Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Ili ujue atakayofanya magufuli huhitaji kufumba macho na kuanza kuyafikiria aliyoyafanya kwa taarifa yako yapo bayana kabisa,kila mtanzania anayajua,sema kinachowauma wachache ni ile wagombea wao kushindwa hilo ndo naweza kuelewa kuwa hoja nyingine hapa ni maumivu ya moyo,na nitoe ushauri hapa kwamba kama hamtoi uchungu wenu wa mioyo na kukubali matokeo mtaumia sana lakini jembe litaendelea kuchapa kazi na bahati mbaya yenu ni kwamba the majority wanafahamu uwezo wa magufuli,mie nikimlinganisha na hata hao mnaowaombolezea na kufikia hadi kuzusha kwa niaba yao haotasaidia kikubwa kubalin yaishe tujenge taifa
 
Well said!
Hapa tatizo ni mfumo huu ulioasisiwa na chama 1!.
Lkn watu hawaelewi
Ooh magufuli jembe sijui nn!
Hakuna jipya chini ya huu mfumo!!

Mfumo ni watu mmoja mmoja na taasisi waziundazo. . . . .Ukipata key palyer mzuri anaweza badili mchezo mkaacha kufungwa mkaingia kwenye kutoa droo. . . . .

So far apewe benefit of doubt. . . . . sababu anaweza akiamua sasa asipoamua tutaanzia hapo japo tutakuwa tumeumia. . . .
 
Asante The Boss kwa mada hii muhimu. Nimepitia michango ya wenzangu waliotangulia, ni kweli kuwa ni wakati muafaka sasa tujadili na kushiriki kutengeneza nchi na taifa letu na historia itatuhukumu hivyo.

1. Kwa CCM suala la Urais kwao halina mjadala ni LAZIMA awe wa kwao hata kama italigharimu Taifa hili uhai wake wote. Hiyo ni siri iliyo wazi kwa miaka mingi tu.

2. Je ni mara ngapi tumewahi kusikia au kuona "viongozi wakuu" kama Rais, Waziri Mkuu, Wabunge na Mawaziri wakisema/kulalamika au kuonyesha "laiti kama ingekuwa ni uwezo/mamlaka yangu basi ninge......." Mifano iko mingi; mfano kauli ya Waziri Mkuu Pinda kuwa "wakiwashughulikia mafisadi nchi itayumba..." Hii inaonyesha kuwa kuna "nguvu" nyuma yao hao wanaonekana kwa macho kuwa "wakuu"; ambayo wao wenyewe wanaiogopa na kutumikia hiyo "nguvu" kwa hiari au shuruti, kwa kujua au kutokujua.

3. Kauli ya Kingunge ni nzito na ya ajabu sana kwa kuzingatia historia, uhusiano na hadhi yake CCM.
Kwangu mimi kauli ile ina vitu vikubwa vine (tofauti na watu waliojitokeza kusema kuwa mzee yule alikuwa anaitishia CCM nyau).
a) Kitengo ni kitu halisi "real"
b) Kitengo, pamoja na kuwa ni halisi, lakini sio kinachofikiwa na wengi (not accessible to all except for a selected few)
c) Kitengo ni fumbo pana na refu (codeword and terible mystery)
d) Kitengo hakina mipaka (kinaweza kuanzia ndani ya CCM lakini hakiishi huko na kinyume chake)

4. Matunda yake yako wazi katika historia ya nchi yetu. Ujinga umeendelea kutusumbua, umaskin umeendelea kuongozeka, maradhi, madawa ya kulevya, rushwa na ufisadi vimeongezeka kila siku na sasa vinatishia mustakabali wa nchi nzima.

5. Ugumu wa fumbo ni pale (kwa mujibu wa Kingunge) Kitengo ndio "kilipika/kilitengeneza" kashfa ya Richmond ili kumtoa Lowassa kutoka kuwa WM (hatujui hasa kwanini), lakini kwa jinsi kilivyo cha ajabu, nusura kiiangushe kabisa Serikali ya Kikwete mwaka 2006! Inaonesha kitengo kiko nje/juu ya mamlaka ya Mkulu. Ni kama vile duara (cycle) huoni mwisho na mwanzo ni mgumu pia kuuona!

HITIMISHO (kwa sasa)
i. TISS, Idara ya Ulinzi/Usalama/Ujasusi wa Chama, Ikulu, Bunge ni sehemu ya Kitengo lakini Kitengo sio Umma (Wananchi wa Tanzania.
ii. Kitengo kipo kiuhalisia ingawa hakipo kwa mujibu wa Katiba yetu ya JMT.

Fumbo bado linataka tuendele mbele zaidi kuchunguza, kudadisi na kuwa wajasiri zaidi ili tusimezwe na "Kitengo"
 

Wewe ndo umeongea point kabisa.....watu hapa wanachangia kisiasa zaidi..,
Ikitokea UKAWA walete mgombea maslahi mfukoni, pia CCM watuleteee mwingne kuipeleka nchi shimoni ndo tuwaache tu kisa nini?
Kuna mambo wananchi hawawezi kuyasikia na ikitokea wakafaham juu ya hao wanaowashabikia wanaweza wakastajaabu na kupata stroke
Hii nchi bado changa sana hata huo upinzani inabidi ujengewe uwezo kuongoza nchi.....Mtauzwa hadi mayai yaliyo tumboni kwa ushabiki watanzania ....tulieni tujenge hii nchi yetu sote si ya kuendeleza kusini, Kaskazini, wala kanda yeyote ile..tunahitaji maendeleo na tuache propaganda tusizozijua kwa undani wake...hatuwezi kabidhi nchi kwa mtu kisa mahaba ya siasa
 
Unless kuna mapinduzi, hiyo ni standard practice dunia nzima.
Fuatilia kilichompata Princess Diana yule wa Uingereza aliyetaka kuolewa na mwarabu, alipatiwa ajali na akamalizwa haraka sana.

