeshwa kama corporate entity - kibiashara.

Sasa katika mikakati yao (short-term na long-term) ya kudhika dola, pengine hizi transactions tunazoziona ni sehemu yake tu.

Pengine CDM inawakaribisha wanaotoka CCM. Baada ya kuwapika vizuri wanawaachilia warudi CCM kutimiza mikakati hiyo mikakati yao.

There might be some genius in this madness.

So what are you saying, sir?

That there is a [scientific] method to all this madness that's going on?
 
Huu mjadala ni mzuri. Mimi binafsi nilivutiwa na “brand” iliyotengenezwa na CHADEMA enzi zile dhidi ya ufisadi ikiwa na timu ya mashambulizi isiyo ya umaarufu wa mtu mmoja pekee.

Nadhani CHADEMA walidanganyika baadaye kudhani kushindwa kwao kuingia ikulu kunatokana na kukosa mshika bendera maarufu kama EL. Kumbe tatizo ni udikteta kamili wa CCM. Na EL alidanganya kuwa anaweza kuizima jeuri hiyo ya CCM.

Sasa imebakia kuwa porojo tu; hakuna cha ikulu na “brand” inazidi kupauka. Tunabakia na mazoea ya kuipenda CHADEMA kwa vile bado ndiyo ngome pekee imara dhidi ya ubaradhuli wa CCM. Bado wako akina Lissu & co. Lakini CCM sasa imeamua kutumia hoja ya bastola waziwazi.
 
Hizi story za Gwajima sielewi hata zina uhusiano gani na nilichozungumza Slaa,Zitto walikuwa puppet but walikuwa na mchango mkubwa kwenye upinzani kuliko hawa kina Sumaye au Lowasa
Sishangai now mchango wa Dr Slaa hauonekani but alifanya kazi kubwa sana ndio maana hata huyo Mbowe unayemsifia hajawahi kumponda Dr Slaa,

Nimemtaja Gwajima ili kuunganisha Doti na kuelewa behavior ya Slaa.
CCM ni kama Nyati(Mbogo) aliyejeruiwa na Simba.

Tena ukiunganisha na hulka na Matendo ya mtawala aliyepo mwenye hasira kuona CCM inazidi kupoteza majimbo. Nia yake ifikapo 2020 arudishe majimbo yote chini ya CCM.

Zama za Slaa, yeye ali operate zama za Jk aliekua akiwapa leisure fair nyingi sana. Walikua wanaitukana serikali na kuikosoa hadharani bila hofu ya kukamatwa. Jk alikua anawaruhusu anawakaribisha ikulu na kuzungumza nao.

Huyu mfalme aliepo madarakani alishasema hajaribiwi...ukimkosoa kama hujafichwa unapigwa hata risasi tu.

Kila mwenye macho anaona wazi kua:- utawala wa sheria haupo nchini.

So Swala hapa sio Slaa wala lowasa.

Swala hapa ni mfumo kandamizi wa utawala uliopo madarakani umejipanga kupambana na ukosoaji wa aina yoyote.
Mtawala ameshajipambanua waziwazi kua yeye hashauriwi na ni mtu na anajiamini..


Kwa mfano:-
Kupiga marufuku mikutano ya kisiasa mpaka 2020.
Hapa hata angerudishwa Dr.slaa ataishia kukaa kimya mpaka uchaguzi ufike ifikapo 2020.

Wakati wa uongozi wa kidemokrasia wa JK, Slaa na timu yake walifanya mikutano muda wote, kama sehemu ya kazi waliojiajiri.

Ikawa Ndio chanzo cha CDM kuiteka Jiji la Mbeya na kujitanua maeneo mbalimbali nchini kuweka matawo yao.
Cdm walianzisha m4C na harakati mbalimbali zilizoweza kuwafikia wananchi.
Lakini zamu hii hawaruhusiwi kufanya siasa.

Iwe kwa Kuandika Gazetini, mtandaoni, bungeni wala Barabarani.
Sasa unapo fanya comparisoni.
Unakuta mtukufu hata mikutano ya kiserikali anafanya Siasa.anatamba.
Akienda jimbo la mpinzani, akialika wenyeji wa hapo. Utakuata Hapokei wapinzani kabisa. amewafanya wapinzani especially CDM kua ni maadui zake.
Alipotoa ripoti ya mwisho ya Bunge kuhusu tanzanite. Ndani alikuwepo Mbowe kama kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani. Lakini alionyesha kuwashukuru wapinzani akamtaja lipumba na John cheyo(mtu wa mwanza) ambaye hata chama chake hakijulikani tena hapa nchini.

