Natafuta Fundi Wa LED Tv

RRONDO

JF-Expert Member
Jan 3, 2010
51,719
107,770
Habari wana jamvi.

Natafuta fundi mzuri na anaejielewa wa LED tv yangu. Ina miaka miwili na ushee ghafla juzi imeanza kuonesha nusu screen mistari chenga chenga na nusu ingine inaonesha clear kabisa.

Anaemjua fundi mzuri, kwa hapa Dar hasa maeneo ya kuanzia kinondoni,mwenge,makumbusho,sinza,magomeni,msasani anijulishe. Sio mbaya hata wa maeneo mengine nikikosa itabidi nimfuate, tafadhali niwekee contacts zake.

875ad109_vbattach219511.jpeg
 
Hili jukwaa la teknolojia halina mafundi wa tv?
 
Vutw subira mafundi wengi wapo site, mimi ni fundi ila niko mbali, Toa specifications full za hio TV tutoe ushauri
 
kanunue nyingine tu. mafundi wa bongo mizengwe tu.
Asante kwa ushauri. Nilifikiria hilo ila nikaona sio vibaya nikijaribu.

Kwa kulijua hili ndio maana nikasema fundi anaejielewa ila kuna muungwana hilo limemkera mpaka anatoa mitusi.
 
Ya kwangu niliipeleka kwa fundi ina miezi nane huko na haijawahi kurudi. Since then vitu vyangu vikiharibika huwa navitengeneza mwenyewe.
Asante mkuu, kwa kulijua hilo nimeomba fundi anaejielewa ila kuna muungwana hilo limemkera hadi kunitukana.
 
Asante kwa ushauri. Nilifikiria hilo ila nikaona sio vibaya nikijaribu.

Kwa kulijua hili ndio maana nikasema fundi anaejielewa ila kuna muungwana hilo limemkera mpaka anatoa mitusi.


kwakua umekuja vizur wacha niishie hapa tu mkuu ila...
 
Kama unao uwezo cheki ebay, amazon, au alibaba kioo cha LED cha tv yako ununue mpelekee fundi akufungie maana hapo hakuna dawa na mafundi wengi ni waswahili...
 
Mwaka huu nimeamua niishi kwa amani bila kumkwaza mtu yeyote. Mungu akubariki mkuu.

nimekuelewa sana hapo kwenye "anayejielewa" maana wengi ukiwapelekea tv au radio wanaiba na kubadilisha baadhi ya vifaa ndani yake afu wanaweka fake.
 
mie ya kwangu imegonga mahala kwenye purukushani screen imeweka crack haionyeshi nimedata kwakweli. yaani hapa nawasha nakutana na mistari nimechoka mwili na akili

hivi naweza pata kioo nikabadilishiwa yaani
 
mie ya kwangu imegonga mahala kwenye purukushani screen imeweka crack haionyeshi nimedata kwakweli. yaani hapa nawasha nakutana na mistari nimechoka mwili na akili

hivi naweza pata kioo nikabadilishiwa yaani
Wanasema vioo vipo kariakoo, ila nimefikiria nimeona ninunue tu ingine kwanza halafu hii ndio nitaamua baadae niifanyie nini.

Experience yangu na mafundi wetu anakwambia tatizo ni A ukileta A kitu hakifanyi kazi anakwambia hapa tubadili na B.

Nilifikiri yangu ina loose connection somewhere ila mafundi wawili wamesema ni kioo hio imenishawishi ninunue ingine.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom