Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Sio vichache anakosea hasa kutubagua watanzania WA ccm a Vyama vingine hili ni kosa namba moja analofanya....... Akiwa km raisi kila mkutano na matamko yake anaanza kuwasema wapinzani ili apigiwe makofi ndo anaendelea Sisi tunaJua yeye ndo kiongozi wa nji hii si wa ccm pekee. Hili kosa akiliacha nitaanza japo kusikiza matamko yake hayo
Sababu kwa sasa sisikilizi bora niangalie muvi za kina rufufu... Inanifanya NA mie ni mbague kuwa ccm wenyewe ndo wamsikilize raisi wao........ Mwambie nimesema

Changamoto kama hizi lazima zifanyiwe kazi,ndiyo mihemko nayoiongelea mkuu
 
Bado mpo mnaotaka Magufuli afanikiwe katika ajenda zake za kutisha na kunyanyasa watu?
 
Nae atamaliza Zama zake, tutamwita kwa kutoa Hesabu.

Wala msihangaike na mtu mliomchagua wenyewe.

Mwanadamu hujiona katika safari ndefu ya maisha kumbe wakati wake u mchache. Basi upitapo katika mapito yako ujichunge katika zama zako. Kwani kupitia hizo Zitakupa furaha ya milele au huzuni ya milele.

Rais aliwekwa kikatiba na wananchi wake, Muacheni afanye vile aonavyo huenda ndio njia yake bora ya kuiendeleza nchi yake. Na ifikapo nyakati za uchaguzi basi angalieni kuwa Yuafaa ama Laa.

Asomaye na Afahamu
 
Sasa ndugu katika akili ya kawaida hili jukwaa la siasa unaona kuna u-great thinker wowote(Niko tayari kukosolewa)
Dada/kaka shida zako zitatatuliwa na wewe mwenyewe tumia akili yako ipasavyo kujenga maisha yako na kutengeneza ajira kwa ndugu zako watanzania.
Mkuu uta nisamehe kama nitatumia Kauli mbaya.

Kwanza kabisa naamini hujui shida za watanzania , hujui maisha ya watanzania ndio maana unaongea kirahisi kama ungejua watanzania wana umasikini kiasi gani usinge ongea.

Pili naamini umekulia katika mikono salama ktk familia iliyojaa kwa kunufaika na lasilimali za wanyonge pasina kujua hujui shida ninini Lakini ni mfumo uliokukuza na kukuathiri ila ipo siku utajua Mungu aendelee kukupa maisha.

Tatu niambie ktk inchi isiyo kuwa na miundo mbinu ya kilimo kama sikimu za umwagiliaji na kilimo bora kwa ujumla na ina 88% ya wakulima inawwzaje kuendelea?

Mwisho naomba kufahamu Elimu yako inahusiana na nini?
Nesi au daktar wa mifugo au watu, elimu ya siasa, mhandis nikifahamu nitajua kwa nini unachukulia mambo kirahisi.
 
Mkuu hayo madawati ni bakuli lilitembezwa kama vile lilivotembezwa kwa ajili ya wahanga wa kagera na pesa kukwibwa
sawa, lakin si bakuli wametembeza wao! mbona akina lowasa na sumaye walipokuwa mawaziri wakuu yaliwashinda kutembeza hilo bakuli watoto wakapata madawati??
 
Nae atamaliza Zama zake, tutamwita kwa kutoa Hesabu.

Wala msihangaike na mtu mliomchagua wenyewe.

Mwanadamu hujiona katika safari ndefu ya maisha kumbe wakati wake u mchache. Basi upitapo katika mapito yako ujichunge katika zama zako. Kwani kupitia hizo Zitakupa furaha ya milele au huzuni ya milele.

Rais aliwekwa kikatiba na wananchi wake, Muacheni afanye vile aonavyo huenda ndio njia yake bora ya kuiendeleza nchi yake. Na ifikapo nyakati za uchaguzi basi angalieni kuwa Yuafaa ama Laa.

Asomaye na Afahamu
mkuu umeongea kwa swaga za kichungaji... safi sana.
 
sawa, lakin si bakuli wametembeza wao! mbona akina lowasa na sumaye walipokuwa mawaziri wakuu yaliwashinda kutembeza hilo bakuli watoto wakapata madawati??
Ukiishi ndani ya maji huwezi kuepuka kulowana
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?

Boss Lady. Capo di tutti signore of JF: check yourself before you wreck yourself.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom