MSIMISEKI SENIOR
JF-Expert Member
- Nov 1, 2014
- 459
- 287
Watu wenye hekima huwa wanawaonya kina Maxence kuhusu kucheka na watu wanaongea pumba na matusi kupitia nyuma ya keyboard lakini hawakusikia, ndiyo malipo ya kulea ujinga wanaanza kuyapata. Watu wanashangaa nini hata Marekani huko mnakotaka kukimbilia ukimbizi mitandao mikubwa kama yahoo inapelekeshwa na serikali itakua hapa? Watu tujifunze kuwa uhuru una mipaka yake, maana kama una uhuru wa kufanya lolote basi ua mtu uone kama huo uhuru wako utafuatwa, sentensi ya Uhuru inasema "una uhuru wa kufanya lolote ili mradi usivunje sheria" kwanini waliongeza hilo neno kuvunja sheria??? lakini MSIMISEKE SENIOR hapa kuna wengi wanajifanya wanajua huko hawajaverify hizo personel details zao. Mbaya zaidi wanaishi bongo na wanatumia mtandao wa bongo. Kwanini wasiende kutapika hizo nyonga zao katika mitandao ya kimataifa maana huko ndiko wataianika serikali labda na wao kiingereza kinawashinda.
Umeongea vyema.
Watu wanasahau hata huko wanakodhani kuna uhuru wa kuyoa maoni wafanye rejeo la mmiliki wa Mtandao wa Wikleaks ni kitu gani kilimpata baada ya kutoa taarifa za kiuchunguzi na kijasusi za baadhi ya mataifa makubwa. Hadi leo yupo mafichoni