Kifulambute
JF-Expert Member
- May 8, 2011
- 2,539
- 762
- Thread starter
- #41
Unajuaje kama unamuumiza moyo? Alikuambia? Afu hapo ulipoandika "xana" badala ya sana nimeshakuelewa. Bado we u mvulana sana. Nani alikuharakisha uoe?
Anaumia sana, nimekaa nae karibu sana na kumpa ushauri mara nyingi. Watu wamewahi kufikiria kumkimbia ama kumtelekeza kwa ajiri ya ugonjwa, nimekuwa nae kwa kipindi chote cha matatizo na nimekuwa nikifanya jitihada ili apone kwa kila anachopata. Anaumia sana na matatizo anayoyapata, kuna siku tulikaa kujadili haya matatizo na yeye anachoamini ni kuwa kuna dada ambaye nilikuwa nae pindi sijamuoa ndio anafanya haya yote, nimekuwa nikimsihi sana asiliweke hili mbele maana halina proof yoyote. Juzi alipougua tena akanambia "naenda nyumbani utaniuguza nikiwa kwetu labda yataisha haya darl", niliumia sana nikachukua usafiri haraka na kurudi Arusha ili niwe nae karibu.