Nataka kuanza kwenda kanisani

Nataka kuanza kwenda kanisani

Acha kuchezea watu wazima akili, kama vipi peleka hili swali lako Facebook. Hapa kila mtu ana imani yake na anafuata nyumba yake ya ibada na anaamini yupo sahihi kuwepo kwenye nyumba hiyo husika ya ibada, hivyo lazima akushauri uende kwake na mwisho wa siku utabaki kuzunguka zunguka tu. This is a platform of great thinkers stop playing with minds and faith of the people. Najua huna lolote wala huna shida na kujua kanisa nia yako ni kuona malumbano tu hapa.
wewe ni mtu mzima kweli?
 
Ooh nimetaja Efatha kwa vile hujalitaja hapo, kuhusu mazingaumbwe nina maana mimi nia yangu sio kwenda kanisani kwaajili ya kuonyeshwa miujiza miujiza wakati jinsi ya kuomba mwenyewe sijuhi maneno ya ushuhuda ndani ya neno la Mungu sina yani silijui neno, sasa hata nikifanyiwa hiyo miujiza siitakua kazi bure tuu sinitakua kilasiku mimi ni mtu wakutafuta miujiza, Nafikiri mwanzilishi wa miujiza alikua YESU KRISTO na aliifanya ili watu wamwamini sasa mtu kama mimi tayari nimeshamwamini YESU KRISTO kwanini nisifundishwe jinsi ya kuomba ili niwe naomba mwenyewekama ni hiyo miujiza itakuja tuu kwakuomba pekeyangu ?

nimekuelewa, makanisa niliyokuwa nimeyataja kwa ujumla wana kama utaratibu unaofanana, utapokelewa then itabidi ufanye mafundisho ya ubatizo ili ujue msingi wa imani yako na kuwa Kristu ni nani na uweze kukiri imani yako, mafundisho yamnaweza kuchukua si chini ya miezi sita alafu utafanya mafundisho mengine ya komnio na kipaimara ili kuzidi kuelewa zaidi na kupokea mapaji ya roho mtakatifu, kulingana na jinsi ratiba ya kanisa ilivyo, n:b Imani ya mtu pia inategemea zaidi na utayari na bidii yako katika kulisoma neno la Mungu, utafundishwa na pia wewe uwe na moyo wa kusoma Biblia na kuitafakari kadri Mungu atakavyokujalia. iyo ni kwa kifupi tu.
 
Basi kama ni hivyo jiunge na jumuiya ili muwe mnasali kila siku na kuomba ila haya makanisa ya kishikaji (Ya wazungu wa sembe) watakulostisha tu na kukufirisi kila kitu huku mitume wenu/wao wanakula raha na kuwacheka kuwa wamepata wajinga wengine.

Huyu aliyetukana makanisa ya kiroho yote hivi siku moja atarudi hapa kutuambia namna gani kakutana na Yesu na kujiunga nao. H
aijalishi imetumwa lini hii.
 
Nimeamua kuwa mkristo natafuta kanisa lakiroho nianzekwenda maeneo ya mabibo hosteli. Sio kanisa la mazingaumbwe noo kanisa la kuijenga roho yangu na uhusiano mzuri na Mungu mwenyezi

kama unatafta sebene, nenda river gospel center, kwa mch. Mwansasu, lkn kama unataka kuijua imani, kukua kiroho, na kuiandaa roho yako, fika Mwembechai sda, opposite kuna kituo cha mafuta cha Michelin, plot inayofuata kuna KANISA LA KRISTO-MWEMBECHAI.

hapo hakuna mazingaombwe, ni kusoma biblia, kuichambua na kuitafakari. na ili uive, hakikisha unashiriki angalau kipindi kimoja cha wiki, hasa cha bible knowledge, baada ya mwaka njoo utupe mrejesho
 
Maana halisi ya kanisa imo rohoni mwako, ukimkubali na kumkiri Yesu Kristo kwa roho na kwakweli kuwa Bwana na Mwokozi wako, kule kanisani ni mahali tu pakukutana na wana kanisa wengine
Tahadhari; Epuka makanisa yanayohubiri miujiza tu Siku zote
Epuka makanisa yenye viongozi wanaojiita mitume na manabii
Epuka makanisa yenye kusisitiza utoaji zaidi kuliko kuhubiri neno la Mungu
Unaweza kusali Anglikana, Katoliki, Lutheran na Pentekose lakini huko kwingine manabii na mitume wenye A.K.A nyiiingi kuwa makini nako, hasa kwakuwa umchanga kiroho

Umenena vema mtumishi.
 
Kanisa ni roho na akili yako,yale uyatendayo yampendeze bwana.Huko kanisani ni show off tu.
 
Karibuni wote wana jf kanisani leo fgbf(kwa kakobe) mwenge
 
siombi ruhusa wala nikwamba naomba kuelekezwa nisije nikakosea njia, makanisa yamekua mengi nayanapingana means imanizao nitofauti kuna ndiyo na siyo





0

We ndugu unamtafuta Mungu au kanisa, maana nasoma tu unavyojitetea na kujikweza na kudhani wewe ni special sana hivyo unataka kuwa pale unapodhani waumini ni watakatifu tayari. Anza kusali kwanza hapo nyumbani kwako. Mungu hajatupatia kazi ya kukutafutia kanisa bali kusali na kuwapokea wanaopenda kumfuata.
 
Hongera sana kwa kuchukua maamuzi sahihi ya kumfuata Yesu Kristo. Umejitengenezea njia sahihi ya kwenda Mbinguni siku zako hapa duniani zikiisha. Nakushauri utafute kanisa la KKKT lililo karibu nawe. Kamuone mchungaji wa kanisa hilo atakuongoza kwa hatua zaidi... Karibu sana nyumbani mwa BWANA...
 
KakaJambazi Ushindwe na ulegee Latifa umechagua jambo jema.Karibu hapa Kinondoni TAG REVIVAL church karibu na biafra kuna kanisa lenye kumtukuza na kumwinua Bwana Ibada kila jumapili 1.00-4.00 asubuhi na 4.00-7.00 mchana wengi wamemwona Bwana katika maisha yao.

Kumtukuza na kumwinua bwana!!! Hapa ndipo huwa nafikia nashindwa kuelewa dhamira yetu ikoje. Sema tu Kumwabudu bwana.
 
Last edited by a moderator:
Karibuni wote wana jf kanisani leo fgbf(kwa kakobe) mwenge

Nilienda hapo siku moja kusali..nikaishia getini simply nimevaa jeans..niliwaambia ni Mara ya kwanza kufika hapa ila bado wakanikazia kwamba nikavae sijui suruali ya kitambaa ndio nitaruhusiwa..
Naomba maelezo kunani kwa mwanaume kuvaa jeans na shati lake zuri tu then unamzuia kujumuika na wakristu wenzake?? Je suruali ya kitambaa ndio kitambulisho cha vazi la heshima na jeans ni vazi la kihuni???
Finally niliishia kuondoka na siku hiyo sikusali tena coz mda ulikuwa umeenda sana.
 
Back
Top Bottom