So you mean hiyo haki yakujiamulia mambo Uganda kama nchi haitakiwi kuwa nayo?
Uganda ina haki ya kujiamulia mambo yake, sawa, lakini siyo kujiamulia kunyanyasa watu hovyohovyo. Leo hii Uganda ikidai kwamba watu wa kabila fulani ni duni na hivyo wanapaswa kuangamizwa kutoka kwenye ramani ya Uganda wewe utaona sawa? Utadai kwamba ni sawa tu kwa vile Uganda kama nchi wana haki ya kujiamulia chochote kile wapendacho?
Mashoga nao ni binadamu. Na kwa huo ubinadamu wao tu wanastahili kupewa haki zote za msingi kama binadamu wengine. Wewe kama hupendi ushoga wao achana nao. Fanya yako waache na wao wafanye yao. Kwani kinakuuma nini wao wakiwa mashoga? Inakuhusu nini wewe wao wakiwa mashoga?
Is it that hard for you and your ilk to mind your own business and live your own life and leave others alone so they live their own lives as well? Why you gotta be all up in their business? Good grief!!
Majority of Ugandan hawakubali mashoga maana ni something against their culture,
That culture card is a bunch bunk. Homosexuality has always been there since the history of existence. So don't even go there and act like it is something brand spanking new to Uganda or any other African country, for that matter.
And you talk about the majority, well, what about the minorities and their right to exist in society? We can't all be the same, for god's sake.
Intelligent people always come up with a modus vivendi so that all can live in society despite their differences and ensure that minorities' rights are protected.
is exotic imposed from foreign countries
You are way off base. Way way off base. Homosexuality has always been there in Uganda and everywhere else and you can't pin it to any specific country as to its origins. I suggest you start reading omnivorously so you can expand those horizons because you appear to be somewhat ignorant on the subject.
sasa leo eti hao waliokuwa imposed wapewe haki na wale wa asili wanyimwe;
Soma vitabu. Narudia tena, soma vitabu. Hakuna aliye-impose ugay Afrika. Ulikuwepo tokea enzi na enzi. Hata wanyama (wasio binadamu) nao wana hayo mambo (lakini sitegemei ulijue hilo kwa sababu umeonyesha ujinga tayari. Hivyo unaweza ku-google ili uweze kujifunza zaidi)
ndiyo definition mpya ya democracy?
Kilichofanyika ndo haswa siyo demokrasia maana kwenye demokrasia haki za wachache nazo huheshimiwa . Uganda imepiga hatua nyuma kwenye hilo!!!!!!! Kwenye demokrasia hakuna mambo ya kusema sijui kwa vile wengi tunataka hivi basi wale wachache ambao wako kinyume na nyie wengi mnavyotaka, haki zao ziminywe. Hapana. Demokrasia ya ukweli haiko hivyo hata kidogo. Hata walio wachache nao wana nafasi yao katika jamii.
Mimi nadhani Museven anatakiwa kuwa supported with other African countries kuwa hao World Bank if they want to be called world institution basi hawana haki ya kuwanyima Uganda kwasababu hiyo itakuwa dictation maana majority ya wananchi wamekataa unless kama wao ni representation ya developed countries and so the word World Bank inakosa legitimacy. Kama hivi ndivyo kwanini nchi za Africa zisijiondoe kwenye umoja wa mataifa kuishinikiza hiyo bank kama wanavyowafanyia wao Uganda kwa niaba ya America?
Wewe hujui kabisa maana ya demokrasia. Unadhania tu kwa vile wengi wamekataa jambo basi wale wachache ndo ile kwao, wanyanyaswe, waadhibiwe, waangamizwe, na upuuzi mwingine kama huo.
Hivi kuna ugumu gani kama wewe hupendi jambo fulani kuachana nalo na uwaache wale wanaopenda wajinafasi kwa raha zao?
Tuache uoga waafrika hatuna chakupoteza kama ni shida tunezizoea tutaishi maisha yetu nje ya huu mfumo dhalili. Tungeweza hili wangekuja wenyewe kutuomba na maneno yao yakisanii deplomacy!
Tunachotakiwa kuacha ni kukiuka haki za binadamu. Kwenye hizi nchi zetu uhai wa binadamu hauthaminiwi kabisa. Ona watu wanaotuhumiwa kuwa wezi wanavyouliwa mabarabarani mchana kweupe bila hata due process. Kinachohitajika ni mtu mmoja tu kupiga kelele za mwizi! mwizi! tosha. Iwe umeiba kweli au la watu hawajali hilo. Utapewa kipondo na kuchomwa moto hadi ufe mbele ya kadamnasi na hakuna mtu atakayekamatwa kwa kosa la mauaji.
I mean, hata kama mtu kaiba kweli, tuseme kanyakua pochi ya mtu. Ndo kweli apigwe hadi afe na watu waliojichukulia tu sheria mkononi? Na wewe hilo unaweza ukalitetea kwa kujenga hoja ya eti 'wengi waliamua apigwe hadi afe kwa hiyo ni sawa tu alichofanyiwa'? Hapana kwa kweli.
Kwanza Kitila kaidanganya dunia Museven na waganda hawajaanza leo kupinga ushoga wamelipinga hili kwa muda mrefu na kumekuwa na argument zao kwa muda sasa, tangu 2011 and even before. Atafute documentation kwenye mtandao aone hadi U-tube zipo za Waganda kupinga hilo....
Waganda na demokrasia ni oxymoron. Hawaelewi maana yake. Hilo li-Museveni ni lidikteta na litafia madarakani. Hivyo sishangai sana lilivyosaini hiyo sheria ya kijinga na kandamizi kwa mashoga wa Kiganda ambao usikute nao ni walipa kodi wazuri kabisa.