Nauli Feri: Mnyika, Hata Wewe?

Nauli Feri: Mnyika, Hata Wewe?

Tatizo ndio lipo hapo; kwanini wabunge walisahau kuhoji hayo wakati kamati ile inawasilisha ripoti yake bungeni na wakaridhika tu na takwimu za milioni tisa mapato kwa siku na milioni 5 surplus kwa mwezi?
Hapo nimekupata!
 
Angewaambia waenda kwa daladala kama huna nauli tembea kwa mguu asingekuwa dharau, lakini kupiga mbizi imekuwa dharau. Na leo serikali ikisema imeshindwa kuendesha kivuko. Watu watafanya nini?

Hivi ni wajibu wa serikali kuwasafirisha watu wa kigamboni? kama ni hivyo basi serikali hii ina ubaguzi wa hali ya juu sana. Maana kule kwetu sijaona usafiri wa serikali, tena mtu akiuugua wanamchukua kwa machela na maanisha machela ya miti miwili na fito, harafu wanatembea kilomita zisizopungua 30 kuifikia hispotali.

Sasa nauliza, hili la kigamboni ni wajibu wa nani ku make shua anafika eneo lake aliloamua kuishi. Mhhh
Kwa mtazamo wako finyu basi hata matatizo kama msongamano wa magari sio tatizo la serikali maana ni wajibu wa kila mtu kufika anakoenda bila kujali atafikaje. Pia kwa mtazamo wako hamna sababu kwanini watu wenye vyombo vya moto vya usafiri walipie matumizi halafu waenda kwa miguu wasilipie! Kwa maana hiyo hata wapita kwa miguu wawe na road licence.
 
Mchambuzi,

Asante kwa maoni yako, hoja zako ni nzuri kwa kuchochea mjadala ingawaje hauko sahahi katika maeneo kadhaa kama ambavyo nitakuja kueleza baada ya kwanza kujibu kauli za Magufuli hoja kwa hoja.

JJ

Tutashukuru sana kiongozi ukituweka sawa katika hili.
 
hata magufuli naye alipoongea na waandishi wa habari, alisema anamshangaa sana mnyika as if mnyika alikuwa peke yake kwenye hiyo hoja.
Hiyo inaonesha chadema ni kioo cha ccm, yaani ccm wakifanya jambo hawajali kuwa wanaccm wenzao wanasema nini maana wanajua kuwa kuna maiti tupu, wakifanya kitu hutathimini kwa kuangalia chadema wamesema nini. ndo maana hata baada ya wabunge wa dar kumpinga yeye ameona kama vile ni mnyika peke yake ndio wa kujibiwa maana wakielewana na mnyika basi wengine ni takataka.
 
Toka Magufuli atoe kauli nimekuwa kimya kumjibu nikiendelea na majukumu mengine jimboni na ya kitaifa. Magufuli hakujibu hoja, na badala yake ametoa kauli zisizokuwa na ukweli wowote dhidi yangu, kauli potofu zikiachwa zitaonekana milele kuwa sahahi. Kwa hiyo nimeamua kesho nizungumze na wanahabari kuweka msimamo wangu wazi ili kuweka rekodi muafaka: Mosi, nitajibu hoja kwa hoja, kwa masuala yote aliyoyasema dhidi yangu. Pili, nitaweka bayana kwanini nimeunga mkono kwa GN ihairishwe kutekelezwa, hoja za msingi zijibiwe na mabadiliko muhimu yafanyike.

JJ

Kwa hiyo sio kweli pale ubungo basi stendi, yani ya kwamba kumsindikiza tu jamaa yako tu kuingia kwa basi inabidi ulipe sh 200. Ha ha ha ha, hili kwa kweli kama ni kweli sijui, ....
 
Angewaambia waenda kwa daladala kama huna nauli tembea kwa mguu asingekuwa dharau, lakini kupiga mbizi imekuwa dharau. Na leo serikali ikisema imeshindwa kuendesha kivuko. Watu watafanya nini?

Kwa hiyo unadhani hiyo sh. 100 itatosha kuendesha hicho kivuko? Kwani tatizo ni nauli kuwa ndogo au ni ubadhirifu kwenye mapato ya kivuko?
 
Kwa mtazamo wako finyu basi hata matatizo kama msongamano wa magari sio tatizo la serikali maana ni wajibu wa kila mtu kufika anakoenda bila kujali atafikaje. Pia kwa mtazamo wako hamna sababu kwanini watu wenye vyombo vya moto vya usafiri walipie matumizi halafu waenda kwa miguu wasilipie! Kwa maana hiyo hata wapita kwa miguu wawe na road licence.

