MarkHilary
JF-Expert Member
- Feb 8, 2015
- 1,761
- 2,027
Mpaka JPM amalize ngwe yake CDM tutakua tumeizika
Masha alipewa kugombea ubunge wa Africa mahaliki Tena wakiwa wawili tu na wenje kutoka chadema...bila wabunge wa ccm kuwapiga chini Masha angekuwa mbuge kutoka chadema kumbe ni mchumia tumbo tu....chadema lazima wajitathimini kwakweliKina Masha ndiyo hao wamekaa miaka miwili bila cheo wametimka!!
Kwa kweli sielewi ni nini kimewakumba vijana hawa wa BAVICHA!!ile Bavicha imekufa kabisa sasa
Mkuu ni muda mrefu tangu,Chadema wanapaswa kuwafanyia assesment wanaotoka CCM na kukimbilia kwao kabla ya kuwapokea na kuwapa nafasi nyeti kwenye chama.Pengo la vijana mahiri kama Mnyika,Zitto,Shonza,Heche,Sugu linaonekana waziwazi ile Bavicha imekufa kabisa sasa wanasubiri kupokea wazee wanaohama CCM
Tatizo wewe unajiona unajua sana na kujifanya 'mchambuzi' wa siasa.Kwa hiyo wewe unataka ccm ichukue wanachama wa chadema lakini chadema isichukue wanachama wa ccm! CCM kuchukua madiwani wa chadema na kuwapa nafasi ya kugombea tena udiwani kupitia CCM wewe unaona sawa.Kwa kweli sielewi ni nini kimewakumba vijana hawa wa BAVICHA!!
Nilichonukuu kinahusiana na hicho ulichoandika? Sisi na niliyekuwa nimemnukuu tulikuwa tunazungumzia utofauti wa BAVICHA ile ya kina Heche na hii ya kina Patrobas. Sasa kuona sawa au si sawa kuhusu kupokea wanaotoka CCM ama CHADEMA Kumekujaje!!Tatizo wewe unajiona unajua sana na kujifanya 'mchambuzi' wa siasa.
Kwa kweli sielewi ni nini kimewakumba vijana hawa wa BAVICHA!!ile Bavicha imekufa kabisa sasa
Umeandika kama mpenzi kweli wa Chadema lkn kwa jicho la tatu unataka Chadema waanze kuwabagua watu eti tu kwa sababu walikuwa CCM.Siasa ni watu yeyote akiona inafaa kuhama chama na afanye hivyo cha msingi havunji sheria za nchi!Ndiyo maana kuna chama cha siasa kinatuhumiwa kuwanunua wanachama wa vyama vingine,ulishawahi kujiuliza kwanini?Naamini, hata waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hawakulenga kinachotokea sasa. Akina Mzee Edwin Mtei, kama waanzilishi walilenga kuifanya CHADEMA iwe chama imara na mbadala. Si sehemu ya kutambia watakavyo wanaCCM.
Kwa uelewa wangu, waanzilishi wa CHADEMA walipanga na kufanya mpango wa kuijenga kwa kutafuta wanachama na hata kuandaa viongozi wa baadaye nje ya CCM. Wanachama walipaswa kusakwa, kulelewa na kukomazwa humo. Ni katika mfumo wa walivyopatikana akina Zitto na Mnyika.
Hivi sasa, mambo yamekuwa tofauti. CHADEMA sasa imekuwa sehemu salama kwa wahamiaji na wahamaji wa CCM. WanaCCM sasa wanahamia na kuhama kadiri watakavyo ndani ya CHADEMA.
Ingekuwa kwenye uga wa masuala ya kodi, CHADEMA ingekuwa ni tax haven. Sehemu salama na ya kukimbilia kujificha.
Anaingia Lazaro Nyalandu, anatoka Laurence Masha. Anaingia mwanaCCM, anatoka mwanaCCM. Viongozi na wanachama wa CHADEMA wanajifariji kwa kusema kuwa eti chama ni watu! Nawahakikishia, wanaCCM watahamishia hata makundi yao CHADEMA. Wataanza kupigana vikumbo kama wapo kule.
CHADEMA, rudini kwenye misingi yenu. Sakeni wanachama wapya bila kusubiri wahamiaji na wahamaji wa CCM. Mkiendelea hivi, mtachaguliwa viongozi na kupangiwa cha kufanya na wanaCCM. Hamtaepuka kuwa CCM B. Msifanye chama chenu tax haven!
Bavicha ilishakufa hata kabla ya Magufuli kuingia madarakani,Ukweli Dr Slaa alijitahidi sana kufanya uenezi wa chama kuanzia level ya chini.Uchaguzi wa 2015 uliwafanya Chadema wakasahau ile mipango endelevu ya miaka mingi wakachagua mipango ya muda mfupi ambayo kiuhalisia ni nguvu kutekelezeka kwa mazingira ya TanzaniaMkuu ni muda mrefu tangu,
Tangu Tanzania ilipojiondoa isivyo rasmi katika Democrasia na ramsi katika Transparency.
Pia utawala wa sheria unaonyesha kukosa makali nchini..
Wasiojulikana wanaonekana kutamba kama vile wako kibiti...
Hao vijana wakina mnyika and the like, ni Brand muhimu sana kwa CDM na nguvu ya upinzani kwa ujumla.
Nguli Mmoja mjenga hoja, na mwanasheria ndugu Tundu Athipas Lisu wamempumzisha na bado hatujui kama walishamsamehe kile wanachotaka hata kupelekea kumiminia Risasi nyingi vile..
Godbless Lema, Mbilinyi wanahofu na mustakabali wao hapa nchini...alishalisema hili Tundu Lisu kabla maswahibu hayajamkuta. Na Joseph Mbilinyi pia anahofu.
Unaweza kua mahiri lakini Hofu ya ubinadamu ikakufanya ufikiri tena na tena kabla ya kuamua kushindana na Chuma cha Reli.
Ukitumia mdomo lakini adui anatumia kila silaha kukunyong'onyeza.
Haki kweli kabisa....Bavicha ilishakufa hata kabla ya Magufuli kuingia madarakani,Ukweli Dr Slaa alijitahidi sana kufanya uenezi wa chama kuanzia level ya chini.Uchaguzi wa 2015 uliwafanya Chadema wakasahau ile mipango endelevu ya miaka mingi wakachagua mipango ya muda mfupi ambayo kiuhalisia ni nguvu kutekelezeka kwa mazingira ya Tanzania
Ni mjinga tu anayefikiri chadema hii ya sasa itakuja shika nchi, wameongeza flava tu ktk chaguzi kuisindikiza sisiemu.Hayo ni mawazo yako tu ndugu Petro E. Mselewa kila zama na kitabu chake na unalijua fika! Whatever utakavyoita kwa kutumia tumsamiati twako twa kisheria ila deep moyoni unafahamu vuguvugu la kisiasa nchini kwa sasa... ni wachache mna tena wenye mioyo mikuu wataendelea kuwa na misimamo ama udhaifu waliokuwa nao kwanza!
Kuna point ya msingi ya CHADEMA kutafakari namna ya kupata wanachama wapya.Sikio la kufa ....Mbowe ndiye mtu anayepaswa kujitafakari binafsi na kuchukua maamuzi magumu ...tusisubiri ya NCCR mageuzi maana naona kabisa Chadema inaenda shimoni na hasa moto utaanzia uchaguzi wa 2020 ....bado mapema kujipanga upya .....
Of course kwa mfumo wa siasa na uchaguzi uliopo sasa, ni vigumu kwa chama tofauti na CCM kushika dola! Utashindanaje na chama dola kweli?Ni mjinga tu anayefikiri chadema hii ya sasa itakuja shika nchi, wameongeza flava tu ktk chaguzi kuisindikiza sisiemu.
Kwamba CCM ndo inamiliki hisa zote za taifa? Ama wameshikilia akili za wananchi wote?..Pambaff!Ni mjinga tu anayefikiri chadema hii ya sasa itakuja shika nchi, wameongeza flava tu ktk chaguzi kuisindikiza sisiemu.
Usiogope, nimesema ni wajinga tu wanaofikiri chadema hii itashika dola, wewe unaamini na kufikiri hivyo, kwa hiyo upo kwenye kundi la niliosema hapa.Kwamba CCM ndo inamiliki hisa zote za taifa? Ama wameshikilia akili za wananchi wote?..Pambaff!