Nataka niache advance PCB nahisi imenishinda

Nataka niache advance PCB nahisi imenishinda

Nenda kasome clinical officer tu

Sent from my TECNO W5 Lite using JamiiForums mobile app
 
Mm mock nilipata four, bit still necta nkapa BBD in PCB, nilikomaa na wale mabundi watabe wa tuit za mgote mbuga, mandia na issue boy, nkatoboa saiv nipo chuo kikuu sec yr. Kaza buti usikate tamaa necta co ngum kivile km tahosa, jikane utatoboa. Jamaa angu alipata moko zero km wew, bt necta kapga 3 yupo chuo now. Kaza upate hata DDD zote chuo unaenda na mkopo unaramba.
JIKANE Dogo
 
Sio kweli kwamba wanafaulu biology wanakalili! Unawezaje kukalili mambo mengi kiasi kile? Ukweli ni kwamba wana uwezo mzuri upstairs!

Lazima ukariri mkuu. + good upstairs.
kwanini??? majina ya vitu mbalimbali hayaitaji kuelewa tu lazima umeze arafu kuelewa ndio kuna weza fanunua au elezea.
 
Mm mock nilipata four, bit still necta nkapa BBD in PCB, nilikomaa na wale mabundi watabe wa tuit za mgote mbuga, mandia na issue boy, nkatoboa saiv nipo chuo kikuu sec yr. Kaza buti usikate tamaa necta co ngum kivile km tahosa, jikane utatoboa. Jamaa angu alipata moko zero km wew, bt necta kapga 3 yupo chuo now. Kaza upate hata DDD zote chuo unaenda na mkopo unaramba.
JIKANE Dogo

Kama ulivyo mwambia Dogo ajikane. Weka malengo. weka timerable vizuri kisha komaa, soma na usisite kuwasumbua nguri hapo shule, sometimes wanafunzi wanaweza kueleweshana vizuri zaidi ya mwalimu.
 
Yaah najua kukariri sana ila nashangaa chem imekuwa complicate sana kwangu physics ndo balaa markd kubwa nilipataga 38

Dogo Physics na Chemistry hutakiwi kumeza tu. Uelewa ni muhimu sana. Formula ndio za kukalili na zinatumika wapi, otherwise kinachofuata hapo ni kuelewa unatumiaje na wapi.
 
muoga wa jf, what's your Plan B endapo utagonga mwamba kwa wazazi suala la ku-drop na kusoma alternative course?!

Kwangu mimi naona huo ndio uamuzi wa busara zaidi lakini ukigonga mwamba; vuta nguvu upya na sahau suala la kukata tamaa! When that happens; tenga muda mfupi sana kwa Physics manake itakupotezea muda wakati productivity ya huo muda inaweza kuwa very minimal. Kinyume chake, wekeza muda kwenye Chemistry na Biology. Trust me, Chemistry ni rahisi sana kufaulu kwa sababu watungaji wa mitihani hawana ubavu wa kwenda mbali sana na vitabu!

Hapo juu umezungumzia uwezo wako wa kukariri! Biology unaweza kukariri lakini Chemistry hata kama kukariri kunalipa (am not sure manake mimi kichwa changu ni kibovu kweli kweli linapokuja suala la kukariri) muhimu kwa Chemistry ni kuzielewa concepts mbalimbali. Chagua topics chache za kuanza nazo ambazo ni rahisi pia kuzielewa. Hizi ziwe zile ambazo zina-cover sehemu kubwa ya mitihani! Wekeza muda wako huko and trust me, hadi May 2018 unaweza kukuta unatoka na angalau FDD.

Ikiwa FDD itakukosesha kusoma Bachelor bado unaweza kwenda kusoma Diploma huku ukiwa na good Form VI results itakayokutofautisha na wenzako waliotoka FIV au waliofeli FVI. Hii good FVI results ndio mtaji wako wa baadae utakapo-apply bachelor with equivalent qualification.

NOTE: Don't give up kabla hujapata formal alternative!!

I repeat, ipunje muda Physics manake Physics haitambui kabisa jitihada za mtu especially kama mtu mwenyewe ni wa PCB!!

In addition, sijui una muda gani hapa JF! Kama hujaizoea sana JF basi at least for now till June 2018 na yenyewe ikalie mbali kama Physics!! JF ni Gogo Zembe! JF ni very addictive!! Though you can learn a lot through JF but for now you don't have luxury time for it!!

Don't say hukuambiwa utakapojikuta unalazimika ku-balance muda wako kwa masomo matatu-- Chemistry, Biology & JF huku JF likiwa ndiyo favorite subject linalohitaji more attention!!!
Mkuu umemaliza kila kitu,Mimi nilisoma PCB miaka ya nyuma,na nilifanya haya unayomshauri dogo baada ya kuona physics inanitesa,nikawa naisoma kwa wiki Mara mbili au tatu tu,nguvu zote zilikuwa kwenye bios na chemia.nashkuru mungu nilipata principle zangu mbili za bios na chemistry kwa SDD. Na physic nikapata subsidiary.ukisoma PCB kweli kuna muda unaona division zero inakuja,but usikate tamaa,matokeo yakitoka huwezi amini maajabu utakayofanya Ikiwa utafanya kama mkuu anavyokushauri
 
Kweli ukijifanya ukomae utajikuta unaleta aibu tu bora ungekuwa cbg ningekwmbia ukomae hapo pcb utatoka na prncple pass moja tu.
 
Kweli ukijifanya ukomae utajikuta unaleta aibu tu bora ungekuwa cbg ningekwmbia ukomae hapo pcb utatoka na prncple pass moja tu.
 
Pole sana Mkuu, Naona umetumia muda mwingi kabla ya kuja na hayo mawazo.

Sijui nikushaurije! Ungekuwa ndo unaanza ningekwambia ujaribu Comb ya CBG.

AU Fanya hivi, Omba Diploma za Afya (CO,PHARM,RADIOLOGY au LAB)

Ukipata ndo uanze kufikiria.
Kama ameshindwa masoma A Level hiyo diploma ya CO ataweza?bora akasome business administration au community development
 
Kama ameshindwa masoma A Level hiyo diploma ya CO ataweza?bora akasome business administration au community development
Hahha...Kwenye Diploma, huwa Masomo yanasomwa kwa kipindi cha Miezi Sita (Semister)...Mwanafunzi akimaliza Semister anayaacha masomo/Mada hizo/hayo na kuanza mengine.
So, Humpunguzia mzigo sana.

Tofauti na Advance; ambapo unasoma kwa Miaka Miwili vitu vingi. Na Mwisho wa Siku unafanya mtihani ambao hujui maswali yatatoka wapi kwenye Topics zote ulizosoma.

Kwa huo utofauti, Diploma inaweza kuwa rahisi kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaonekana hukujiandaa pindi unasubir kwenda advance yaani hukusoma tution, chamuhimu tafuta tution anza kupiga, tumia mudawako mwingi katika kusoma then mambo yatakua sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCP Enginer sijui kama aliuona huu uzi..

Physic niliiacha kuisoma tangia nikiwa form 2, form 4 nikatoka zangu na 4 ya 31... Sasa hvi mim ni mjumbe kwenye bodi ya Madalali

Phys ni soma ambalo lipo kwenye damu za watu, usi force maji kupanda mlima
 
Write your reply...badala ya kusoma muda huu upo jf
alafu unataka maajabu 😎 PCB lazima ikutoe jasho
 
Back
Top Bottom