Ndani ya BBC: Kitila Mkumbo atetea 'Ushoga'

Ndani ya BBC: Kitila Mkumbo atetea 'Ushoga'

Ukisoma majibu ya watu humu inaonesha kuna mashoga wengi saaaaana!!!!!!
Kibadiru unawaona???!!
 
Last edited by a moderator:
Yeye dr nilivyomuelewa mm nikwamba huyu Museveni amesigni sheria hiyo ili waganda waweze kumruhusu aendele kuitawala nchi hiyo hali mda wake umeisha

your very okey.ameitumia kisiasa ili waganda wampe kura 2016
 
asiyemsupport Museven kwa hili ni kichaaa

hata ukiniita kichaa poa,nimeishi na kukaa uganda na kuoa huko kwanza suala la ushoga sio kubwa kama m7 anavyotaka kulitumia kisiasa kiukwel uchumi utamfanya ajifikilie upya
 
Acha kupotosha, kwa jinsi alivyoulizwa na alivyojibu ameonyesha dhahiri kabisa angependa mashoga waachwe huru, huyu hafai kabisa ndiyo maana CDM walimfukuza. Mhadhiri mzima unatetea ushoga? Au na yeye ni shoga?

mkuu hebu sema alichosema Dr.kitila huenda mimi sijasikia,lakini kama ile habar ya BBC swahili na charles hilary kitila hajasema na wala hajaulizwa kama anaunga mkono ushoga au la.
 
Ukisoma majibu ya watu humu inaonesha kuna mashoga wengi saaaaana!!!!!!
Kibadiru unawaona???!!

Hapana. Mimi siwezi kujua nani ni shoga na nani si shoga humu kwa kuangalia tu waandikacho.

Maandishi hayamfanyi mtu kuwa shoga. Waweza kuta hao wanaojifanya kupinga sana huo ushoga ndo mashoga waliokubuhu kabisa.

Hivyo mi sina ujuzi wa kujua nani ni nani humu. Kama wewe unao basi hongera maana wakati mwingine 'it takes one to know one'.
 
Hapana. Mimi siwezi kujua nani ni shoga na nani si shoga humu kwa kuangalia tu waandikacho.

Maandishi hayamfanyi mtu kuwa shoga. Waweza kuta hao wanaojifanya kupinga sana huo ushoga ndo mashoga waliokubuhu kabisa.

Hivyo mi sina ujuzi wa kujua nani ni nani humu. Kama wewe unao basi hongera maana wakati mwingine 'it takes one to know one'.

u made it very clear....
 
yaani ww pixel acha kua mvivu kuchambua maelezo ya mtu ..

ww ulitaka aongee direct...

Na kwann kasema bado afrika tunahotaji misaada ... ukirelate na issue ya Uganda ni kwamba anataka Museven asingesign mkataba huo au.. anmeonyesha kujali misaada kuliku Ushoga .

Kuasema Muaeven kajivisha ubabe asioueza maana yake nn ...embu tuambie ..
au ww unaona hayo aliyoyasema yana relate vip basi kwa upande wako ,ikiwa swali aliloulizwa ni juu ya ushoga,embu tupe maoni yako.

mkuu kwanza nikushukuru kwa kuheshimu mawazo na uchambuzi wangu juu ya ile habari.Uganda ni nchi masikini na inategemea misaada ya nje.hao wanaotoa misaada kwa uganda ndio mashetani wanaolazimisha ushoga ukubalike Afrika.ukitaka kuwakataa anza kujipanga kwa kutotegemea misaada yao,sasa uganda imejiandaa kuishi bila pesa zao?kama bado basi wasingesaini sheria kibabe.M7 angeendelea kupiga danadana juu ya mambo haya kama inavyofanya Tanzania.Labda tumuombe Dr.kitila aje hapa JF amalizie hoja yake iliyokatika BBC swahili mimi nimeelewa hivyo.
 
u made it very clear....

Yup..made it crystal clear that I can't tell who is gay and who is not based on what people post using fake names.

For all I know you could be a seasoned homosexual.
 
Pixel u can actually see IQ za wenzetu hapo juu zilivyo,wakiambiwa wana udumavu wa akili huwa hawaamini

Bad enough Dr kitila hajatoa kauli ya kuunga mkono ushoga na pia mawasiliano yalikatika.tunawezaje kuweka conclusion?mimi binafsi siwezi kumuonea mtu hata kama simpendi.
 
Museven ameonesha njia sahihi, lazma na cc 2ifuate. Ushoga na kutembea nusu uchi lazma upigwe vita hadharani bila kumung'unya maneno eti kisa misaada ya wazungu! Aibu yenu africans. Kama vp mashoga wote wakamatwe wapewe visa waende kwa Obama.
 
Kwahiyo ulitaka m7 akubali kupunuliwa kwa ajili ya misaada! ulivyo mburuula huo Ni kabsaaa kwamba Kitila c riziki? Au na wewe ni mojawapo fuuuuuuu kichogoni.

Mkuu cc;Jambohili kwanza usinitukane ili kunishinikiza niseme unachotaka wewe.niache niseme nilivyoelewa na wewe sema ulivyoelewa kisha tuunganishe hoja zetu.M7 sio kwamba amesaini tu,bali amesaini kibabe kwa maana kua hahitaji misaada ya wazungu tena.wakati amesaini kibabe jamaa wamekata misaada na ameanza kulalamika jumuia ya kimataifa imemsaliti.hiyo inamaana kua ataondoa hiyo sheria na kusaini kukubali ushoga siku si nyingi.hiyo ndio hoja aliyokua nayo Dr kitila mimi ndivyo nilivyoelewa.
 
Tunajadili ili kumfanya kitila aonekane ametetea ushoga?? Mm nilimsikiliza mwanzo mpaka mwisho. Nilichoelewa alikuwa anaongelea jinsi nchi za magharib zinavyojarib kuitawala afrika kwa kupitia misaada, na akajarib kuongelea kuhusu viongoz wa afrika wanavyojarib kujitia ujasir kny baadh ya mambo na kuyaacha Yale ya msingi kabisa kma umasikin na ufisad. Akasisitiza viongoz wa afrika lazima wafikirie kupunguza utegemezi. Tupunguze chuki za kikasuku.
 
Tusipotoshe. Katika mazungumzo yangu sikutetea wala kupinga ushoga kwa sababu hiyo haikuwa mada. Nilichosema:

i) Misaada kutoka nchi za magharibi huambatana na masharti. Masharti mengi yanalenga katika kuchochea utawala bora hasa ukilenga kukuza demokrasia ya kimagharibi na kulinda haki za binadamu. Moja ya haki ambazo zinalindwa sana na nchi za kimagharibi ni haki za wapenzi wa jinsi moja. Kwa hiyo ilitarajiwa kwamba nchi hizo zingeikatia misaada nchi ya Uganda pale ambapo Rais Museveni angesaini sheria inayotoa adhabu kali kwa wapenzi wa jinsi moja. Nikasisitiza hakuna njia ya kukwepa masharti haya kama nchi za kiafrika zitaendelea kutegemea misaada kutoka magharibi. Hatuwezi tukala keki na tukawa nayo at the same time.

ii) Viongozi wa kiafrika wanapenda kujivika ujasiri bandia katika mambo yasiyo na tija. Katika bara la Afrika kuna matatizo mengi na makubwa zaidi kuliko ushoga. Lakini wanatumia kadi ya ushoga kwa sababu ni swala gumu katika bara la Afrika ili kujipatia umaarufu hewa. Ushoga haliwezi kuwa tatizo kubwa kuliko rushwa na wizi wa raslimali unaoendelea bara la Afrika. Rais Museveni ana matatizo makubwa ya kiutawala na hali yake kisiasa si njema kuelekea uchaguzi wa mwaka 2016 na anatumia hili la ushoga ili kujikweza na kujiweka sawa katika kuwasaulisha waganda matatizo ya kisiasa na kiuchumi yaliyosababishwa na utawala wake. Anatumia pia kadi ya ushoga ili aendelee kugombea kiti cha urais wakati alipaswa kuondoka juzi.

Bahati mbaya mawasiliano yalikatika na nikaishia hapo.
 
Uko sawa mkuu kuna watu hapa wanakurupuka tu hawajasilkiliza hata hicho kipindi wanaongozwa na chuki binafsi tuu


kweli kabisa mkuu,jamaa wengi hawajasikiliza kipindi.
 
Back
Top Bottom