ubinaadamukwanza
JF-Expert Member
- Nov 5, 2016
- 222
- 198
Wengi humu waliinishwa kuwa Uarabu ni rangi.
Kama ni rangi tu, mbona wapo wengi wanakuwa "Waarabu", wake kwa waume!, jionee:
![]()
![]()
View attachment 471295
![]()
![]()
![]()
Picha zote kwa hisani ya google "mkorogo".
Hongera kwa kuleta ufahamu huu.
Waarabu "Asil" sio weupe kama wengi wanavyofikiria. Asili ya Waarabu wametokea Afrika. Baba wa Waarabu katokea Babiloni (leo Iraq), na Mama wa Waarabu ni Mwafrika halisi kutoka Afrika. Waarabu ni wajomba zetu. Waarabu ni kizazi kilichochanganya mataifa, wapo Waarabu weusi kama Jaluo, na wako wengine ni maji ya kunde na wengine ni weupe haswa wale waliochanganya wakati walopowateka Waroma, kuna mchanganyiko pale Tatar alipotawala Uarabuni nk.
Tabia ya "Mkorogo" inahusiana na ugonjwa wa akili unaojulikana kama "Borderline Personality Disorder au BPD".
Pia katika project Waamerika Weusi walioandaliwa ilikuwa ni kubadilisha fikra zao na wajione kuwa wao ni watu duni, na kuonyeshwa kuwa mtu mweupe ndio aliyebarikiwa. Project hiyo imefanikiwa sana. Wengi wamechoma nywele zao, kujichubua na kuvaa nywele za bandia za kihindi na kizungu zilizotengenezwa na plastic.
Ndio maana leo tuko pia Waafrika wenye fikra duni wanavaa suti na tai na kupandisha bendera ya Kizayuni ya Ubaguzi wa Israel hapa Tanzania. Utumwa wa kisasa. Tumepoteza maadili. Kwa ajili ya ubishi, matamanio binafsi, ujinga tunakuta tunasaliti na tunarudi kwenye utumwa bila ya kulazimishwa.
