Toka Magufuli atoe kauli nimekuwa kimya kumjibu nikiendelea na majukumu mengine jimboni na ya kitaifa. Magufuli hakujibu hoja, na badala yake ametoa kauli zisizokuwa na ukweli wowote dhidi yangu, kauli potofu zikiachwa zitaonekana milele kuwa sahahi. Kwa hiyo nimeamua kesho nizungumze na wanahabari kuweka msimamo wangu wazi ili kuweka rekodi muafaka: Mosi, nitajibu hoja kwa hoja, kwa masuala yote aliyoyasema dhidi yangu. Pili, nitaweka bayana kwanini nimeunga mkono kwa GN ihairishwe kutekelezwa, hoja za msingi zijibiwe na mabadiliko muhimu yafanyike.
JJ