Nashauri tupunguze idadi ya wabunge

singojr

JF-Expert Member
Oct 28, 2014
5,308
6,884
Bunge letu ni kubwa sana kwa uchumi tulio nao na ukubwa wa eneo tulilo nalo.

Kwa sasa tuna wabunge takribani 400. Na tuna wilaya 169.

Kwanini tusiwe na wabunge wanaoendana na wilaya zetu kwa kupunguza idadi ya majimbo.

Uwepo wa wabunge wengi kwanza unapunguza muda wa kujadili mambo kwa kina kwa kuharakisha kila mtu apate muda wa kuongea.

Pia kunatoa mwanya wa wabunge wavivu kujificha kwenye umati, wanatoroka wanakula posho hawachangii chochote.

Idadi hii kubwa ya bunge ni mzigo kwa taifa ni fedha kiasi gani tutaokoa ili tuzielekeze katika mambo mengine ya msingi?

Je, kiwango cha matumizi yao kinaakisi faida wanayoleta katika taifa?

Mambo wanayopitisha na kujadili yana faida kwa taifa kiasi cha kutuingiza kwenye hii hasara kubwa ya kuwalipa?
 
Ukiwaza na gharama za magari wanayopewa unafikiria hivi wanatuonaje?
Kwakweli vinchi vya Kiafrika kwa kujitutumua kuna baadhi ya Nchi zilizoendelea Wabunge wanatumia Magari ya kawaida

Hawa wa kwetu gari V8 inabugia mafuta kama haina akili halafu hapo mlipaji ni Mwananchi anayenyonywa kila uchwao

Gari kama Landrover Station wagon ingewafaa hawa Wabunge
 
Wabunge wetu bahati mbaya wamekuwa ni wachumia matumbo, na ukianza kuwasemea maslahi yao, utashangaa utajua hakuna upinzani, wataungana na lao litakuwa moja.

Watakuambia wana kazi nyingi, kazi za kupigana vijembe!

Kenyatta alithubutu, akafyekelea mbali mishahara iliyokuwa mzigo alipoingia ofisini.

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Wengine wamekosa vya kujadili wameanza kujadili nguvu za kiume ni aina ya Bunge kubwa linaloteketeza pesa za walipa kodi, turejee kama zamani bunge la Nyerere halikuwa na umati wa wabunge kama sasa
 
Sasa wanahangaika na nguvu za kiume huku Msukuma na Lusinde kibajaji wao wametumwa na Ndungai kuwatukana wapinzani, hawapo serious na bajeti
Wana lao jambo, hiyo ni distraction tu, kutakuwa na kitu kitapita bila ya sisi kujua, kitu cha kuumiza wananchi, wanatupoteza maboya.

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Wabunge wetu bahati mbaya wamekuwa ni wachumia matumbo, na ukianza kuwasemea maslahi yao, utashangaa utajua hakuna upinzani, wataungana na lao litakuwa moja.
Watakuambia wana kazi nyingi, kazi za kupigana vijembe!
Kenyatta alithubutu, akafyekelea mbali mishahara iliyokuwa mzigo alipoingia ofisini.

Everyday is Saturday............................... :cool:

Na sisi tunashindwa nini kujaribu hili? Ni nani anayepanga mishahara ya wabunge?
 
Back
Top Bottom