Nawaheshimu walimu

Bongo nyoso sana aisee niliona volunteer tasisi ya serikal wanawafukuza Sasa mtu anakaz na salary anayo ila anamuwekea vikwazo intern/volunteer aisee.
Mzee watu weusi tuna laana. Laana ya milele... Yani muomba ushauri hapa ajitafute kwelikweli. Mana hata mifumo ya intern hasa kwa ofisi private sio rafiki.

Binafsi nashauri awekeze sana kwenye competency. Ajitahidi kusaka uwelewa wa chochote ili kusavaivu na ajiimarishe hapo. Huku kwingine Kuna matatizo ambayo hayavumiliki
 
Kabisa mzee.ajitafute tu kivingine.
 
Ni kweli ukiona mtu anadharau ajira huyo ameshiba na ana pesa.

Ualimu wa Dada yangu
1. Ulinisomesha
2. Tulijenge nyumba ya matofali zamani ya makuti
3. Wazazi wake woote wanapata matibabu ya Bima ya Afya bila utata.
4. Watoto wake wanasoma shule
5. Anapata mlo na mahitaji ya kawaida kwa uhakika.
 
Najuta na umri umeshaenda sijui pa kuanzia biashara nayo chenga mtaji ulikata [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Ufinyu TU wa maarifa ila huwezi kuniambia Hana Cha kuanzia wakati ni mzima sio kilema. Kitendo Cha yeye kuwa mzima ni mtaji tosha. Cha kuanzia anacho.​
 
Tatizo Sasa ushauri kama huu naupata too late kipindi Niko chuo hamna mtu wa kukumentor
Yaani unajikuta unajifanyia mambo mwenyewe tuu bila muongozo hasa Kwa sisi yatima tusio na wazazi ndugu hawahangaiki kabisa
Kuwa Yatima mwisho ni miaka 18 wewe kwa sasa usijiite Yatima maana wewe ndio Baba na Mama yako!
Pambana usikate tamaa kama kazi kupata kwa hiyo course utapata ni swala la muda tuu!
Usijute kusoma ulichosoma you can not take it back….! Songa mbele kama kuna fursa nyingine ichukue…

Usijali mtu na usijilinganishe na mtu kama uko hai na unapumua bado muda wa kushinda upo na upo usijali mazingira wala miaka na muda kwenda cha msingi wewe amini katika mapambano yako ni lazima kazi uipate!

Kama huna mishe kwa sasa anza kuzungusha bahasha yenye CV na kila kitu uwe tayari kufanya kazi hata ambayo ujasomea lakini uwe tayari kujifunza …usikubali kulala ndani wewe ni mwanaume pambana pambana usikubali kabisa…

Nyanyuka zungusha huo mwili kila ofisi hakika mkaa bure sio sawa na mtembea bure….Pambana mkuu utatoka
 
Mpaka nimelia [emoji24][emoji24][emoji24] Asante mkuu ubarikiwe
 
Mpaka nimelia [emoji24][emoji24][emoji24] Asante mkuu ubarikiwe
Kingine si sawa kujilinganisha na wadogo zako walimu, kwenye maisha kila binadamu ana timeline yake ambayo haifanani na mwingine, pita njia yako , wakati wa Mungu ni wakati sahihi usikate tamaa.

Kuna mdau hapo juu kasema kuingia kozi nyingine ukiwa huna connection baada ya kuhitimu ni wastage of time.
Amependekeza kama hiyo pesa ipo ifanyie uwekezaji kwa nidhamu.

Zingatia hilo....
 
Tatizo Sasa ushauri kama huu naupata too late kipindi Niko chuo hamna mtu wa kukumentor
Yaani unajikuta unajifanyia mambo mwenyewe tuu bila muongozo hasa Kwa sisi yatima tusio na wazazi ndugu hawahangaiki kabisa
Point.
 
Kwa niaba ya Mpwayungu Village, ahsante sana!!!🙏🙏🙏🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…