So
Ili kubalance equation:-

Ni lazima uangalie nani amevuna makumi elfu wakati mfupi?. Jibu ni lowasa pekee. Kwasababu impact ya Lowasa ilitingisha chama cha CCM nje na ndani.
Wakati Slaa aliweza kuitingisha nje tu.after many years of stuggle. Kwa maneno mengi na maelezo yaliojaa kiroba.wakti kwa ndani CCM ilikua imara sana.
Lowasa alipohama tu. Pale Shinyanga Wanccm 200 walihamia Cdm.
Pale Arusha ofisi za CCM zilifungwa.
WanaCCM wengi sana walihama chama chao.

Mchango wa lowasa na Sumaye ni mkubwa zaidi kihistoria. Na utabaki kua hivyo.

Matokeo ya uraisi ni Ushahidi tosha kua Lowasa ana mchango mkubwa kuliko wapinzani wengine wote. Number don't lie.
.
It is either half full glass or half empty glass..
 
Naamini, hata waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hawakulenga kinachotokea sasa. Akina Mzee Edwin Mtei, kama waanzilishi walilenga kuifanya CHADEMA iwe chama imara na mbadala. Si sehemu ya kutambia watakavyo wanaCCM.

Kwa uelewa wangu, waanzilishi wa CHADEMA walipanga na kufanya mpango wa kuijenga kwa kutafuta wanachama na hata kuandaa viongozi wa baadaye nje ya CCM. Wanachama walipaswa kusakwa, kulelewa na kukomazwa humo. Ni katika mfumo wa walivyopatikana akina Zitto na Mnyika.

Hivi sasa, mambo yamekuwa tofauti. CHADEMA sasa imekuwa sehemu salama kwa wahamiaji na wahamaji wa CCM. WanaCCM sasa wanahamia na kuhama kadiri watakavyo ndani ya CHADEMA.

Ingekuwa kwenye uga wa masuala ya kodi, CHADEMA ingekuwa ni tax haven. Sehemu salama na ya kukimbilia kujificha.

Anaingia Lazaro Nyalandu, anatoka Laurence Masha. Anaingia mwanaCCM, anatoka mwanaCCM. Viongozi na wanachama wa CHADEMA wanajifariji kwa kusema kuwa eti chama ni watu! Nawahakikishia, wanaCCM watahamishia hata makundi yao CHADEMA. Wataanza kupigana vikumbo kama wapo kule.

CHADEMA, rudini kwenye misingi yenu. Sakeni wanachama wapya bila kusubiri wahamiaji na wahamaji wa CCM. Mkiendelea hivi, mtachaguliwa viongozi na kupangiwa cha kufanya na wanaCCM. Hamtaepuka kuwa CCM B. Msifanye chama chenu tax haven!
We we ulizaliwa 1999 au? Wooote tulikuwa ccm kabla ya 1993 mfumo wa multi party ulipoanzishwa, sasa sijui umeandika utumbo UPI !!!!!! Katiba na sheria za nchi je zinaruhusu? Poorly mind!!!!;;;;
 
So what are you saying, sir?

That there is a [scientific] method to all this madness that's going on?
We are talking about Master of industry and corporate strategies here Sir. One, and only Aikaeli Mbowe.

Leader extraordinaire of scores of professors, lawyers, political scientists, tycoons and millions of graduates.

No madness here my friend, just pure, unadulterated METHODS.

Hail to the Chief.
 
Naamini, hata waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hawakulenga kinachotokea sasa. Akina Mzee Edwin Mtei, kama waanzilishi walilenga kuifanya CHADEMA iwe chama imara na mbadala. Si sehemu ya kutambia watakavyo wanaCCM.

Kwa uelewa wangu, waanzilishi wa CHADEMA walipanga na kufanya mpango wa kuijenga kwa kutafuta wanachama na hata kuandaa viongozi wa baadaye nje ya CCM. Wanachama walipaswa kusakwa, kulelewa na kukomazwa humo. Ni katika mfumo wa walivyopatikana akina Zitto na Mnyika.

Hivi sasa, mambo yamekuwa tofauti. CHADEMA sasa imekuwa sehemu salama kwa wahamiaji na wahamaji wa CCM. WanaCCM sasa wanahamia na kuhama kadiri watakavyo ndani ya CHADEMA.

Ingekuwa kwenye uga wa masuala ya kodi, CHADEMA ingekuwa ni tax haven. Sehemu salama na ya kukimbilia kujificha.

Anaingia Lazaro Nyalandu, anatoka Laurence Masha. Anaingia mwanaCCM, anatoka mwanaCCM. Viongozi na wanachama wa CHADEMA wanajifariji kwa kusema kuwa eti chama ni watu! Nawahakikishia, wanaCCM watahamishia hata makundi yao CHADEMA. Wataanza kupigana vikumbo kama wapo kule.

CHADEMA, rudini kwenye misingi yenu. Sakeni wanachama wapya bila kusubiri wahamiaji na wahamaji wa CCM. Mkiendelea hivi, mtachaguliwa viongozi na kupangiwa cha kufanya na wanaCCM. Hamtaepuka kuwa CCM B. Msifanye chama chenu tax haven!

Umetumia vipimo/vigezo gani wewe "wakili msomi" kufikiri, kuandika na kuja na hitimisho la namna hii?

Nadhani ktk mada zote ulizowahi kuposti, hii ni mojawapo ya mada zako nyingi dhaifu zisizofanyiwa utafiti wa kutosha kabla ya kuiachia iruke hewani...

Nakuambia hivi kwa sbb zifuatazo:

Mosi, ni makosa kuilinganisha CHADEMA ya sasa na kizazi hiki na NCCR Mageuzi ya kizazi kile na ya wakati ule kwa sbb ya wakati...

Kwamba, hata hutambui kuwa, time changes na watu Siku zote hujifunza na hubadilika pia kimbinu, kimkakati na kimaono.....

I'm not sure kama wewe unaamini kuwa makosa waliyoyafanya NCCR Mageuzi yaweza kufanywa na CHADEMA hii ya siasa za kisasa ya kizazi cha dot.com...

Kama unadhani Magufuli huyu mshamba wa mikakati ya kisiasa za kileo aweza kuua siasa za vyama strong vya upinzani, nakushauri urudi chumbani mwako ukae na ufikiri tena mara mbilimbili, kisha njoo tena uandike upya...

Pili, hebu rudi nyuma kidogo miaka 8 au 10 nyuma wakati wa JK.

Una reflect kitu gani?

Yawezekana umesahau. Naomba nikukumbushe.....

Kwamba, huko kwenu CCM ndiyo ilikuwa rising generation ya kina Mwigulu Nchemba chini ya katibu mkuu wake Wilson Mkama na yule mzee wa fitna Steven Wassira a. k. a Tyson....

Ndicho kipindi ambacho kauli kalikali kabisa kuliko hii yako kuwa, CHADEMA by 2013 ama 2015 ingekuwa ni historia kabisa....yaani ingekufa kifo cha mende!!

Haikuwa inaeleweka exactly, walikuwa na mikakati gani ya kuua.

Labda kupitia njia za kina Mwigulu Nchemba kuandaa video za kigaidi kwa ambazo in return zili back fire vibaya sana....

Do you remember, what happened eventually? I hope, jibu unalo ktk mtima wako....

Lakini kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sawa, ngoja nikukumbushe....

Wakati majigambo haya ya kuua vyama mbadala hususani CHADEMA kabla ya 2010 na baadaye wakaja kubadilika na kuwa itakufa kabla ya 2015....

Kumbuka wakati huo CHADEMA ilikuwa ina wabunge wasiozidi 42 na wakati huohuo wakiongoza baadhi ya halmashauri kadhaa kama tatu ama tano hivi nchi nzima...

Hayawi hayawi uchaguzi mkuu 2015 hip ukafika.....

Unajua matokeo yake?

For the first time ever in its history, CHADEMA ikatoa upinzani mkali kupita kipimo cha CCM ktk kinyang'anyiro cha uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani....

For the first time ever, CHADEMA pamoja na mfumo mbaya wa uhesabuji kura za urais chini ya NEC - CCM sambamba uchakachuji (wizi) ikapata kura za urais karibu 7,000,000 tofauti ya kura karibu 1.5m tu za mshindi wa CCM.....

For the first time ever, CHADEMA ikashinda majimbo ya ubunge mengi zaidi na kupata wabunge mara mbili kuliko wale ktk uchaguzi uliopita i. e 2010....!!

For the first time ever, CHADEMA sambamba na vyama washirika wenzake wa UKAWA ikatwaa na kuongoza halmashauri nyingi zaidi kuliko ktk uchaguzi uliopita wa 2010 likiwemo majiji matatu DSM, Mbeya na Arusha....!!

Ndiyo for the time ever CCM Zanzibar inashindwa mchana kweupe na CUF ktk sanduku la kura na kwa ubabe wa kijeshi inapindua matakeo na kuzua mgogoro wa kikatiba mpaka leo...!!

Kwa maelezo haya, ndiyo maana nimetangulia kukuuliza umetumia vigezo gani kuja na post dhaifu wewe "verified user" kabisa yenye conclusion ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia wa mambo?

Je, ni kwamba unataka kuanzisha kauli zile za miaka ile za akina Mwigulu Nchemba na akina Steven Wassira za kwamba watauteketeza upinzani kabla ya 2010 na baadaye wakageuka ikawa kabla ya 2015?

Je, ni kwa sbb baadhi ya wanaCCM wanaachana na chama chao na kujiunga na upinzani hususani CHADEMA?

