Nikianza na mfano wako wa SA Watu weusi wamekuwa majority siku zote. Makuburu ndio walikuwa minority na Utawala wao ulijulikana kama "White-minority rule"
Tukija hapa kwetu bado ni mjadala kusema wanawake ni minority group kama vile walemavu katika uwakilishi wa ubunge na udiwani.Wanawake Tanzania wanaweza kugombea katika vyama vyao kupata nafasi za uwakilishi bila ubaguzi, hakuna sheria, mazingira au mifumo katika vyama vyetu vya siasa zinazozuia wanawake kuwa wagombea ndio maana unaona wako wengi katika nafasi hizo.
Pia tufahamu kwamba ubunge ni kazi ya uwakilishi wa wananchi wa eneo fulani.Watu wa jimbo wanakuchagua ukawe sauti yao bungeni. Kama wananchi wa jinsia zote kutoka majimbo yote ya nchi wameamua kuchagua wanaume kuwa wabunge kupitia uchaguzi huru na wa haki "well and good" wameona hao ndio wanafaa kuwa wawakilishi wao. Lazima tuheshimu hivyo
Hatuhitaji kuwa na wabunge wasiowakilisha maeneo kama hawa wa viti maalum na wakuteuliwa na rais kwa kigezo chochote.