Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
Nafasi ya uongozi (UBUNGE) kama ya kina Waheshimiwa Mnyika, Mtemvu, Ndungulile, Zungu, ni moja na nafasi za juu sana za uongozi katika Jamhuri yoyote ile. Wabunge wanawakilisha MATUMAINI, HOFU, SHABAHA na KIU ya wananchi. Ndio maana nafasi hii inahitaji utashi wa hali ya juu. Mbunge anatakiwa awe na sifa za ‘kiongozi bora' (sio ‘bora kiongozi'), vinginevyo ataishia kuwa kiongozi mpotoshaji, na anayeongoza au kutoa maamuzi kwa kufuata upepo, huruma kwa wapiga kura wake, pamoja na ‘maslahi binafsi'. Mbunge anatakiwa awe na sifa pamoja na:
· Consistency au uthabiti katika maamuzi na utendaji, na sio leo hili, kesho lile.
· Upeo na uelewa wa mambo anayoyasimamia au zungumzia kwenye umma.
· Ujasiri wa kuwaambia hali halisi wapiga kura wake, bila ya uwoga.
· Uwezo wa kutofautisha baina hoja/maamuzi ya kisiasa na yale ya kimantiki.
· Msimamo usiobadilika/kuyumba kutokana na upepo wa kisiasa.
· Ujasiri wa kusimamia kitu anachokiamini/maamuzi magumu.
· Uwezo wa kufikiri kabla ya kufanya maamuzi muhimu/kutoa kauli au msimamo mbele ya umma.
Katika sakata la Magufuli na nauli feri, ni dhahiri kwamba wabunge wetu hawa - Waheshimiwa Mnyika, Mtemvu, Zungu, Ndugullile, Mnyika na wengineo, wamepwaya katika sifa nyingi hizi. Kwa nafasi zao, wameonyesha ukosefu wa uthabiti (consistency) katika kauli/maamuzi yao, wamekosa upeo, wamekosa ujasiri wa kuwaambia ukweli wapiga kura wao bila ya uwoga, washindwa tofautisha hoja/maamuzi ya kisiasa na ya kimantiki, wameji expose kwenye mazingira ya kuweza badili misimamo yao siku za mbeleni, wameshindwa kuwa na ujasiri wa kuunga mkono maamuzi ya kimantiki ya magufuli, na wameshindwa kufikiri kwanza kabla ya kutoa kauli nzito kwa umma/wapiga kura wao. Ndio maana, kwa haya yote, Magufuli amewapiku, ingawa wanajidanganya mbele ya umma, kwamba wao ndio wapo sahihi, na magufuli ndio hayupo sahihi. Nitafafanua.
Feri ya Kigamboni ni kivuko ambacho kinaendeshwa kwa ruzuku kubwa sana ya serikali (yani government subsidy). Sina uhakika kama waheshimiwa wetu hawa wanalielewa hilo. Vinginevyo watumiaji wa kivuko kile wangekuwa wanalipa nauli kubwa sana kama kivuko kingekuwa kinaendeshwa na sekta binafsi, au hata kwa ubia kati ya sekta binafsi na serikali (yani Public –Private Partnership).
Waheshimiwa wabunge Mnyika na wengineo, kwenye sekta ya usafiri wa umma (madaladala) ambayo ipo chini ya soko huru, na kusimamiwa na Sumatra, mtumiaji wa chombo cha usafiri (daladala) kutokea Feri hadi Posta, anatozwa shillingi 300 (mia moja zaidi ya nauli ya Feri ya sh.200). Ikumbukwe kwamba umbali kutoka Feri Hadi Posta ni kama Kilometa 3, hivyo mtu ukiamua kutembea, unaweza kufanya hivyo. Kwa maana nyingine, ni hiyari kwa mtu kulipa nauli ya sh. 300 au kutembea. Lakini wengi huwa wanaamua kulipa sh.300, na shughuli za uchumi zinaendelea.
