Nina umri usiozidi 31, nina watoto 4 kila mmoja na mama yake, wa kwanza nilimpata nikiwa sekondari, wa pili nikiwa chuoni, wa tatu nikiwa internship na wa nne nikiwa chuoni tena. Wawili kati ya hao wadada wameshaolewa, natamani sana kuoa sasa. Nilipowaendea hao wawili waliobaki kila mtu kwa nafasi yake walikubali ombi langu ila hakuna anayetaka kuletewa mtoto wa nje. Nimeshindwa nifanyaje kwasababu siwezi kuwa mbali na wanangu, hivi sasa nimeshawachukua wawili wapo boarding school na hao waliobaki natarajia kuwachukua ASAP. Wanajamvi natamani sana kuoa lakini mambo ndo hivo yalivyo. Nifanye je?