Ha ha ha ha
Weye mwenye mtazamo mpana, unatoka nje ya uwezo wako mpana na majawabu yake unaonekana una mtazamo finyu na butu. Kwa mtazamo wako mpana kuna siku utanunua petroli na kuiweka kwenye nyumba yako ya msonge ya nyasi na unapikia humohumo. Harafu ukiuungua humo na petroli yako utakuja hapa kulalamika kwanini serikali inaruhusu kukuuzia petroli, hivyo ikupe mahala pa kukuhifadhi kwa sababu ni wajibu wake. Ha ha ha ha
 
Haya sasa mnaona Mnyika naye anaanza kucheza Politics ktk swala kama hili. Alichosema Magufuli hakihitaji kujibiwa mwache akushangae, wewe tetea maslahi ya wananchi kama unaamini yamekiukwa na zungumza unataka iwe nauli za guta zipunguzwe au makosa yako wapi. Hizi habari za kurushiana maneno mkuu wangu hazifai hata kidogo maana Magufuli anaifanya kazi yake kama Waziri kofia ya pili mlomvika na sii kama Mbunge...

Mnyika sisi wanajanvi tunakutaji hapa.. na binafsi naamini kabisa kama sikukusikia vizuri ulichogomba ni matumizi ya matusi ktk lugha ya waziri lakini kama unasema Tsh 100 inatosha kuendesha mradi wa Pantoni kigamboni bila shaka utakuwa umepewa report mbaya sana na kusema kweli binafsi siamini hata wanaposema mapato kwa siku ni Mil 9. Hii sii kweli kwa sababu kila siku ina mauzo yake na huwezi kabisa kunambia kila siku mauzo yanalingana kuwa millioni 9 kisha ati salio surplus ni Millioni 5 kwa mwezi sijui baada ya matumizi yote ama kabla ya kulipa mishahara - Profit and loss account.

Sasa najua wewe unajua zaidi ya hayo nakuomba uje hapa utwambie kwa nini unaamini Tsh 100 inatosha kuendesha mradi ule bila kukisia isipokuwa kwa kutumia takwimu za mapato na uendeshaji wa kivuko hicho..
 
Kwa hiyo unadhani hiyo sh. 100 itatosha kuendesha hicho kivuko? Kwani tatizo ni nauli kuwa ndogo au ni ubadhirifu kwenye mapato ya kivuko?

Tanzania kila sehemu ni wabadhirifu sana, na hata hivyo kiuhalisia nauli hiyo haitoshi kuendesha kituo. Sh100 ni sawa cent 5 za EURO, ha ha ha na ukumbuke mafuta yananunuliwa kwa dolaaaa ama eurooooooo. Na hayauzwi bei rahisi kulingana na umasikini wako ama wangu.
 
Haya sasa mnaona Mnyika naye anaanza kucheza Politics ktk swala kama hili. Alichosema Magufuli hakihitaji kujibiwa mwache akushangae, wewe tetea maslahi ya wananchi kama unaamini yamekiukwa na zungumza unataka iwe nauli za guta zipunguzwe au makosa yako wapi. Hizi habari za kurushiana maneno mkuu wangu hazifai hata kidogo maana Magufuli anaifanya kazi yake kama Waziri kofia ya pili mlomvika na sii kama Mbunge...

Mnyika sisi wanajanvi tunakutaji hapa.. na binafsi naamini kabisa kama sikukusikia vizuri ulichogomba ni matumizi ya matusi ktk lugha ya waziri lakini kama unasema Tsh 100 inatosha kuendesha mradi wa Pantoni kigamboni bila shaka utakuwa umepewa report mbaya sana na kusema kweli binafsi siamini hata wanaposema mapato kwa siku ni Mil 9. Hii sii kweli kwa sababu kila siku ina mauzo yake na huwezi kabisa kunambia kila siku mauzo yanalingana kuwa millioni 9 kisha ati salio surplus ni Millioni 5 kwa mwezi sijui baada ya matumizi yote ama kabla ya kulipa mishahara - Profit and loss account.

Sasa najua wewe unajua zaidi ya hayo nakuomba uje hapa utwambie kwa nini unaamini Tsh 100 inatosha kuendesha mradi ule bila kukisia isipokuwa kwa kutumia takwimu za mapato na uendeshaji wa kivuko hicho..

Magufuli amewambia live kwa sentenso rahisi kabisa, kama namna gani basi waombe wepewe hilo feri waliendeshe kwa sh 100. Mbona wanaruka kimanga.
 
· Ibaneni serikali juu ya misamaha ya kodi kwa mwaka ambayo inakaribia asilimia 20 ya bajeti nzima ya mwaka, na muelekeze suala la subsidy ya kigamboni huko, sio kwa magufuli.
Hapa umetoa ushauri wa maana lakini unatafuta hasira nyengine za wenye kufaidika nayo.Kama Mnyika alivyokosa hekima kuhusu sakata la kivuko na hapa watu wa maana katika JF wanaweza wakakuwacha mkono wakifikiria nani anayefaidika na misamaha ya kodi na nani wanaoumia zaidi.
 
Mi nafikiri kuwa Kwa kweli tunaitaji ufahamu zaidi pale linapotokea jambo la kijamii i mean linaloigusa jamii ktk maradhi,chakula,education,transportation,mawasiliano,na mengineyo ambayo hawa viongozi wetu ndio haswaa tumewachagua ili kwa namna moja ama nyingine pale mambo yasipoenda sawa wao ndo wanakuwa mstari wa mbele kuihoji serikari au mamlaka husika kulikoni..? Sasa kwa hili ni kweli kabisa viongozi wetu wanapaswa watuelimishe kwa utulivu na umakini sana kwa sababu tumetofutiana katika jinsi ya kufahamu na kuelewa jambo,kuna watu wanaona waziri yupo sahihi na wengine wanaona wanaompinga wapo sahihi so ni lazima tupime uzito kwa kuangalia pande zote,jinsi ya kuwasaidia wananchi,kama makosa yalifanyika tunayatatua vipi na kama yanataka kufanyika tunayazuia vipi ili yasilete athari. Nampongeza sana sana Mchambuzi kwa uchambuzi wako yakinifu,na pia nampongeza Mh Mbunge Ndg Mnyika kwa kutujibu nini mwongozo wake. Asanteni
 
hapa umaetumia akili yako mwenyewe hujashikwa popote ndo maana umeweka uwazi,ila Magufuli naye amezidi kuropoka niliwahi kumsikia akiwatukana makandarasi wa barabara kisa wanadai pesa zao tena mbele ya [Pinda na sasa nasikia eti wabunge wanamshitaki kwakwe ili iweje?
 
Hili la kivuko cha Kigamboni linageuzwa kisiasa kwasababu wananchi wa Kigamboni ni muhimu sana kwa wanasiasa wetu au ni kwasababu wabunge hawa wa Dar wanajaribu kulishupalia kujikweza kisiasa? Mh. Magufuli aliweka wazi baadhi ya vivuko na gharama zake, kivuko cha Pangani nimewahi kukitumia sikuona wananchi wa Pangani wakilalamika kulipia shs 200; ukiangalia kwa undani wananchi wa Pangani hawana shughuli kubwa za kiuchumi ukilinganisha na Kigamboni, kumalaumu mh. Magufuli si suluhisho ukweli nauli ya shs 100 haiendani na wakati; hawa waheshimiwa wabunge wanajaribu kulitumia hili swala la kivuko kutulaghai wananchi, hawa si wenzetu; kwanza wangetueleza wamejiongezea vipi posho hadi shs 200,000 kwa siku? Hata kuongezeka kwa nauli ya feri Kigamboni inachangiwa na kuongezeka kwa gharama za serikali, posho za wabunge ikiwa ni mojawapo. Tusikurupuke tu kumlaumu mh. Magufuli kwa hisia zinazojengwa kisiasa tujaribu kuangalia ukweli wa suala zima kwa mapana na marefu.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Tanzania kila sehemu ni wabadhirifu sana, na hata hivyo kiuhalisia nauli hiyo haitoshi kuendesha kituo. Sh100 ni sawa cent 5 za EURO, ha ha ha na ukumbuke mafuta yananunuliwa kwa dolaaaa ama eurooooooo. Na hayauzwi bei rahisi kulingana na umasikini wako ama wangu.
Ndio maana nikawarudisha watu nyuma wakumbuke kwamba UDA ilikufa kwa sababu - WALISEMA -Nyerere sio mchumi huwezi kutoza watu Tsh 1 kwa usafiri japokuwa dollar ilikuwa Tsh17 hiyo ilikuwa kama senti 6 kisha ikapandishwa hadi Tsh 5 (sent 30) bado haikutosha leo hii watu tunalalamika na kuongezeka Tsh 200 ili kufikia senti 13 ya dollar... gharama za kuendesha Pantoni au gari Tanzania ni ghali sawa au kuliko Ulaya kwenyewe..

Jamani hata ile shilingi tano ya Nyerere ilikuwa kubwa mara ngapi ukilinganisha na Tsh 100 ya leo?... Ni sawa na senti ngapi 6 na ushee, watu wote wanalia ingawa binafsi hata hiyo Tsh 300 ya daladala bado ni ndogo sana haifiki hata senti 20 ya dollar...Halafu tunaambiwa ati nchi imeendelea tunapaa.. haya ebu wekeni kiwango cha daladala sawa na wakati wa Nyerere hata senti 30 tu ya dollar (Tsh 500) tuone hicho kilio cha wananchi -Tumeendelea!
 
Magufuli si suluhisho ukweli nauli ya shs 100 haiendani na wakati;
Serikali ilikuwa wapi muda wote wa miaka 14 isipandishe nauli kama walivyokuwa wanapandisha sehemu nyingine? Why now?
 
Serikali ilikuwa wapi muda wote wa miaka 14 isipandishe nauli kama walivyokuwa wanapandisha sehemu nyingine? Why now?
Why not now? maana ukifikiria hivyo basi hakuna siku inayotakiwa kufanya mabadiliko..Mzigo ukikuelemea unautua na Magufuli hakuwa wizara hiyo kwa miaka yote 14..tatizo letu nini hatutaki kulipa kwa sababu kasema maghufuli au kwa sababu ambazo yeye kazisema na kawakilisha hadi bungeni.. Kila waziri ana mtazamo wake ktk maswala wengine hawakujali na ndio maana Pantoni kibao nyuma zimekufa haraka nyingine karibu kuua watu..
 
Why not now maana ukifikiria hivyo basi hakuna siku inayotakiwa kufanya mabadiliko..Mzigo ukikuelemea unautua na Magufuli hakuwa wizara hiyo kwa miaka yote 14..

Why not now? Kwa sababu wangeweza kupandisha nauli kwenye hiyo miaka 14 iliyopita. Nini kilikuwa kinawazuia kupandisha nauli? Kama ni kupanda kwa mishahara ya wafanyakazi kama alivyodai magufuli, kwani hiyo mishahara imeanza kupanda mwaka huu? Kwani gharama za undeshaji wa kivuko zimeanza kupanda mwaka huu?

Hujanielewa. Serikali inatakiwa kufanya mabadiliko kwa kuendana na wakati. Sio kukaa miaka 14 bila kufanya chochote huku ikipoteza public money kama ruzuku ya kuendesha kivuko. Serikali ilikuwa wapi kipindi chote cha miaka 14 wakati taxpayers money ikiteketea pale feri?

The fact kuwa Magufuli hakuwa kwenye hiyo wizara, does not exempt the government from liability. Serikali sio Magufuli pekee. BTW Magufuli kaendesha hiyo wizara kwa miaka mingapi?
 
Tujue kwanza kinacholalamikiwa ndio tujadili mada!!
Issue sio kupanda kwa bei, bali mchakato uliotumika kuipandsha hiyo bei!!! Ulishirikisha wakazi wa pale??
Jana nimevuka pale nikapiga story na wale wahudumu, wakaniambia kua Bakhresa alilamikia kodi ya vibaiskeli vyake vya ice-cream basi ikashuka mpaka Tshs 300, tuseme kwakua wenye maguta hawana wa kuwatetea hivyo waendelee kutaabika tu???
Yaani bora upite na GX 110 utalipa less kuliko Guta, ni haki kweli hii???
 
Mchambuzi,

Asante kwa maoni yako, hoja zako ni nzuri kwa kuchochea mjadala ingawaje hauko sahahi katika maeneo kadhaa kama ambavyo nitakuja kueleza baada ya kwanza kujibu kauli za Magufuli hoja kwa hoja.

JJ

Wananchi wako wanalazimishwa kupanda Chai maharage kutoka Tangibovu hadi Goba. Abiria wanajazwa hadi kukosa hewa wakati ambapo kuna daladala zipo ila zinatakiwa zifuate foleni. Kisa ajira kwa wapiga kura wako vijana wanoshika kijidaftari na kutoza pesa wakisahau kadhia za abIria ambao pia nwapiga kura wako! Hili ni lako pamoja na maji hayopo Goba kwa urasimu wa kamati yenu fisadi.
 
Back
Top Bottom