Nashauri tupunguze idadi ya wabunge

Nashauri tupunguze idadi ya wabunge

Sasa hivi hakuna upinzani mjengoni, huwa ndio wakati mzuri wa kuwabana.
Wabunge wetu bahati mbaya wamekuwa ni wachumia matumbo, na ukianza kuwasemea maslahi yao, utashangaa utajua hakuna upinzani, wataungana na lao litakuwa moja.
Watakuambia wana kazi nyingi, kazi za kupigana vijembe!
Kenyatta alithubutu, akafyekelea mbali mishahara iliyokuwa mzigo alipoingia ofisini.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Tunaweza kuondoa wabunge wa vitu maalum. Hakuna uhitaji huo tena.
Nchi ya watu 60 million, ina idadi kubwa ya wabunge sawa na India nchi yenye watu 1 Billion,
Mzee Warioba alipendekeza wabunge wasizidi 70, ambao wamesoma (Gender izingatiwe)
Ile rasimu ingepita tungepunguza kadhia ya kuwa na vichaa wengi sana kule bungeni.
 
Bunge letu ni kubwa sana kwa uchumi tulio nao na ukubwa wa eneo tulilo nalo.
Kwa sasa tuna wabunge takribani 400. Na tuna wilaya 169.
Kwanini tusiwe na wabunge wanaoendana na wilaya zetu kwa kupunguza idadi ya majimbo.
Uwepo wa wabunge wengi kwanza unapunguza muda wa kujadili mambo kwa kina kwa kuharakisha kila mtu apate muda wa kuongea.
Pia kunatoa mwanya wa wabunge wavivu kujificha kwenye umati, wanatoroka wanakula posho hawachangii chochote.
Idadi hii kubwa ya bunge ni mzigo kwa taifa ni fedha kiasi gani tutaokoa ili tuzielekeze katika mambo mengine ya msingi?
Je kiwango cha matumizi yao kinaakisi faida wanayoleta katika taifa?
Mambo wanayopitisha na kujadili yana faida kwa taifa kiasi cha kutuingiza kwenye hii hasara kubwa ya kuwalipa?

Tungependekeza wafute kabisa maana sioni kazi wanayofanya Subwoofer anakua kama rabastampu ya mapendekezo yote ya serikali.
 
Sasa hivi hakuna upinzani mjengoni, huwa ndio wakati mzuri wa kuwabana.
Ile team covid ipo kule mkuu!
Wanatuchezea akili, siyo wanachama wa chama cha siasa ila ni wabunge!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Bunge letu ni kubwa sana kwa uchumi tulio nao na ukubwa wa eneo tulilo nalo.
Kwa sasa tuna wabunge takribani 400. Na tuna wilaya 169.
Kwanini tusiwe na wabunge wanaoendana na wilaya zetu kwa kupunguza idadi ya majimbo.
Uwepo wa wabunge wengi kwanza unapunguza muda wa kujadili mambo kwa kina kwa kuharakisha kila mtu apate muda wa kuongea.
Pia kunatoa mwanya wa wabunge wavivu kujificha kwenye umati, wanatoroka wanakula posho hawachangii chochote.
Idadi hii kubwa ya bunge ni mzigo kwa taifa ni fedha kiasi gani tutaokoa ili tuzielekeze katika mambo mengine ya msingi?
Je kiwango cha matumizi yao kinaakisi faida wanayoleta katika taifa?
Mambo wanayopitisha na kujadili yana faida kwa taifa kiasi cha kutuingiza kwenye hii hasara kubwa ya kuwalipa?
Na mishahara ipunguzwe,walipwe laki 5 tu..hapa wazalendo tutawapata wa kuwatetea wananchi la sivyo wananchi wataona ubunge ni fursa.Mkuu naww UNADEMKA?😊😊
 
Huu Uzi nimeupenda.Yaani ingewezekana Uchaguzi wa 2025,hii Kitu ianze rasmi.Kila Wilaya kuwepo na mbunge mmoja TU wa kuchaguliwa bila kujali ukubwa wa Wilaya husika.Mbona KILA Wilaya tuna MKUU mmoja TU wa Wilaya(bila kujali ukubwa wa Wilaya) na Mambo yanaenda ? Hoja yako Nimeipenda mkuu.Ila kwa kuongezea hoja yako,Hata wabunge wa viti Maalum kwa KILA mkoa pia wangeondolewa,wabaki wabunge wa viti Maalum kwa baadhi TU ya makundi muhimu ya akina mama.Viti Maalum kwa KILA mkoa Ni Nafasi zimewekwa kupeana ulaji TU.
 
