Nashauri tupunguze idadi ya wabunge

Tuondoe vitu maalum na Rais apewe nafasi 10 za Uwaziri zisizotokana na Ubunge au Mawaziri isiwe lazima wawe wabunge kama ambavyo Spika wa bunge sio lazima awe mbunge.
Kwa maoni yangu viti maalum waondolewe lakini wa kuteuliwa wabaki.
Wakuteuliwa wabaki kwa sababu Raisi anaweza asipate anayemhitaji kutoka kwa wabunge waliochaguliwa hivyo anaweza kuteua watu anaowaona watamsaidia zaidi kutimiza majukumu yake.
Raisi anaweza kuwa na mtu ambaye amefanya nae kazi kwa kipindi fulani akapenda utendaje kazi wake kama hakuchaguliwa kuwa mbunge ni rahisi kumteua kuja kusaidia.
Nionavyo mimi.
 
Bunge letu ni kubwa sana kwa uchumi tulio nao na ukubwa wa eneo tulilo nalo.

Kwa sasa tuna wabunge takribani 400. Na tuna wilaya 169.

Kwanini tusiwe na wabunge wanaoendana na wilaya zetu kwa kupunguza idadi ya majimbo.

Uwepo wa wabunge wengi kwanza unapunguza muda wa kujadili mambo kwa kina kwa kuharakisha kila mtu apate muda wa kuongea.

Pia kunatoa mwanya wa wabunge wavivu kujificha kwenye umati, wanatoroka wanakula posho hawachangii chochote.

Idadi hii kubwa ya bunge ni mzigo kwa taifa ni fedha kiasi gani tutaokoa ili tuzielekeze katika mambo mengine ya msingi?

Je, kiwango cha matumizi yao kinaakisi faida wanayoleta katika taifa?

Mambo wanayopitisha na kujadili yana faida kwa taifa kiasi cha kutuingiza kwenye hii hasara kubwa ya kuwalipa?
Wazo Nzuri sana, wabunge wachaguliwe kwa wilaya sio majimbo
 
Wabunge wetu bahati mbaya wamekuwa ni wachumia matumbo, na ukianza kuwasemea maslahi yao, utashangaa utajua hakuna upinzani, wataungana na lao litakuwa moja.

Watakuambia wana kazi nyingi, kazi za kupigana vijembe!

Kenyatta alithubutu, akafyekelea mbali mishahara iliyokuwa mzigo alipoingia ofisini.

Everyday is Saturday............................... :cool:
Wewe unapenda upinzani?
Au ni kuwachezea shere tu?
 
Minority ni suala la Idadi ndogo kwa kuanzia mambo ya degree of vulnerability and power yanafuata baadaye.
Nadhani bado unapata shida kupembua, kuchamba na kuchambua hoja tunayozungumza. Mimi nimezungumzia A Minority Group siyo Minority: Semantically and Technically haya maneno hayana maana sawa. Wanazuoni waliounda na kutafasiri hilo neno kama Prof Lous Wirth hawakuzungumzia idadi peke yake bali Power and Vulnerability.

Huko tunapoamini demokrasia ndipo ilianzia, ambapo demokrasia ndio inapaita nyumbani kwake hakuna kitu kama mbunge wa viti maalum au wa kuteuliwa.Huwezi kuingia bungeni pasipo kuchaguliwa na wananchi wa eneo fulani.
Pia, nadhani huna taarifa za kutosha kuhusu demokrasia, hasahasa jinsi ilivyoanza kule Athene ya Ugiriki ya kale ndiyo maana unahisi naleta maneno yasiyo muhimu (Fallacies) kwenye hoja. Ungefanya tafiti kidogo basi naamini tungekuwa kwenye ukurasa mmoja.

Haya sasa angalia hoja yako kuhusu demokrasia ilivyokuwa nyepesi: Plato kwenye kitabu chake cha The Republic anazungumzia mfumo wa demokrasia ambao ulianzia Athene ya Ugiriki. Anasema hakukuwa na Representative Democracy kama wewe unavyotanabaisha hapa, bali kulikuwa na Direct Democracy.

Watu wote wa mji waliitwa kwenye mkutano wa pamoja ambao uliamua mambo yao mbalimbali. Mkutano huo ulikuwa unafanya kazi kama bunge na mahakama, jambo nyeti halikufanyika bila wananchi wote kuridhia. Sasa nadhani unavyozungumzia kuhusu demokrasia nadhani hili uliweke kichwani.

Wabunge wote kuchaguliwa kupitia maeneo ya kijimbo haiwezi kuzuia watu kujadili mambo ya kitaifa juu ya yale yanayohusu majimbo yao. Hiyo issue ya mandate ni dilemma isiyo na mashiko, ni straw man fallacy.
Unafahamu maana ya The Doctrine of Mandate ???
 
Bunge letu ni kubwa sana kwa uchumi tulio nao na ukubwa wa eneo tulilo nalo.

Kwa sasa tuna wabunge takribani 400. Na tuna wilaya 169.

Kwanini tusiwe na wabunge wanaoendana na wilaya zetu kwa kupunguza idadi ya majimbo.

Uwepo wa wabunge wengi kwanza unapunguza muda wa kujadili mambo kwa kina kwa kuharakisha kila mtu apate muda wa kuongea.

Pia kunatoa mwanya wa wabunge wavivu kujificha kwenye umati, wanatoroka wanakula posho hawachangii chochote.

Idadi hii kubwa ya bunge ni mzigo kwa taifa ni fedha kiasi gani tutaokoa ili tuzielekeze katika mambo mengine ya msingi?

Je, kiwango cha matumizi yao kinaakisi faida wanayoleta katika taifa?

Mambo wanayopitisha na kujadili yana faida kwa taifa kiasi cha kutuingiza kwenye hii hasara kubwa ya kuwalipa?
Wabunge wanaopaswa kupunguzwa ni wa Zanzibar

Kwa idadi ya watu Zanzibar ina watu wa chache ukilinganisha mkoa mmoja tu wa Dar es salaam lakini ina wabunge zaidi ya 60

Kwa ukubwa wa kieneo Zanzibar ni ndogo sana ukilinganisha na mkoa wowote ule lakini ina wabunge zaidi ya 60
 
Back
Top Bottom