Lakini suala la kivuko cha ferry ni tofauti. Kivuko cha Feri hakiendeshwi na kanuni za soko huria. Umbali wa kivuko kile ni takribani kilometa moja kutoka upande mmoja hadi mwingine. Na tofauti na umbali kutoka Feri hadi posta ambao mwananchi ana hiyari ya kuchagua kati ya kutembea au kulipa nauli ya dala dala ya sh. 300, mwananchi hana hiyari kuchagua kupanda pantoni au kuongelea. Hivyo, lazima mwananchi alipe shillingi 200 kuvuka upande wa pili. Lakini ni muhimu nikasisitiza hili: miaka ya nyuma, serikali ilikuwa inatoa huduma ya kivuko kuanzia asubuhi hadi saa sita usiku. Lakini kwa sababu ya kujali wananchi wake, ikaamua huduma ile itolewe masaa 24. Tusisahau kwamba huduma hii ilitolewa kwa masaa 24 kwa kipindi kirefu sana kwa nauli ya shillingi 100. Na pia tusisahau kwamba pantoni lile likiwashwa asubuhi, halizimwi tena, hivyo kupelekea gharama za uendeshaji kuwa kubwa mno, in terms of fuel consumption (mafuta ya diesel). Sasa katika mazingira haya, Mheshimiwa Mnyika na wengine, tatizo lipo wapi serikali ikiamua kuongeza nauli kwa shillingi mia moja?
Waheshimiwa wabunge Mnyika na wengineo, tuseme basi serikali inajitahidi kukamilisha daraja la kigamboni ili kurahisisha usafiri kwa wakazi wa eneo lile. Je, mtakuwa na consistency katika hoja zenu? Kwani ni dhahiri kwamba, Daraja likikamilika leo, litakuwa na urefu wa kilomita sio chini ya saba (kati ya 7-10), na ramani zinaonyesha kwamba litaanzia maeneo ya Kurasini na Kushukia maeneo ya Kibada. Umbali huu wa kilometa saba, ni karibia mara saba ya umbali kutokea Feri hadi Posta ambako watu wanalipa nauli ya daladala sh.300. Daraja likikamilika, ni wazi usafiri kwa umma kutoka kurasini (DSM) hadi kibada (kigamboni), utaendeshwa chini ya kanuni za soko huria (madaladala), na wasafiri watalipa sio chini ya sh.300. Muhimu zaidi ni kwamba wananchi watakuwa na uhuru wa kuchagua kutumia daladala (chini ya soko huria) au pantoni (iwapo economics za pantoni zitakuwa bado zinaruhusu). Je, waheshimiwa wabunge, tuseme kwamba wananchi wafanye mgomo juu ya nauli ya kuvuka daraja kwa daladala (chini ya kanuni za soko huria) kwa sh. 300 au zaidi, mtakuwa upande gani, wa Sumatra au Wananchi? Ikumbukwe pia kwamba hili daraja kushukia Kibada haina maana msafiri amekamilisha safari yake kwenda upande wa pili wa feri, kwani umbali kutokea Kibada hadi upande wa pili wa feri (kigamboni) ni karibia kilometa 18. Sasa ukimjulisha umbali wa kivuko cha daraja (kilometa 7) na umbali wa Kibada hadi upande wa pili wa feri (kilometa 18), tunapata jumla ya umbali wa kilometa sio chini ya 25. Je, nauli mpya ya daladala chini ya soko huria kwa umbali wa kilometa 25 itakuwa sh 200 kama ya kivuko? Jibu ni hapana.
Waheshimiwa wabunge, kuna wakati bunge letu tukufu liliunda kamati maalumu kuchunguza gharama za uendeshaji wa kivuko cha kigamboni ili kubaini changamoto zilizopo, lengo likiwa ni kutafuta njia za kuboreshwa huduma ile kwa wananchi. Nyinyi kama wabunge mlikuwepo bungeni kuweza kuhoji mengi sana, lakini hamkufanya hivyo, na badala yake mnakuja kuyahoji masuala ya mapato barabarani. Kwa mfano, ripoti ya bunge ilibaini kwamba mapato kwa siku ni 9,000.000 (shillingi milioni tisa - enzi za nauli ya shillingi 100); Ripoti ile ikaendelea kusema kwamba ziada (yani surplus) kwa mwezi ni shillingi milioni tano. Lakini kamati ile haikutoa takwimu juu ya gharama za uendeshaji, na badala yake, ikatoa taarifa za masalio kwa mwezi. Sasa hoja yenu kwamba kuna ufisadi katika ukusanyaji wa mapato, kwanini hamkuijadili bungeni wakati kamati ile inatoa ripoti yake? Waheshimiwa wabunge, mngekuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuhoji ongezeko la Magufuli la sh 200 leo iwapo tu mngekuwa makini bungeni, kuhoji takwimu juu ya gharama za uendeshaji kwa siku katika kivuko cha ferry ni zipi. Au pengine hamkuwepo bungeni, au hamkuwa na upeo wa mbali, vinginevyo mlipoteza fursa nzuri sana, ambayo ingeweza kutuokoa na sakati hili linalochanganya wananchi. Wapiga kura wenu ni muhimu wakagundua uzembe wenu huu.
Kwa vile kamati ya bunge haikutoa takwimu juu ya gharama, nimejaribu kutumia nyingine ili angalau tupate makisio ya gharama kwa siku na kubaini yafuatayo i.e. if we work backwards: Mapato kwa siku sh. 9,000,000 (chini ya nauli ya sh.100) ; Masalio (surplus) kwa mwezi, sh.5, 000,000 (chini ya nauli ya sh.100). Hii ina maana kwamba masalio/surplus kwa siku ni Sh. [5,000,000] GAWANYA KWA [SIKU 30[, ambayo inatupa Sh. 166,666 kama masalio/surplus kwa siku. Hivyo basi, gharama kwa siku itakuwa: [Sh. 9,000,000] TOA [Sh. 166,666], ambayo ni sawa na na Sh. 8,833,333 kwa siku.
Waheshimiwa wabunge, kwa kutumia simple economics peke yake – gharama za kuendesha kivuko hiki ni 98% ya mapato kwa siku. Sasa tukianza kuangalia suala la kupanda kwa gharama za bidhaa muhimu kama mafuta n.k, JE, ni haki kweli kumshambulia magufuli, kisa, amepandisha nauli kwa sh. 100, hivyo kufanya masalio kwa siku yawe sh.333, 332 (laki tatu), badala ya Sh. 166,666? Inawezekana kinachoogopesha wabunge hapa ni the fact kwamba nauli imepanda kwa asilimia 100, kwani ulilitazama suala hili ki-asilimia, bila ya kuwa makini, kitakwimu, ongezeko la asilimia 100 ni kubwa sana. Vinginevyo, kwa sasa, shillingi mia moja ya kitanzania ni karibia na SENTI SITA katika dollar za kimarekani. Waheshimiwa, sote tunajua jinsi gani bei ya mafuta katika soko la dunia imekuwa inaongezeka kila kukicha. Serikali ilianza kutoa huduma ya kivuko kwa masaa 24 kwa kipindi kirefu sana kwa nauli ya Sh.100. Je, mnajua ilikuwa inatoa ruzuku kiasi gani? Na imechukua muda mrefu sana kabla serikali kupandisha nauli kwa shilling mia zaidi (sawa na SENTI SITA za kimarekani), katika kipindi ambacho bei ya mafuta duniani imepanda kwa mamia zaidi, ya hiyo senti sita ya dollar.
Kuna hoja pia kwamba Magufuli hakufuata Sheria, Je ni sheria ipi iliyo muhimu zaidi ya ile iliyopitishwa na Bunge ambalo nyinyi ni wawakilishi wetu - THE FERRY ACT ambayo ukiitazama, utabaini kwamba Magufuli na washauri wake, wameifuata mstari kwa mstari kabla ya kufikia uamauzi wa kuongeza nauli kwa shillingi 100? Waheshimiwa, na hasa John Mnyika - ambapo Ubungo ni Jimbo lako, kwanini haufuatilii suala la Kituo cha mabasi cha ubungo ambako kuna usumbufu na gharama zisizo na sababu kwa wananchi, pengine kuliko suala la kigamboni? Mfano, ili mtu uingie kituo cha ubungo kwa mguu, kwa dakika moja tu kumsindikiza ndugu yako anaesafiri ambae anahitaji msaada kwa sababu ya uzee, au ulemavu au umri mdogo (mtoto wa shule), unatozwa sh 200, je hamuoni kwamba hili nalo ni tatizo? Au ni kwa sababu, tofauti na mapato ya ferry ambayo hayapo chini ya manispaa, mapato ya Ubungo yapo chini ya manispaa ambako kwa nafasi zenu kama wabunge, mnakaa kwenye VIKAO kama madiwani kupitia/kupanga bajeti, na kula posho za vikao?
