Nataka kuanza kwenda kanisani

Nataka kuanza kwenda kanisani

Nakushauri ukamuone Mama Zungu (Rwakatare), Zungu Kakobe, Zungu Mwingira, kama hawa hauwataki pale Mabibo karibia na baa ya Rangers kuna wale waNigeria (wakimashaka) wanahubiri neno la Mungu pia tena wana maajabu ya balaa kama vile nyoka anakutoka tu ghafla mfukoni, mtu kuanguka (msanii) toka juu ya mti huku akilia alitumwa na Mungu kuna wanigeria watamsaidia kuokoka ndipo akaja pale. Mbona makanisa ya hajabu yako mengi tu. Kama unataka ni pm nije nikuchukue nikupeleke ila mwezi ujao kwani kwa sasa niko mbali kidogo.
makanisa kwaajili ya mazingaumbwe siyataki wala ya kulipa hela ili Mungu ajibu sitaki. Nataka kanisa dogo lenye imani ya kweli na unyenyekevu kwa Mungu
 
Maana halisi ya kanisa imo rohoni mwako, ukimkubali na kumkiri Yesu Kristo kwa roho na kwakweli kuwa Bwana na Mwokozi wako, kule kanisani ni mahali tu pakukutana na wana kanisa wengine
Tahadhari; Epuka makanisa yanayohubiri miujiza tu Siku zote
Epuka makanisa yenye viongozi wanaojiita mitume na manabii
Epuka makanisa yenye kusisitiza utoaji zaidi kuliko kuhubiri neno la Mungu
Unaweza kusali Anglikana, Katoliki, Lutheran na Pentekose lakini huko kwingine manabii na mitume wenye A.K.A nyiiingi kuwa makini nako, hasa kwakuwa umchanga kiroho

Nimeupenda ushauri wako.
Na sabato pia ni kanisa lenye misingi mizuri.
 
makanisa kwaajili ya mazingaumbwe siyataki wala ya kulipa hela ili Mungu ajibu sitaki. Nataka kanisa dogo lenye imani ya kweli na unyenyekevu kwa Mungu


Haya makanisa madogo ya kisuhikaji wala usiende kwani huko ndiyo kuna mafuska waliotukuka. Wengi wao wameacha uchangu na sasa wanajifanya wameokoka. Dini ni imani yako tu, amini na kumuomba Mungu kwa nafsi yako atakusaidia tu.
 
minimetokea Msikitini

kwahiyo unataka kuniambia Rutheran na Roman Catholic ni sawa na msikitini? You must be kidding; and l think the whole kwenda kanisani thing is a joke.
 
Nimeamua kuwa mkristo natafuta kanisa lakiroho nianzekwenda maeneo ya mabibo hosteli. Sio kanisa la mazingaumbwe noo kanisa la kuijenga roho yangu na uhusiano mzuri na Mungu mwenyezi
Umeijuwa kweli na kweli itakuweka huru, nenda kaabudu kanisa lolote lile, kama mafundisho yake si mazuri ndio uhame.
 
Kuna sehemu inaitwa Changamkeni hapo dar.kuna kanisa linaitwa New Testament Ministry.chini ya mch Oscar Mahenge nenda utasaidiwa
 
mbona mnamwelekeza kwenye makanisa ya mihemko tu. Latifa kaa mbali name hay yanayoitwa ya walokole
 
Last edited by a moderator:
Kanisa ka kweli liko ndani ya moyo wako.Msikilize Yesu anavyokuhitaji. Yohana.10:7-16. Ukisoma hapo na kulielewa hilo andiko, soma pia. Warumi. 10:9-13. Pia ujiweke kwenye maombi Mungu atakuonyesha kwa kwenda. Ila ushauri wa @By mshana jr ni wa kizingatia.
 
Kanisa ni mwili wa Kristo dada ila ni vema kuwa na ushirika.Unaweza kujumuika na wakristo wenzio pale kanisa la Deeper Life Bible church Ubungo,kituo cha maji kwa mbele kidogo upande wa kulia kama unatokea Kariakoo.Roho wa Bwana azidi kukujalia maarifa na hekima ya kumjua yeye.Nakutakia safari njema ya mafanikio katika maisha yako mapya ya Kikristo.Ubarikiwe sana.
 
Nakutakia kila la heri
Umechagua fungu jema

Nguzo yako kuu iwe kusoma biblia, mengine Mwneyezi Mungu atakuongoza.

Ni furaha kubwa mbinguni 'mmoja' tu anamkiri na kumfuata Bwana Yesu, nakutamani for real.
 
Haya makanisa madogo ya kisuhikaji wala usiende kwani huko ndiyo kuna mafuska waliotukuka. Wengi wao wameacha uchangu na sasa wanajifanya wameokoka. Dini ni imani yako tu, amini na kumuomba Mungu kwa nafsi yako atakusaidia tu.
ni kweli ila nataka kushirikiana na wenzangu kwenye ibada
 
Umeijuwa kweli na kweli itakuweka huru, nenda kaabudu kanisa lolote lile, kama mafundisho yake si mazuri ndio uhame.
Ni kweli ndio maana niko huru kutafuta mahali pakuabudu
 
Back
Top Bottom