Nauona mwisho wa CCM

Nauona mwisho wa CCM

Kama haya yooote yalitokea yet tukajenga miradi ya trillions then undeestand the guy is smart!

Hata mfanye vipi hamwezi kuondoa legacy yake
Hana legacy yoyote zaidi ya ufisadi wa hali ya juu
 
Kama haya yooote yalitokea yet tukajenga miradi ya trillions then undeestand the guy is smart!

Hata mfanye vipi hamwezi kuondoa legacy yake
Smart? Wastaaf wanazungushwa mafao yao mpaka leo sababu mifuko haina hela, fao la kujitoa sababu mifuko haina hela. Wanufaika wa bodi ya mikopo wanakatwa 15% hata wale waliosaini mkataba wa makato ya 8%.

Hapo u smart uko wapi wakat wenye haki zao hawapewi, alaf hela kibao zimepigwa kama hivyo
 
Kwa haya yanayofanywa na CCM waelewe tu sisi wananchi sio wajinga tuliyaona waliyoyafanya tukayaona aliyoyafanya meko na tunaona wanayoyafanya sasa waelewe sisi Watanzania sasa sio wajinga tena tuna akili na tunauelewa mkubwa sana tukutane 2025.
Uko sawa kabisa na ni muda wa wapinzani nao kutudanganya wakiwa na madaraka
 
Kama sio kuchafua uchaguzi mkuu uliopita leo ccm ingekuwa marehemu hayati siku nyingi sana
kosa kubwa la kihistoria lilifanyika 2015, ule muungano wa vyama vya upinzani ulipowakaribisha na kuwapa usukani wale vigogo!! Leo tungekuwa tunaongea habari nyingine.
 
Bila katiba mpya wananchi tususie chaguzi zijazo mpaka maombi yetu yakubaliwe!
Hao viongozi wenyewe wa upinzani wana njaa hawawezi kususia kwa hiyo hata wewe ukisusia haita saidia
 
Mwisho wa CCM utamalizwa na katiba mpya na tume huru pekee mkuu! Vinginevyo haya manyang'au yatazidi kutuminya..
Kwani hiyo katiba mpya itapitishwa na bunge lipi?

Idadi ya wabunge wa CCM bungeni unaifahamu wewe?

Rais ndo atateua wajumbe wa tume na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi,hatakama katiba iliyopitishwa na wabunge wengi wa CCM itamtaka apeleke jina kwanza bungeni,ambako nano kuna wabunge wengi wa CCM.....na atapita na kwenda kutekeleza agenda za CCM tumeni.

Na mahali popote penye serikali inayosimamia kila kitu.....hakuna kitu kinachokuwa huru isipokuwa serikali yenyewe.

Usijidanganye na usiwadanganye wenzako. CCM itatoka madarakani siku akipatikana mtu asiyekuwa mwanaCCM kuiongoza nchi hii na CCM yenyewe kitu ambacho ni kigumu mno.
 
Kama sio kuchafua uchaguzi mkuu uliopita leo ccm ingekuwa marehemu hayati siku nyingi sana
Usijidanganye Mkuu......CCM haikuwahi kushindwa katika uchaguzi wowote mkuu hasa uoande wa bara. Zanzibar sawa naweza kukuelewa. Hebu niaminishe kuwa Lisu alishinda uchaguzi wa 2020 ila kura zake zikaibiwa.
 
Kigwangala alitumia 172M kuandaa Kili challenge lakini pesa hizo hazijulikani zilitumikaje (hazina risiti).

Akaunti ya jeshi la zimamoto ilitumika kupitisha 261M. Yani watu walipiga "mchongo" wakakosa akaunti ya kupitishia, wakatumia akaunti ya zimamoto. Zilipoingia wakazitoa wakasepa. Just imagine watu wana ujasiri wa kupitisha pesa chafu kwenye akaunti ya jeshi? Halafu tunaambiwa mwendazake alinyoosha nchi...
Nitaelewa zaidi siku hizi kwere zikishindikana kutolewa ufafanuzi. Ila kwa mimi ambaye nafahamu mambo ya ki ukaguzi na lugha zake,sishabikii hii report coz najua wahusika watapelekewa na kutakiwa kujieleza kwakupeleka vielelzo. So nitakuwa wa mwisho kushabikia na kuita serikali ya awamu ya 5 ni ya kifisadi.
 
Angalia sasa hivi humu mitandaoni watu wanamshambulia mtu mmoja tu na ambaye ameshakufa hivyo hata kuendelea kumsema haisadii lolote,lakini cha kushangaza zaidi ni jinsi anavyosemwa huyo Marehemu utadhani kwamba kabla yake mambo yalikuwa sawa katika hii nchi kwamba yeye tu ndio aliharibu kila kitu.
Kusemwa halali yake pale alipokosea mbona yeye aliposhika madaraka aliwasema watangulizi wake? Na kinachosababisha asemwe sana alijiona kuwa yeye malaika hawezi kukosea na wapambe wake wakamsifu kwa nyimbo na mapambio pale akipobinya Uhuru wa kuongea
 
Kama haya yooote yalitokea yet tukajenga miradi ya trillions then undeestand the guy is smart!

Hata mfanye vipi hamwezi kuondoa legacy yake
Wanataka tuamini kuwa Magufuli alikuwa fisadi. Ila ukipita kila mahali mambo yamefanyika. Walinganishe awamu zilizopita na ya 5. Yaani ni kinyesi na mkate.
 
Shida sisi wananchi tuna maneno mengi sana hasa mitandaoni,lakini hatuna maamuzi juu ya nchi yetu,tunafarijiana tu humu,tunakosoana tu humu lakini mwisho wa siku hoja zetu zinaishia humu,wananchi ndo wenye maamuzi juu ya mstakabali wa nchi yetu,mfano kama wamekataa kutupatia katiba mpya,kwa nini tusisusie chaguzi? Kwani huwa tunalazimishwa kwenda kupiga kura? Wananchi wote tususe ijulikane tu wameingia madarakani pasipo uhalali,tuache kuwaimbia mapambio hasa wanapokuja majukwaani kujinasibu kuwa wamamefanya haya,kumbe wezi wakubwa wanafaidisha familia zao na kutaacha sisi tukiteseka mtaani!

Tatizo wengi wakiangushiwe buku 7, bia mbili na paketi ya sigara husahau yote . Bado tuna watu wenye akili za kuku , very sad 😡😡
 
Sawa tumekusikia.sasa baada ya CCM kufa ni chama gani icho kitakachoshika madaraka kwa mfano?
 
Hana legacy yoyote zaidi ya ufisadi wa hali ya juu
Pole yeye kapumzika kwa amani, kaumbika tayari na mimi moja naiona, jiulize wewe je natamani nikufahamu ni jua ila experience inaonyesha wa jinsi yako hata kwenye level ya family hawana cha kuonyesha, naomba Mungu isiwe na kwako ndiyo hivyo...
 
Pole yeye kapumzika kwa amani, kaumbika tayari na mimi moja naiona, jiulize wewe je natamani nikufahamu ni jua ila experience inaonyesha wa jinsi yako hata kwenye level ya family hawana cha kuonyesha, naomba Mungu isiwe na kwako ndiyo hivyo...
Naona umeandika huku machozi yakikutoka kisa siri za ufisadi wenu kufichuliwa na wana ccm wenzenu wasiytaka tabia za kifisadi
 
Back
Top Bottom