Ni ushauri mzuri sana lakini nakushauri uutathmini kwa maandiko ya Biblia kinyume na hapo ni Busara tu za mwanadamu ambazo Mungu ameziita UPUMBAVU!! Kwa sababu unashauriwa na MTU, usiende kwa watumishi wanaojiita MITUME; Lakini Neno linasemaje, "Kanisa linajengwa chini ya Misingi ya MITUME NA MANABII" Na pia Usiende kwa watumishi wanaohubiri sana utoaji! Nakukumbusha tu kwamba usiposisitizwa na kufundishwa vyema kuhusu UTOAJI NA NAMNA YA KUTOA, Amini usiamini hutatoa na usipotoa Hapo ibada ni batili, kumbuka Mungu amekataza kabisa kujaribiwa na MTU, lakini sehemu moja tu ameruhusu for purpose amesema; "Nijaribuni Kwa Matoleo Muone kama Sitafungua Madirisha ya Mbingu na kuwamwagia Mibaraka tele..." Lakini pia baraka za Baba yetu wa Imani zilikuja Kwa kutoa (tena mwanae Isaka wa Pekee) na Yesu Mwenyewe akajitoa sadaka kwa ajili yetu, hivyo kupinga makanisa yanayosisitiza utoaji tafakari kwanza na Muulize Roho Mtakatifu atakufunulia namna ya kufanya.Na ukishauriwa Kupiga makanisa yanafanya Miujiza tafadhali Roho mtakatifu na akupe hekima ya kutambua miujiza ya Mungu na ile ya Kishetani, kwani Maandiko yako Wazi kuwa Yesu Kristo tunayemfuata hakuwahi kuhubiri pasipo kutenda miujiza ili kuwavuta wasioamini waamini baada ya kuyaona matendo Makuu ya Mungu kupitia kwa Mtumishi wake, kadhalika hata mitume wake aliowaacha nao hawakuwahi kuhubiri Injili chukwuchukwu ila iliyoambatana na ishara na maajabu ili kuwavuta wasioamini waokoke na kutubu dhambi zao.Unaonaje mtumishi anapokusisitiza kila siku kuwa Yesu anaokoa na kuponya halafu katika utumishi wake hata siku moja hujawahi kushuhudia akiokoa(kumtoa mtu katika maisha ya dhambi) wala kumponya walau Mgonjwa wa mafua tu!!? Roho Mtakatifu na akutafakarishe na hili pia kabla ya kufanya uamuzi.UBARIKIWE SANA!