Nauona mwisho wa CCM

Okk
 
Ndugu anza kwanza kurekebisha 'r' na 'l' kwenye hizi hisia zako...
 
Kipindi hiki tutapata wapiga ramli wengi kweli.
Na hao wote wanaojifanya watabiri ama kuibua utabiri wao uchwara kipindi hiki cha ccm kujivua gamba, ni haohao wachumia tumbo ama marafiki zao wanufaika.

Ccm haiwezi kusambaratika kwa sababu ya kuondokewa na mumiani waliolifikisha taifa icu!
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini Sana siasa za Tanzania. Naweza nikasema tangu mwaka 2000.

Tangu wakati huo CCM haijawahi fiwa na mwenyekiti wake . Na hata taifa halijawahi kupoteza Rais.

Mwaka 1995 nikiwa bado Niko shule lakini historia inaonesha kulikuwa na mnyukano mkubwa Sana ndani Cha Chama kwenye uchaguzi wa Urais. Mkapa na Kikwete walichuana vilivyo.

Mwaka 2005 mchuano ulikuwepo lakini haukuwa mkubwa Sana.

Mwaka 2015 mchuano ulikuwa mkubwa mno na Makundi yalikuwa na nguvu Sana kitu ambacho kiliwafanya Wagombea kutembeza rushwa nje nje.

Mwaka huu Hayati JPM aliibuka kidedea kwa kile kinachosadikiwa kuwa ni vita kati ya Lowasa na Membe. Lakini wengine wanaamini ulikuwa ni mpango wa Mungu JPM kuongoza hili taifa.

2015 ndio mwaka ambao upinzani ulikuwa na nguvu Sana na huo mwaka CCM walimtumia hayati JPM kama daraja la kushinda uchaguzi.

"Mabango karibu yote yalikuwa *Chagua Magufuli mchapakazi, makali, mfuatiliaji, n.k". Hii yote ilikuwa ni kujibu mapungufu aliyokuwa nayo Kikwete kama vile ufisadi, dhaifu na mpenda safari Mara kwa mara.

Magufuli alipoingia madarakani alifanya kazi yake kadili ya uwezo wake wote.

Bahati mbaya ameondoka kabla ya 2025. Na hiyo 2025 iko karibu Sana. Wakati huu wananchi wengi wanataka utawala wa radha nyingine tofauti na ya hayati JPM. Hii Ndio kawaida ya watu kutaka kubadili radha ya mtawala kwa maana hakuna mkamilifu.

Hapa ndipo hoja yangu ilipo

Samia ameingia wakati ngumu Sana.

Kwanza, kumalizia Kazi alizo ziacha JPM.
Pili, kuwatuliza watu waliokuwa kwenye mbinyo wa JPM ili nao wapumue .
Tatu, kujitengenezea njia ilu 2025 apate turufu ya kugombea tena.

Nne, kuepuka mitego ya watu wanataka madaraka maana JPM alikuwa ameshawajua na hivyo walikuwa hawampi shida.

Tano kusimamia ustawi wa nchi. Ikiwemo usalama, uchumi, na huduma kwa jamii n.k.

Sita, kuendelea kuwafuta machozi na kuwa fariji walio kuwa Wana mpenda Hayati JPM. Ikiwemo familia yake, wateule wake, watu wa kanda ya Ziwa hususani wasukuma. Bila kuonesha chuki ama toka kwake Moja kwa Moja ama kwa wateule wake ama wafuasi wake.

Haya yote yanamkuta mda ambao alikuwa hajajianda

Samia akishindwa kufanya hayo yote ni wazi kwamba atapoteza kiti mapema Sana lambda akichuke kwa nguvu. Na huo Ndio mwanzo wa kifo Cha CCM.