Alaa, sasa hii yaweza kuwa sbb kweli ya kuiona CHADEMA kuwa inakosa mwelekeo? Kwani ni wanaChadema wangapi wangapi wanakwenda CCM bwana? Je, ndiyo tuseme kuwa CCM inakosa mwelekeo kwa sbb wanapokea wanachama toka CHADEMA??

Mimi, sikubaliani na wewe kwa sbb inaelekea hata hujui CHADEMA inaingiza wanachama wapya wangapi kila siku. Na likely huna ufahamu wa mikakati waliyo nayo hawa jamaa kukabiliana na CCM iliyokwisha kufa chini ya Magufuli....

Mimi ninakuhakikishia, 2020 itakupa majibu kuwa your perception kuhusu CHADEMA na upinzani kwa ujumla is wrong kwa matokeo ya uchaguzi huo....!!

Ushahidi mwingine ulio wazi kuwa CCM hii chini ya Magufuli ni mfu, ni jinsi tu wanavyoendesha mambo yao na nchi kwa ujumla....

Wanatumia nguvu kubwa kuliko akili. Wanajihami zaidi kwa kila kitu kuliko kuonesha jinsi wanavyotekeleza mipango na sera zao....

Huu ni ushahidi dhihiri kuwa, CCM imekabwa koo kuliko udhaniavyo. Angalia tu ujinga wanaoufanya dhidi ya Lazaro Nyalandu yaani utadhani huyu jamaa ni mwizi na fisadi kuliko hata John Pombe Magufuli mwenyewe....kitu ambacho ni kinyume chake...

Wanafanya yote haya wakiwa na akili na fikra kama zako, kwamba watanzania wa leo ni wajinga jinga tuuu sawa sawa na wale wa miaka ya 1995 enzi za NCCCR Mageuzi ya akina Agustino Lyatonga Mrema...!!
 
Sikio la kufa ....Mbowe ndiye mtu anayepaswa kujitafakari binafsi na kuchukua maamuzi magumu ...tusisubiri ya NCCR mageuzi maana naona kabisa Chadema inaenda shimoni na hasa moto utaanzia uchaguzi wa 2020 ....bado mapema kujipanga upya .....
Mkuu I assure you CHADEMA Haiwezi kurudi kuwa kama enzi zile.
 
Katika ufuatiliaji wangu wa siasa za Tanzania nimegundua kuwa kuna sababu kubwa ya kusema wapinzani wanafeli a big time. Turudi nyuma tangu tangu kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 kumekuwa na wimbi kubwa la kuhama kwa baadhi ya watu maarufu kutoka chama kimoja kwenda kingine.
Imekuwa ni desturi kwa upinzani kukaribisha watu kutoka chama tawala na kusema kuwa ni haki yao kikatiba kuhama chama tawala na kutoa sababu kuwa chama tawala kimepoteza mwelekeo. Lakini katika kitu ambacho kimeonekana kuwa ni kituko cha mwaka ni pale ambapo mtu anahama kutoka upinzani kwenda CCM, watu hao wamekuwa wakibezwa kwa kusema kuwa njaa zinawasumbua.

Napata shaka sana juu ya upinzani huu! Mbali na hilo kunatuhuma nyingi sana zilizotolewa na upinzani kuhusu ufisadi na ufujaji wa mali za umma unaofanywa na baadhi ya viongozi lakini pindi watu hao wanapoanza kuchukuliwa hatua huamua kukimbilia upinzani ili kutaka huruma ya wananchi kuwa wanaonewa kwasababu wamekihama chama tawala.
 
Ndiyo for the time ever CCM Zanzibar inashindwa mchana kweupe na CUF ktk sanduku la kura na kwa ubabe wa kijeshi inapindua matakeo na kuzua mgogoro wa kikatiba mpaka leo...!!

Unasema "for the first time"?
Nimekushtukia wewe utakuwa LUMUMBA buku saba.
Kwa taarifa yako Seif hajawahi kushindwa uchaguzi Zanzbar. Ndo maana wenye akili tunajua Seif ni pandikizi la CCM na anatumiwa na CCM kuwazuga wazanzbari ili iendelee kutawala miaka yote.
 
Wasafi watabaki ccm,,,CHADEMA watu wanacheza na saikolojia ndo maan wale mliowaumbua kuwa mafisad na wez ndo wanahamia kwen ili wawafunge midomo ya kuongelea maswala yao ili waendelee kunemeeka na vle walivyovivuna,,,,,,kama una akil kamwe huwez kubakia CHADEMA ila kama ndo umeshikiwa akil utabaki ili uendelee kuwapgia debe vgogo hku ww ukilia njaa na familia yako ukimkosoa maguful kila ck,,,
 
Back
Top Bottom