Nataka nikope benki niwekeze UTT

Nataka nikope benki niwekeze UTT

Nimeona UTT inajadiliwa sana kuna mmoja amesema ukiwekeza mil 50 kila mwezi utapata faida ya 400k,

Nataka nikope mil 50 NIWEKEZE UTT ili zile faida za 400k

Kila mwezi nirejeshe benki mwisho wa siku niwe na mil 50 zangu UTT na deni nimemaliza

Riba ya benki (wastani wa 18% kwa mwaka) ni kubwa kuliko faida ya UTT (wastani wa 13% kwa mwaka. Utapata hasara.
 
Ila huyu mleta mada huenda ana hoja.

Hebu tu assume umekopa hiyo 50m ukajenga nyumba ya kupanga. Je, ndani ya miaka 7 itakua imerudisha hela ili uanze kupata faida?
Bado angalau miaka 12 ndio utaanza kuona faida
 
Kama hiyo 200K ni kwa mwezi.

200 000 ×(15×12)= 36,000,000.

Au nakosea.
Upo sahihi. Lakini kimahesabu ATAKUA ameweka cash zake 36m. Hizo cash zinaleta riba. Ikiwa hatachukua hizo riba, ATAKUA na jumla ya 102M at the end ya miaka 15.

Unaweza kuwatembelea utt kupata uelewa zaidi. Pia unaweza kuuliza ChartGPT maswali inafafanua vizuri.

P.s. utt ni co ya serikali yenye ukwasi wa zaidi ya 1.6 trillion....
 
Riba ya benki (wastani wa 18% kwa mwaka) ni kubwa kuliko faida ya UTT (wastani wa 13% kwa mwaka. Utapata hasara.
Ahsante kwa elimu mkuu HATA m nilitaka kujiulizaa bank ipi inatoanfaida zaidi ya utt
 
Piga hesabu hatua kwa hatua tuone plus interest unazolipa na unazotoa tuone kama ni kweli utabakia na plus au minus....

Financial institutions sio mataahira kuacha loopholes kama hizi na kama zipo basi watazifinya...
 
Nimeona UTT inajadiliwa sana kuna mmoja amesema ukiwekeza mil 50 kila mwezi utapata faida ya 400k,

Nataka nikope mil 50 NIWEKEZE UTT ili zile faida za 400k

Kila mwezi nirejeshe benki mwisho wa siku niwe na mil 50 zangu UTT na deni nimemaliza
Unacheza pata potea ndugu ..marejesho bank sio chini ya milion kadhaa.maana ukikopa 10m roughly marejesho ni 800-900k
 
Ukiweka utt 50m
Kwa mwezi utapata faida ya 500k
Kwa mwaka ni 6m

Je marejesho ambayo utakuwa unarudisha kwenye huo mkopo utatoa wapi???

Na kama utakuwa unakatwa kwenye mshahara then what?

Ushauri wangu weka kila mwezi laki mbili kwa miaka 15 utapata si chini ya 55m
Hisabati ulipata ngapi!!?????
 
Swali, UTT wanafanyia kazi gani hizo fedha katika kuzizalisha?
 
Kiufupi huko mkopo wa kulipa laki nne kila mwezi kwenye 50M haupo. Hapa nimekuwekea tu break down ya iwapo mkopo utaulipa kwa miaka 20, ina maana rejesho litakuwa 771,700 kila mwezi na mwisho wa mkopo utakuwa umelipa riba ya sh 135,196,898. Ina maana kwa rejesho la 400,000 unaweza kulipa kwa miaka 25 labda. Na hakuna benk inatoa mikopo ya hivyo isipokuwa ile ya nyumba (mortgage). So wazo lako haiwezekani. Labda uweke bond uikopee
 

Attachments

  • Screenshot_20250724-125336_1.jpg
    Screenshot_20250724-125336_1.jpg
    976.7 KB · Views: 18
Hapo bank watakula hela nyingi, shida ni riba ya bank ni kubwa
 
Kwa bond za bot unapata almost 7,415,393.89 kwa mwaka kwa interest ya 25 kwa 15.75 ebu jaribu kulinganisha apo
 
Nimeona UTT inajadiliwa sana kuna mmoja amesema ukiwekeza mil 50 kila mwezi utapata faida ya 400k,

Nataka nikope mil 50 NIWEKEZE UTT ili zile faida za 400k

Kila mwezi nirejeshe benki mwisho wa siku niwe na mil 50 zangu UTT na deni nimemaliza
Ningekuwa mimi ndiyo wewe ningekopa hiyo hela then ningewekeza kwenye cryptocurrencies zenye future techs ambazo zitausaidia ulimwengu very soon current financial system itakapocollapse. Nina uhakika ungekuwa billionaire na watu wangesema wewe ni freemason. Elewa sijasema usiwekeze UTT! Ila kumbuka high risks high returns na uwekezaji kwenye cryptocurrencies inabidi uwe na uelewa tena mkubwa. if huna uelewa na hauko tayari kujifunza then nakushauri please usijiingize kwenye cryptocurrencies please wekeza tu UTT.
 
Ningekuwa mimi ndiyo wewe ningekopa hiyo hela then ningewekeza kwenye cryptocurrencies zenye future techs ambazo zitausaidia ulimwengu very soon current financial system itakapocollapse. Nina uhakika ungekuwa billionaire na watu wangesema wewe ni freemason. Elewa sijasema usiwekeze UTT! Ila kumbuka high risks high returns na uwekezaji kwenye cryptocurrencies inabidi uwe na uelewa tena mkubwa. if huna uelewa na hauko tayari kujifunza then nakushauri please usijiingize kwenye cryptocurrencies please wekeza tu UTT.
Sasa hela yakukopa uweke tena kwenye risk kubwa?
 
Back
Top Bottom