Nape: Wafanyabiashara wa fedha za kigeni walioporwa fedha zao wamefutwa machozi

Pac the Don

JF-Expert Member
Feb 17, 2021
6,177
7,699
Kwa lengo gani? Je kwanini wahusika warudishiwe haki yao? Ilikuwa uporaji?

===
Nape akiwa Clouds FM amesema

"Rais Samia Suluhu Hassan katika miaka hii 2 ya uongozi amefanya kazi ya kuwafuta watu machozi na amefanya kazi ya kurudisha furaha na tabasamu kwenye maisha ya watu. "Wale wanasiasa wenzangu waliokimbia nchi machozi yao yamefutwa na na furaha imerudishwa kwao wamerudi nyumbani"

"Wale Wenye mahotel ambao hotel zao zilifungwa kwa sababu ya COVID 19 machozi yao yamefutwa kupitia royal tour. Watalii wamejaa. Wale waliokuwa na magari ya kusafirisha watalii waliokuwa wamepaki Arusha na kwingineko wamefutwa machozi na Rais Samia Suluhu Hassan".

"Wale wafanyabiashara waliokuwa wakiuza fedha za kigeni ambao maduka yao yalifungwa na fedha zao zikachukuliwa machozi yao yamefutwa kwa kurudishiwa fedha zao na kuruhusiwa kufungua maduka tena"

"Kubwa ni kwamba tumefurahishwa na umeendelea kutugusa sana Waziri Nape.


Asante kwa kufika na Tarehe 25 tutakuwa hapa kwenye Kilele cha Malkia wa Nguvu kwa ajili ya kuwapa tuzo akina dada na mama zetu waliosababisha na kufanya vyema katika nyanja mbalimbali".

Nape.jpg
 
Waziri Nape Nnauye akiwa katika kongamano la miaka 2 ya Rais Samia, amesema Rais amewafuta machozi watu wengi walioonewa na utawala uliopita.

Kama vile wale wafanyabishara wa fedha za kigeni ambao maduka yao yalivamiwa ghafla na wanajeshi wenye mitutu na kuchota fedha zote kisha kufunga maduka hayo.

Rais Samia amewafidia na kuruhusu maduka yao kufunguliwa tena.


Screenshot_20230320-090508.png

===
"Rais Samia Suluhu Hassan katika miaka hii 2 ya uongozi amefanya kazi ya kuwafuta watu machozi na amefanya kazi ya kurudisha furaha na tabasamu kwenye maisha ya watu. "Wale wanasiasa wenzangu waliokimbia nchi machozi yao yamefutwa na na furaha imerudishwa kwao wamerudi nyumbani"

"Wale Wenye mahotel ambao hotel zao zilifungwa kwa sababu ya COVID 19 machozi yao yamefutwa kupitia royal tour. Watalii wamejaa. Wale waliokuwa na magari ya kusafirisha watalii waliokuwa wamepaki Arusha na kwingineko wamefutwa machozi na Rais Samia Suluhu Hassan".

"Wale wafanyabiashara waliokuwa wakiuza fedha za kigeni ambao maduka yao yalifungwa na fedha zao zikachukuliwa machozi yao yamefutwa kwa kurudishiwa fedha zao na kuruhusiwa kufungua maduka tena"

"Kubwa ni kwamba tumefurahishwa na umeendelea kutugusa sana Waziri Nape.

Asante kwa kufika na Tarehe 25 tutakuwa hapa kwenye Kilele cha Malkia wa Nguvu kwa ajili ya kuwapa tuzo akina dada na mama zetu waliosababisha na kufanya vyema katika nyanja mbalimbali".
 
Kuna mtu niliwahi kukaa nae Arusha alikua na bureau, alinipa mkasa mzima

Aisee Hio siku walipofungua bureau zilikuja defender na 'vyuma' yaani walichukua pesa zote hata coin haikubaki, na katika askari waliotelekeza amri hii na kupeleka pesa bot wengi walitajirika maana kama unavyotujua wabongo huwezi kunipa maburungutu ya pesa ambayo hayana hesabu nikayafikisha yote

Ila Hawa watu nao walikua wanaibia taifa sana pesa na wengi walikua wanatakatisha sana pesa chafu, kiufupi walijisahau sana jiwe akaamua kuwapiga ambush kiroho mbaya,

Hii nchi watu hawaelewi tu, hakuna watu hawapendi kulipa Kodi kama matajiri, ukishaona mtu ana bilion kadhaa bank asimilia 90 ya hao watu ni janja janja nyingi tu na kuibia serikali mapato

Swala la kuwanyoosha Hawa matajiri waiba Kodi sijawahi kumpinga magufuli japokua nilikua simkubali, ila la kudeal na Hawa wezi wa Kodi hapo Mzee nilimkubali
 
Back
Top Bottom