Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Iwapendeze wakuu;
Akiwa katika harakati za kumjibu Wassira juu ya swala lake la kutochaguliwa kwa kuwa hana mke kijana huyu (Joshua Nassari) mbele ya Kiongozi wake wa Kitaifa alitamka kuwa akiwa Mbunge basi atamuoa Mhe. Halima Mdee ili Jimbo lake la Arumeru Mashariki linufaike mara dufu kwa kuwa na Wabunge wawili.
Nimeshindwa kujua kama ni akili zake ama ni za jirani manake nimejiuliza; Je ni kweli kwamba hajui ama hafahamu kuwa hata akijaliwa hilo ambalo yeye amesema anamwomba Mungu ili litimie haliwezi kamwe kubadilisha nafasi aliyo nayo Halima katika kutekeleza wajibu wake kwa watu wa Kawe na vitongoji vyake?? Lakini hata kama ni ndoto hivi kumbe anachotaka yeye si tu kumuoa Halima kama mke bali anataka kufaidi ama kupata faida kutoka kwa Halima kwa kupitia nafasi aliyo nayo kama Mbunge!
Vijana kwa kweli kazi tunayo ugonjwa ni ule ule wa kujibizana na kukosa kipi cha kuzungumza kwa wakati gani???
Akiwa katika harakati za kumjibu Wassira juu ya swala lake la kutochaguliwa kwa kuwa hana mke kijana huyu (Joshua Nassari) mbele ya Kiongozi wake wa Kitaifa alitamka kuwa akiwa Mbunge basi atamuoa Mhe. Halima Mdee ili Jimbo lake la Arumeru Mashariki linufaike mara dufu kwa kuwa na Wabunge wawili.
Nimeshindwa kujua kama ni akili zake ama ni za jirani manake nimejiuliza; Je ni kweli kwamba hajui ama hafahamu kuwa hata akijaliwa hilo ambalo yeye amesema anamwomba Mungu ili litimie haliwezi kamwe kubadilisha nafasi aliyo nayo Halima katika kutekeleza wajibu wake kwa watu wa Kawe na vitongoji vyake?? Lakini hata kama ni ndoto hivi kumbe anachotaka yeye si tu kumuoa Halima kama mke bali anataka kufaidi ama kupata faida kutoka kwa Halima kwa kupitia nafasi aliyo nayo kama Mbunge!
Vijana kwa kweli kazi tunayo ugonjwa ni ule ule wa kujibizana na kukosa kipi cha kuzungumza kwa wakati gani???