Natafuta bajaji ya 1.5m mpaka 2m isiwe trip garage

Natafuta bajaji ya 1.5m mpaka 2m isiwe trip garage

Kevzy

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2026
Posts
969
Reaction score
1,696
Habari
“Matatizo unayatafuta mwenyewe kaka” nilipompa wazo hili jamaa yangu kuwa natafuta bajaji ya bei hiyo.. majibu yake yalikuwa hayo

Mwenye connection ya minada ya serikali ya bajaji na pikipiki zilizokamatwa na makosa mbali mbali kama na madawa na wenye vyombo wakavitelekeza kituoni.. naomba anisaidie connection hiyo natanguliza shukran

Au mwenye bajaji ya bei hiyo ya 1.5m mpaka 2m anisaidie kijana mwenzake, mdogo wake ,mwanae

Sijali kuhusu body, mashine iwe nzuri inafanya kazi vizuri, hata wiki ndio niende garage, ukweli ni zipo bajaji nzuri kwa bei hiyo

Isiwe ya mkopo mtu akaniuzia kwa kunikomoa wenye bajaji yao waje kuichukua

Isiwe ya wizi, nitahaibika mjini hapa sina mtaji mwingine zaidi ya hii pesa niliyonayo

Mtu anaweza akawa amechoka na bajaji akaamua tu kuuza ila inaweza isiwe na tatzo lolote nitashukuru, sijali kuhusu kilometa iwe tu inafanya kazi vizuri na isiwe trip kwa fundi

Nawapenda wana jf
 
Kaka bajaj bei yake karibu 10m wewe unatafuta ya 1m unakuwa mkali masharti yote haya?
Mkuu inawezekana mtu kaitumia kwa hata miaka kumi na imempa faida na bado ipo vizuri ila akaamua kuiuza tu , Mkuu
 
Kama bajeti yako ni hiyohiyo, nakushauri achana na hilo wazo.

Kwa pesa hiyo utapata bajaji chokambaya utatakiwa kuwa na extra money kwajili ya maintanance ili ikae road.
 
Kama bajeti yako ni hiyohiyo, nakushauri achana na hilo wazo.

Kwa pesa hiyo utapata bajaji chokambaya utatakiwa kuwa na extra money kwajili ya maintanance ili ikae road.
Boss hivi ushawahi pata nafasi ukaenda kwenye minada ya serikali ya vyombo vilivyotelekezwa na wenye vyombo?
 
Back
Top Bottom