Hadi Sasa utasikia mengi Sana hasa toka kwa waliokuwa na chuki na JPM walimsifia Sana Samia ili tu kuwabagaza waliokuwa wateule na wapenzi wa Hayati JPM. Hii ni hatari kwa usitawi wa Chama. Hii ni hatari maana hadi Sasa hakuna jambo ambalo unaweza sema Samia amewafanyia hao wapinzaniwa Hayati JPM.

Samia anakazi kubwa tumuombee. Maana wanao msifia wengi sio wanachama wa CCM lakini lengo lao ni kuwaweka njia panda Wana CCM waliojengwa na Hayati JPM . Mwaka 2025 ndipo utawaona Hawa waliokatishwa Tamaa ndani ya CCM wakikimbilia upinzani.

Samia chama kiko mikononi kwako. Kife ama kipone.

Pole kwa Msiba Mzito Rais Samia.

Hongera kwa kuwa Rais wetu
 
Kimbembe kipo kwenye kumpata katibu mkuu wa CCM, kuna watu wapo kusuka mipango kwa ajili ya 2025- 2030. Juzi Rais Samia alionya kwenye suala hili la urais 2025 sababu anajua kinachoendelea.

CCM ikipasuka yenyewe, kukatokea mgawanyiko mkubwa na upinzani ukiwa kwenye hali nzuri, basi hyo ndio itakua mwisho wa enzi wa CCM

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Kampeni za 2020 kwa asilimia kubwa zilifanywa na Mh Rais Samia.
2015 CCM ilisaka kura za kina mama kupitia Samia na ilizipata.
Magufuli na Samia wanetekeleza ilani ya CCM kwa kiwango cha hali ya juu.
ni uzuzu kufikiri CCM inaweza kuanguka 2025.
 
Katibu Mkuu ni Bashiru, kwani ulisikia amekabidhi ofisi tangu ateuliwe kuwa KMK, bado anafaa kuwa KM CCM ushindi uko palepale
 
Hapo kwamba kufuta machozi wasukuma, dah!!!🤣🤣🤣🤣
 
Baada ya kuona tabiri na maji mengi ya baraka yanaponya/kusaidia sasa kila mtu ni mtabiri /pastor mwenye maono lukuki.

Wanatumia njia zile zile ambazo lorries nyingi zilinasa kwenye barabara hizo.

Kutimia kwa tabiri juu ya mama Samia kusibadili kazi za watu kutoka uchimba chumvi kuja kuwa kina sheikh Yahya Hussein
 
Kampeni za 2020 kwa asilimia kubwa zilifanywa na Mh Rais Samia.
2015 CCM ilisaka kura za kina mama kupitia Samia na ilizipata.
Magufuli na Samia wanetekeleza ilani ya CCM kwa kiwango cha hali ya juu.
ni uzuzu kufikiri CCM inaweza kuanguka 2025.
Hii ni theory tu. Ukweli ni kwamba ccm changa iko kwenye wakati mgumu.

Japo naamini Samia anaweza akafanya kitu na chama kikapona.
 
CCM inaenda kufa natural Death kama Mwenyekiti wao
 
Itakuwa mwisho wa CCM kama tu CCM itameguka au wapiga kura wasiwe Watanzania...
 

CCM haiwezi kutolewa na chama pinzani, kuna factors mbili kubwa zinaweza kuitoa ccm na ikawa mwisho wake, 1) mpasuko ndan ya chama atleast iwe zaidi ya 2015 (sasa shida ya hapa wapinzani mpaka leo hakuna chma cha kurusha kadi kwao incase ccm itapasuka maaana ikipasuka lazima upinzani wachezewe ndumba alafu wajimalize wenyewe)

2) hii ndo kubwa na ya uhakika, wananchi wenyewe waamue kufanya vurugu hapa ccm itatoka ila kwa coverage ccm ilionayo na imani iliorudisha kwa wnanachi hmm miaka 60 tena
 

Hapa umejaribu kugusia vitu vimavyoweza kuingusha CCM.

Bado hujataja vizuri sababu zinazoiweka CCM madarakani. Na hizi ndizo zitaiondoa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…