Natafta mganga wa kuagua wa ukweli.

Natafta mganga wa kuagua wa ukweli.

Monomer

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2023
Posts
680
Reaction score
1,260
Sikubali haiwezekani mtoto afikishe miaka mitatu anaongea vizuri,alikua anabwabwaja maneno chungu nzima gafla tu akaanza kua na kigugumizi Toka hapo Yani anateseka sana kwenye kuongea hadi utamuonea huruma.

Hua najiuliza ni nini kilitokea sijawahi pata jibu.Hivyo natafta mganga amuague pengine huezi jua ya walimwengu mi nahisi kabisa Kuna mtu alimfunga mdomo kwa manufaa yake mwenyewe.
 
Sikubali haiwezekani mtoto afikishe miaka mitatu anaongea vizuri,alikua anabwabwaja maneno chungu nzima gafla tu akaanza kua na kigugumizi Toka hapo Yani anateseka sana kwenye kuongea hadi utamuonea huruma.

Hua najiuliza ni nini kilitokea sijawahi pata jibu.Hivyo natafta mganga amuague pengine huezi jua ya walimwengu mi nahisi kabisa Kuna mtu alimfunga mdomo kwa manufaa yake mwenyewe.
Tatizo ni hili. Unachokitafuta haki-exist. Kwa kifupi ni kuwa hakuna mganga wa ukweli.
 
Sasa hapo sijui. Ila tambua kuwa ubongo unahusika Moja kwa moja katika masuala yahusuyo kuongea.
Alo we acha mtoto alikua anaongea vizuri bila tatizo lolote anapangilia maneno hadi basi gafla tu kama vile mtu amenyamanzishwa,mi mpaka Leo sijawahi kuamini kama ni tatizo la kawaida
 
Alo we acha mtoto alikua anaongea vizuri bila tatizo lolote anapangilia maneno hadi basi gafla tu kama vile mtu amenyamanzishwa,mi mpaka Leo sijawahi kuamini kama ni tatizo la kawaida
Pole sana. Kwa msaada mpeleke hospitalini, siyo Kwa waganga wa jadi.
 
Mkuu ebu elezea vizuri tatizo ni hicho kigugumizi tu au nini hasa?
Kama ni kigugumizi tu wala huhitaji kuhangaika.
 
Niliwahi kupatwa na hali hiyo nikiwa darasa la 5, ilidumu kama miezi kadhaa baadae ikapotea ila ninachokigugumizi kwa mbali.

Hadi leo sijui ilikuaje.
 
downloadfile.jpg
 
Mkuu ebu elezea vizuri tatizo ni hicho kigugumizi tu au nini hasa?
Kama ni kigugumizi tu wala huhitaji kuhangaika.
Kinachonifanya nihangaike ni kua mwanzo alikua anaongea vizuri lakini alipofikisha miaka 3 tu kikamuanza asa kadri anavokua ndo chaongezeka badala kupungua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom