Bahati mbaya siwezi kukujibu point by point kwa device niliyonayo lakini acha nikupe msaada pengine you can recover your conscious!
Let not your heart be troubled.
Kitu gani kinakufanya wewe uchague wizi ambao ni tabia iwe mbaya kwa waganda kuliko ushoga ambao wao wana u perceive ni laana?
Mimi nipige box masaa 60 kwa wiki, nipinde mgongo na kibyongo juu, Ijumaa ni payday niende kuchukua cheki yangu. Nikitoka hapo niende kui-cash lakini kabla sijafika kwenye check cashing store, uibuke from nowhere huku umenishikia bastola ukiniamrisha nikupe kila nilichonacho mfukoni la sivyo utakipasulia mbali kichwa changu. Natii amri yako, nakupa check yangu.
Narudi zangu nyumbani mikono mitupu. Check umenipora na kili kilichokuwemo mfukoni mwangu umekichukua kimaguvu. Mimi check yangu nimeifanyia kazi, nimeitolea jasho, wewe umekuja na kuichukua.
Kwa akili, hekima, na busara zako zote ulizopewa na ulizorithi, unaona ni sawa ulivyonifanyia? Unadhani baada ya kunipora nami ntafurahi tu, ntarudi nyumbani nikichekelea nikiwa na shauku ya kumsimulia Bi. Kibadiru ambaye naye ananisubiri nyumbani nije na mboga?
Sasa ushoga unajifanyia mwenyewe huko. Kama ni laana utalaanika mwenyewe. Kimbelembele cha mimi kuja kukulazimisha kufanya tofauti na utakavyo kinahusu nini?
Mbona ni suala jepesi kabisa hilo....
Yaani kama hilo la tofauti ya wizi na ushoga nalo unahitaji kuelezewa, basi, nasalimu amri maana naweza kuwa najadiliana na mtu mwenye uwezo wa chini kidogo.
Labda ujifikirie mwenyewe kati ya laana na tabia mbaya ipi ina hitaji heavy punishment.
Unaonaje tukianzia na fasili za hayo mambo mawili? Ili walau tukubaliane kabisa kwamba 'laana' maana yake ni hii na 'tabia mbaya' maana yake ni hii. Tuanzie hapo kwanza. Unaonaje?
Alafu una justify vipi perception yako ndiyo iwe benchmark ya ile ya waganda?
Waganda wapi unaowazungumzia wewe? Waganda mashoga au wale wanaopinga ushoga? Maana si Waganda wote wana 'benchmark' (whatever you meant by that) iliyo sawa.
Then kama definition ya wizi inatumia maneno ya wanadamu na ufahamu wao vipi uikataye hii waliyojiwekea waganda wenye quality zote za ubinadamu kama wewe?
Huwezi kulinganisha wizi na ushoga. Mtu yeyote yule mwenye akili tu za wastani anajua hilo. Sasa wewe sijui kwa nini tu umeng'ang'ania kulinganisha hayo mambo mawili.
Hivi kwa mfano, nikikuibia hela zako zote ulizozipata kwa kufanya kazi na ambazo zipo kwenye akaunti yako utafurahi?
Kwakukusaidia google hii concept ya egocentrism wanayotumia wana soholojia ku iron out some of your doubts......
Hata sijakuelewa hapo. Ni iron out doubts gani?
Kama ilivyo right kwako ku punish what you define crime ndivyo ilivyo kwa
Waganda katika jurisdiction yao ku exercise hiyo privilege na wewe una responsibility yakuheshimu rights zao kama ilivyo kwao kwako na Tanzania
Yako
But homosexuality is not and should not be a crime. No one is hurt by it. If you don't like it, don't partake in it. Mind yours and let others mind theirs.