Kwanini huwa amhoji sheria zinazotumika na Sumatra kupandisha nauli za daladala ovyo? Au ni kwasababu mna imani kubwa sana kwamba soko huria huwa halifanyi makosa, na badala yake makosa hufanywa na serikali tu? Ni dhahiri kwamba kwenye usafiri wa umma ulio chini ya soko huria (daladala), wapo waheshimiwa wengi wenye maslahi binafsi. Vinginevyo, hata kwenye suala la nauli za mateksi, bajaji, ilitakiwa wabunge pia waibane serikali isimamie hilo, sio kuwaachia wamiliki wa vyombo hivi kuwaburuza wananchi watakavyo. Hata nchi za wenzetu, nauli za mateksi sio za makisio, ni kwa mujibu wa sheria.
Ushauri:
· Ongezeni juhudi katika kujenga hoja zenye mantiki, na mjifunze umuhimu wa kukwepa maamuzi ya kisiasa pale pasipotakiwa, vinginevyo mtachanganya wananchi.
· Elimisheni wapiga kura wenu kwamba uamuzi wa Magufuli ni sahihi, na toeni ahadi kwao kwamba mkienda bungeni mwisho wa mwezi huu, mtaenda kuhoji kamati husika kuhusu suala ambalo mlilizembea kweney vikao vilivyopita - takwimu juu gharama za uendeshaji wa pantoni kwa siku, ili muwe na legitimacy ya kuhoji mnayohoji leo juu ya shilling 200, vinginevyo, hamna that legitimacy as we speak.
· Ibabeni serikali juu ya misamaha ya kodi kwa mwaka ambayo inakaribia asilimia 20 ya bajeti nzima ya mwaka, na muelekeze suala la subsidy ya kigamboni huko, sio kwa magufuli.
· Litazameni suala la market failure kwa makini ili muelewe mapungufu, sio juu ya Ferry pekee, bali hata madala dala, bajaji, na mateksi.
· Vinginevyo, kama hamridhiki, nyinyi ndio watungaji wa sheria zetu, fuateni ushauri wa Magufuli kwamba, pengine Manispaa zichukue jukumu la kuendesha Ferry ili muelewe economics zake, kwani huko mkiwa kama sehemu ya madiwani, pengine mtatusaidia kutuondolea siasa kwa jambo ambalo limejaa mantiki tupu.
· Na Mwisho, Magufuli anastahili kuomba msamaha kwa kauli zake zilizokosa ustaarabu, lakini hastahili kubadilisha msimamo juu ya ongezeko la nauli, kwani uamuzi wake ni sahihi.
· Consistency au uthabiti katika maamuzi na utendaji, na sio leo hili, kesho lile.
· Upeo na uelewa wa mambo anayoyasimamia au zungumzia kwenye umma.
· Ujasiri wa kuwaambia hali halisi wapiga kura wake, bila ya uwoga.
· Uwezo wa kutofautisha baina hoja/maamuzi ya kisiasa na yale ya kimantiki.
· Msimamo usiobadilika/kuyumba kutokana na upepo wa kisiasa.
· Ujasiri wa kusimamia kitu anachokiamini/maamuzi magumu.
· Uwezo wa kufikiri kabla ya kufanya maamuzi muhimu/kutoa kauli au msimamo mbele ya umma.
Katika sakata la Magufuli na nauli feri, ni dhahiri kwamba wabunge wetu hawa - Waheshimiwa Mnyika, Mtemvu, Zungu, Ndugullile, Mnyika na wengineo, wamepwaya katika sifa nyingi hizi. Kwa nafasi zao, wameonyesha ukosefu wa uthabiti (consistency) katika kauli/maamuzi yao, wamekosa upeo, wamekosa ujasiri wa kuwaambia ukweli wapiga kura wao bila ya uwoga, washindwa tofautisha hoja/maamuzi ya kisiasa na ya kimantiki, wameji expose kwenye mazingira ya kuweza badili misimamo yao siku za mbeleni, wameshindwa kuwa na ujasiri wa kuunga mkono maamuzi ya kimantiki ya magufuli, na wameshindwa kufikiri kwanza kabla ya kutoa kauli nzito kwa umma/wapiga kura wao. Ndio maana, kwa haya yote, Magufuli amewapiku, ingawa wanajidanganya mbele ya umma, kwamba wao ndio wapo sahihi, na magufuli ndio hayupo sahihi. Nitafafanua.
Feri ya Kigamboni ni kivuko ambacho kinaendeshwa kwa ruzuku kubwa sana ya serikali (yani government subsidy). Sina uhakika kama waheshimiwa wetu hawa wanalielewa hilo. Vinginevyo watumiaji wa kivuko kile wangekuwa wanalipa nauli kubwa sana kama kivuko kingekuwa kinaendeshwa na sekta binafsi, au hata kwa ubia kati ya sekta binafsi na serikali (yani Public –Private Partnership).
Waheshimiwa wabunge Mnyika na wengineo, kwenye sekta ya usafiri wa umma (madaladala) ambayo ipo chini ya soko huru, na kusimamiwa na Sumatra, mtumiaji wa chombo cha usafiri (daladala) kutokea Feri hadi Posta, anatozwa shillingi 300 (mia moja zaidi ya nauli ya Feri ya sh.200). Ikumbukwe kwamba umbali kutoka Feri Hadi Posta ni kama Kilometa 3, hivyo mtu ukiamua kutembea, unaweza kufanya hivyo. Kwa maana nyingine, ni hiyari kwa mtu kulipa nauli ya sh. 300 au kutembea. Lakini wengi huwa wanaamua kulipa sh.300, na shughuli za uchumi zinaendelea.
Lakini suala la kivuko cha ferry ni tofauti. Kivuko cha Feri hakiendeshwi na kanuni za soko huria. Umbali wa kivuko kile ni takribani kilometa moja kutoka upande mmoja hadi mwingine. Na tofauti na umbali kutoka Feri hadi posta ambao mwananchi ana hiyari ya kuchagua kati ya kutembea au kulipa nauli ya dala dala ya sh. 300, mwananchi hana hiyari kuchagua kupanda pantoni au kuongelea. Hivyo, lazima mwananchi alipe shillingi 200 kuvuka upande wa pili. Lakini ni muhimu nikasisitiza hili: miaka ya nyuma, serikali ilikuwa inatoa huduma ya kivuko kuanzia asubuhi hadi saa sita usiku. Lakini kwa sababu ya kujali wananchi wake, ikaamua huduma ile itolewe masaa 24. Tusisahau kwamba huduma hii ilitolewa kwa masaa 24 kwa kipindi kirefu sana kwa nauli ya shillingi 100. Na pia tusisahau kwamba pantoni lile likiwashwa asubuhi, halizimwi tena, hivyo kupelekea gharama za uendeshaji kuwa kubwa mno, in terms of fuel consumption (mafuta ya diesel). Sasa katika mazingira haya, Mheshimiwa Mnyika na wengine, tatizo lipo wapi serikali ikiamua kuongeza nauli kwa shillingi mia moja?
Waheshimiwa wabunge Mnyika na wengineo, tuseme basi serikali inajitahidi kukamilisha daraja la kigamboni ili kurahisisha usafiri kwa wakazi wa eneo lile. Je, mtakuwa na consistency katika hoja zenu? Kwani ni dhahiri kwamba, Daraja likikamilika leo, litakuwa na urefu wa kilomita sio chini ya saba (kati ya 7-10), na ramani zinaonyesha kwamba litaanzia maeneo ya Kurasini na Kushukia maeneo ya Kibada. Umbali huu wa kilometa saba, ni karibia mara saba ya umbali kutokea Feri hadi Posta ambako watu wanalipa nauli ya daladala sh.300. Daraja likikamilika, ni wazi usafiri kwa umma kutoka kurasini (DSM) hadi kibada (kigamboni), utaendeshwa chini ya kanuni za soko huria (madaladala), na wasafiri watalipa sio chini ya sh.300. Muhimu zaidi ni kwamba wananchi watakuwa na uhuru wa kuchagua kutumia daladala (chini ya soko huria) au pantoni (iwapo economics za pantoni zitakuwa bado zinaruhusu). Je, waheshimiwa wabunge, tuseme kwamba wananchi wafanye mgomo juu ya nauli ya kuvuka daraja kwa daladala (chini ya kanuni za soko huria) kwa sh. 300 au zaidi, mtakuwa upande gani, wa Sumatra au Wananchi? Ikumbukwe pia kwamba hili daraja kushukia Kibada haina maana msafiri amekamilisha safari yake kwenda upande wa pili wa feri, kwani umbali kutokea Kibada hadi upande wa pili wa feri (kigamboni) ni karibia kilometa 18. Sasa ukimjulisha umbali wa kivuko cha daraja (kilometa 7) na umbali wa Kibada hadi upande wa pili wa feri (kilometa 18), tunapata jumla ya umbali wa kilometa sio chini ya 25. Je, nauli mpya ya daladala chini ya soko huria kwa umbali wa kilometa 25 itakuwa sh 200 kama ya kivuko? Jibu ni hapana.
Waheshimiwa wabunge, kuna wakati bunge letu tukufu liliunda kamati maalumu kuchunguza gharama za uendeshaji wa kivuko cha kigamboni ili kubaini changamoto zilizopo, lengo likiwa ni kutafuta njia za kuboreshwa huduma ile kwa wananchi. Nyinyi kama wabunge mlikuwepo bungeni kuweza kuhoji mengi sana, lakini hamkufanya hivyo, na badala yake mnakuja kuyahoji masuala ya mapato barabarani. Kwa mfano, ripoti ya bunge ilibaini kwamba mapato kwa siku ni 9,000.000 (shillingi milioni tisa - enzi za nauli ya shillingi 100); Ripoti ile ikaendelea kusema kwamba ziada (yani surplus) kwa mwezi ni shillingi milioni tano. Lakini kamati ile haikutoa takwimu juu ya gharama za uendeshaji, na badala yake, ikatoa taarifa za masalio kwa mwezi. Sasa hoja yenu kwamba kuna ufisadi katika ukusanyaji wa mapato, kwanini hamkuijadili bungeni wakati kamati ile inatoa ripoti yake? Waheshimiwa wabunge, mngekuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuhoji ongezeko la Magufuli la sh 200 leo iwapo tu mngekuwa makini bungeni, kuhoji takwimu juu ya gharama za uendeshaji kwa siku katika kivuko cha ferry ni zipi. Au pengine hamkuwepo bungeni, au hamkuwa na upeo wa mbali, vinginevyo mlipoteza fursa nzuri sana, ambayo ingeweza kutuokoa na sakati hili linalochanganya wananchi. Wapiga kura wenu ni muhimu wakagundua uzembe wenu huu.
Kwa vile kamati ya bunge haikutoa takwimu juu ya gharama, nimejaribu kutumia nyingine ili angalau tupate makisio ya gharama kwa siku na kubaini yafuatayo i.e. if we work backwards: Mapato kwa siku sh. 9,000,000 (chini ya nauli ya sh.100) ; Masalio (surplus) kwa mwezi, sh.5, 000,000 (chini ya nauli ya sh.100). Hii ina maana kwamba masalio/surplus kwa siku ni Sh. [5,000,000] GAWANYA KWA [SIKU 30[, ambayo inatupa Sh. 166,666 kama masalio/surplus kwa siku. Hivyo basi, gharama kwa siku itakuwa: [Sh. 9,000,000] TOA [Sh. 166,666], ambayo ni sawa na na Sh. 8,833,333 kwa siku.
Waheshimiwa wabunge, kwa kutumia simple economics peke yake – gharama za kuendesha kivuko hiki ni 98% ya mapato kwa siku. Sasa tukianza kuangalia suala la kupanda kwa gharama za bidhaa muhimu kama mafuta n.k, JE, ni haki kweli kumshambulia magufuli, kisa, amepandisha nauli kwa sh. 100, hivyo kufanya masalio kwa siku yawe sh.333, 332 (laki tatu), badala ya Sh. 166,666? Inawezekana kinachoogopesha wabunge hapa ni the fact kwamba nauli imepanda kwa asilimia 100, kwani ulilitazama suala hili ki-asilimia, bila ya kuwa makini, kitakwimu, ongezeko la asilimia 100 ni kubwa sana. Vinginevyo, kwa sasa, shillingi mia moja ya kitanzania ni karibia na SENTI SITA katika dollar za kimarekani. Waheshimiwa, sote tunajua jinsi gani bei ya mafuta katika soko la dunia imekuwa inaongezeka kila kukicha. Serikali ilianza kutoa huduma ya kivuko kwa masaa 24 kwa kipindi kirefu sana kwa nauli ya Sh.100. Je, mnajua ilikuwa inatoa ruzuku kiasi gani? Na imechukua muda mrefu sana kabla serikali kupandisha nauli kwa shilling mia zaidi (sawa na SENTI SITA za kimarekani), katika kipindi ambacho bei ya mafuta duniani imepanda kwa mamia zaidi, ya hiyo senti sita ya dollar.