Viti Maalum ni upigaji mtupu wa pesa za walipa kodi
Huu Uzi nimeupenda.Yaani ingewezekana Uchaguzi wa 2025,hii Kitu ianze rasmi.Kila Wilaya kuwepo na mbunge mmoja TU wa kuchaguliwa bila kujali ukubwa wa Wilaya husika.Mbona KILA Wilaya tuna MKUU mmoja TU wa Wilaya(bila kujali ukubwa wa Wilaya) na Mambo yanaenda ? Hoja yako Nimeipenda mkuu.Ila kwa kuongezea hoja yako,Hata wabunge wa viti Maalum kwa KILA mkoa pia wangeondolewa,wabaki wabunge wa viti Maalum kwa baadhi TU ya makundi muhimu ya akina mama.Viti Maalum kwa KILA mkoa Ni Nafasi zimewekwa kupeana ulaji TU.
 
Nami naunga mkono. Hivi Nani huwa anatengeneza majimbo, je ana uwezo wa kuvunja na kukuunganisha Jimbo?
Isije ikawa mpaka suala license kuamuliwa bungeni na wabunge wenyewe, hapo mjadala utafeli
 
Serikali ndio inaamua idadi ya majimbo
Nami naunga mkono. Hivi Nani huwa anatengeneza majimbo, je ana uwezo wa kuvunja na kukuunganisha Jimbo?
Isije ikawa mpaka suala license kuamuliwa bungeni na wabunge wenyewe, hapo mjadala utafeli
 
Hata watumishi wa umma nao wapunguzwe wabaki wachache watakaoboreshewa maslahi yao na kupewa vitendea kazi ili utendaji wao uwe na tija
 
Wabunge wa Zanzibar wangepunguzwa.ila.idadinya kura zao zingehesabiwa kulingana.na uwiano wa sasa mfano kama sasa hivi idadi yao ni 113! Sawa na asilimia 40 wanaweza kupunguzwa hadi wabunge 40 lakini kwenye upigaji kura kila kura moja ikahesabika Ni kura 2.825 huku bara nqo wqkipunguza wabunge kwenye majimbo yenye idadi ndogo ya wqtu pamoja nq kupunguza viti maalumu
 
Wabunge wa Zanzibar wangepunguzwa.ila.idadinya kura zao zingehesabiwa kulingana.na uwiano wa sasa mfano kama sasa hivi idadi yao ni 113! Sawa na asilimia 40 wanaweza kupunguzwa hadi wabunge 40 lakini kwenye upigaji kura kila kura moja ikahesabika Ni kura 2.825 huku bara nqo wqkipunguza wabunge kwenye majimbo yenye idadi ndogo ya wqtu pamoja nq kupunguza viti maalumu
Pia Bunge la Zanzibar sasa iwe lazima wabunge tokea Tanganyika waingie kule, siyo wao kuwa na Bunge lao binafsi kisha wao wanaingia Bungeni Dodoma pasipo wa wabunge wa Tanganyika kwenda Bungeni kwao, cha Zanzibar ni cha wazanzibar tu na cha Tanganyika ni cha wote hii dhana ifutwe sasa, wabunge wawe huru kuingia Bungeni kote kote, Zanzibar kuendelea kula posho Dodoma ni wizi lazima wabunge wa Tanganyika wale posho Zanzibar iwe ngoma sawa.
 
Hata watumishi wa umma nao wapunguzwe wabaki wachache watakaoboreshewa maslahi yao na kupewa vitendea kazi ili utendaji wao uwe na tija
Watumishi wakipunguzwa itakuwa tabu mitaani familia zitataabika mno, wa kupunguzwa ni wabunge pekee ndiyo wameonekana mzigo kwa kodi za watanzania
 
Back
Top Bottom