Hakuna ushahidi kwamba aliuliwa, kule kuna waandishi wa habari wanojua kufuatilia habari in deep. Kwa hiyo hizo habari unazosema sio za kweli na huna ushahidi nazo, ni habari za vijiweni.
 
Sasa hao usalama wa taifa si waingie na kwenye michakato ya vyama vingine ili kuweka usawa katika kupata mtu safi mbele ya wananchi?

Hapa ndipo tunapotofautiana, Usalama wa taifa iachwe ifanye kazi zake kiuweledi bila ya kuingilia siasa. Kama kuna mtu fisadi basi wanatakiwa wamshughulikie kama muhalifu hata kama ni Waziri au mtu yoyote aliyevunja sheria za nchi. Wasisubiri mpaka huyo mtu anapotaka kugombea nafasi kwenye chama chake. hapo ni kuingilia kazi za vyama vya siasa. Sasa hivi Usalama wa Taifa umeshajisahau kuwapo kwa ajili ya kulinda taifa, badala ya kufanya ukachero wa kulinda taifa sasa wanafanya ukachero kulinda ccm.
 

Na km kuumia ni Miaka 10 tena!!!

Siamini km ataweza,kwenda kinyume na matakwa ya "kitengo" sidhani km ni rahisi!!!
 

Umeshaambiwa kitengo walashapanga Rais awe membe lakini wajumbe wakakigomea kitengo wakaamua kupiga kura Kwa magufuli , kitengo sasa wote wapo Kwa magufuli watahakikisha anakuwa Rais mpende msipende hata kama kura za wananchi zitakwenda Ukawa lakini wajue Rais ni magufuli tu.
 
Well nailed. . . . .
 
We need people like John Edgar Hoover katika ofisi za Usalama wa Taifa. Mtu akayepigania Usalama wa taifa uwe na nguvu kama walizokuwa nazo enzi za Nyerere au zaidi ya hapo. Wawe na misuli ya kwenda sehemu yoyote ya nchi na nje ya nchi bila ya kuingiliwa na wanasiasa. wakatae kutumika kisiasa kama John Edgar Hoover, wajikite kwenye ufanisi wa kazi zao.

 
kitengo ndicho chenye kuamua mpaka hesabu za kura ziendee kwa nani.

Ndiyo maana yake kitengo wana matokea tayari hapo wanasubiri mda watangaze Rais magufuli , kule Zanzibar tokea 1995 CUF imekuwa ikishinda Uchaguzi lakini kitengo hubadilisha matokeo na ccm kupewa ushindi wa mezani kirahisi ina maana Zanzibar hata wana ccm wasipopiga kura ccm itashinda tu kupitia Kwa njia za kitengo.
 
ha ha ha...naona sasa vijana wamelipwa kuja mitandaoni kutuletea porojo.
ACHENI POROJO NA KUTUMIKA...
Lowasa mwenyewe ni hatari kwa afya yake binafsi...sembuse familia yake na watanzania.

Hivi kweli bado kuna WaTz wa namna hii? yaani umeshindwa kuziona logic zote, umeona Lowasa tu...

Chukua yale mazuri, ya Lowasa yaache.
 

Nyani Ngabu Umemaliza kila kitu hapo, tanzania hakuna demokrasia ya vyama vingi bali kuna kiini macho cha demokrasia. Uchaguzi unakuwa sio wa haki. tatizo kubwa tunalo sisi wenyewe watanzania, tunachezewa vibaya sana na hawa wahuni
 
Kubali ukatae kitengo ni kila kitu hapa Tanzania japo kuna sehemu wanashindwa mfano wameshindwa kumpenyeza Membe na January machaguo ya Jk na Nape , sasa wanajipanga kumpa Membe uwazi Mkuu na Nape atakuwa waziri wa Utawala bora au mambo ya ndani ili waanze kuwakomesha timu Lowasa , kitengo wana uhakika Kwa 1000% magufuli atakuwa Rais na membe atapewa ulaji sanjari na Nape .
 
Kuna wapiga kura mil 20, ccm ina wanachama mil6 , ukawa wa jitahidi kuvuna wana chama at least wawe mil 8 kwa mwaka 2025, waende kwenye matawi chini huko , then watafute suppor ya kitengo , kitengo hakiwezi kumpa mbowe nchi au slaa. Tanzania sio uingereza au marekani , demokrasia yetu inavyoendeshwa ni kama urusi na China , hizo nchi zote vyama Vya upinzani havijawahi shika nchi , comrade kinana amekirudisha chama huko hadi kapeleka watu kwenye mafunzo China kwanini haendi uingereza hadi Balozi wa China kasimama jukwaa la ccm , kitengo kina nguvu sana ila kwa ugomvi wa membe na lowassa kumteua magufuli aisee Jamaa wamecheza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…