Kuna hoja pia kwamba Magufuli hakufuata Sheria, Je ni sheria ipi iliyo muhimu zaidi ya ile iliyopitishwa na Bunge ambalo nyinyi ni wawakilishi wetu - THE FERRY ACT ambayo ukiitazama, utabaini kwamba Magufuli na washauri wake, wameifuata mstari kwa mstari kabla ya kufikia uamauzi wa kuongeza nauli kwa shillingi 100? Waheshimiwa, na hasa John Mnyika - ambapo Ubungo ni Jimbo lako, kwanini haufuatilii suala la Kituo cha mabasi cha ubungo ambako kuna usumbufu na gharama zisizo na sababu kwa wananchi, pengine kuliko suala la kigamboni? Mfano, ili mtu uingie kituo cha ubungo kwa mguu, kwa dakika moja tu kumsindikiza ndugu yako anaesafiri ambae anahitaji msaada kwa sababu ya uzee, au ulemavu au umri mdogo (mtoto wa shule), unatozwa sh 200, je hamuoni kwamba hili nalo ni tatizo? Au ni kwa sababu, tofauti na mapato ya ferry ambayo hayapo chini ya manispaa, mapato ya Ubungo yapo chini ya manispaa ambako kwa nafasi zenu kama wabunge, mnakaa kwenye VIKAO kama madiwani kupitia/kupanga bajeti, na kula posho za vikao?
Kwanini huwa amhoji sheria zinazotumika na Sumatra kupandisha nauli za daladala ovyo? Au ni kwasababu mna imani kubwa sana kwamba soko huria huwa halifanyi makosa, na badala yake makosa hufanywa na serikali tu? Ni dhahiri kwamba kwenye usafiri wa umma ulio chini ya soko huria (daladala), wapo waheshimiwa wengi wenye maslahi binafsi. Vinginevyo, hata kwenye suala la nauli za mateksi, bajaji, ilitakiwa wabunge pia waibane serikali isimamie hilo, sio kuwaachia wamiliki wa vyombo hivi kuwaburuza wananchi watakavyo. Hata nchi za wenzetu, nauli za mateksi sio za makisio, ni kwa mujibu wa sheria.
Ushauri:
· Ongezeni juhudi katika kujenga hoja zenye mantiki, na mjifunze umuhimu wa kukwepa maamuzi ya kisiasa pale pasipotakiwa, vinginevyo mtachanganya wananchi.
· Elimisheni wapiga kura wenu kwamba uamuzi wa Magufuli ni sahihi, na toeni ahadi kwao kwamba mkienda bungeni mwisho wa mwezi huu, mtaenda kuhoji kamati husika kuhusu suala ambalo mlilizembea kweney vikao vilivyopita - takwimu juu gharama za uendeshaji wa pantoni kwa siku, ili muwe na legitimacy ya kuhoji mnayohoji leo juu ya shilling 200, vinginevyo, hamna that legitimacy as we speak.
· Ibabeni serikali juu ya misamaha ya kodi kwa mwaka ambayo inakaribia asilimia 20 ya bajeti nzima ya mwaka, na muelekeze suala la subsidy ya kigamboni huko, sio kwa magufuli.
· Litazameni suala la market failure kwa makini ili muelewe mapungufu, sio juu ya Ferry pekee, bali hata madala dala, bajaji, na mateksi.
· Vinginevyo, kama hamridhiki, nyinyi ndio watungaji wa sheria zetu, fuateni ushauri wa Magufuli kwamba, pengine Manispaa zichukue jukumu la kuendesha Ferry ili muelewe economics zake, kwani huko mkiwa kama sehemu ya madiwani, pengine mtatusaidia kutuondolea siasa kwa jambo ambalo limejaa mantiki tupu.
· Na Mwisho, Magufuli anastahili kuomba msamaha kwa kauli zake zilizokosa ustaarabu, lakini hastahili kubadilisha msimamo juu ya ongezeko la nauli, kwani uamuzi wake ni sahihi.