NAPE: Nalipenda sana gwanda la CHADEMA

NAPE: Nalipenda sana gwanda la CHADEMA

Si amini kama NAPE akija CDM atakua na msaada kwani damu yake 85% ni rangi ya kijani
 
Kama una mapenzi na cdm ingia mzima mzima usiogope mkuu nape.
 
Kaka Nape nafac bado unayo ya kujisahihisha,waweza kuhamia cdm maana huko uliko mambo ya kujivua gamba yatakuponza
 
Wakuu, kila anpoongea bwana Nape muwe mnamwangilia usoni vizuri, huwa anaongea yale asiyo yaamini kabisa, huyu kijana yupo ccm kwasababu ya nja tu, moyo wake upo Mageuzi kabisa, kinacho msumbua ni nja na tamaa ya madaraka, akiongoka kwenye hayo 2 basi anakuwa kijana mzuri tu tena mwenye great future kwa hapa Bongo.

Nasikia hata uchaguzi mkuu uliopita (mara baada ya kushindwa kukisajiri chama chao cha CCJ) alikwenda CDM kuomba kugombea Ubungo, muziki wa John Mnyika ukawa mkubwa kwake, so please kwa wale mnao jua Body language, mwangaliieni vizuri huyu bwana mdogo kila anapoongea, utaona tu mwili wake hasa macho yake, anacho kisema hakitoki kabisa moyoni mwake, yaani hata yeye anajua ccm mahali ilipofika hairekebishiki zaidi ya kufa.
 
hata hivyo anasaidia sana cdm alikuja mwanza mwaka jana pale magomeni akadai wana mwanza atawashikisha ukuta hiyo nayo imesaidia sana cdm kuchukua kata ya kirumba karibu tena mwanza uje ujenge cdm
 
Na January anamuogopa baba yake but anaitaka sana Chadema
Ni huyuhuyu January aliyechangiwa na wezi wa madini yetu ili apite ubunge bila kupingwa kwa lengo la kupewa uwaziri wa madini ili awawezeshe hao wezi wa madini yetu kutuibia kwa kasi zaidi. Hii ndiyo sababu ya chuki ya January kwa Ngeleja. Kama na yeye anaitaka CDM, soon CDM itakuwa kichaka cha wezi.
 
Jana nilivyokuwa namuona akizungumza alikuwa mpole sana na nafikili roho ilikuwa ikimuuma sana hasa akikumbuka yale maneno yake "ARUMERU TUTASHINDA KWA KISHINDO"
 
Gwanda lake feki, sie chadema huwa twatumia rangi hiyo kwenye misiba!

Tayari Nape anazika ccemu,kavaa magwanda za makamanda wanazotumia kwenye mazishi,peopleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeezzzzzzz
 
Tusimsakame Nape kwa kuvaa gwanda, tuwakosoe kwa matendo yao potofu. Mwacheni akitangaze chama
 
i dont see any problem with Nape, the guy is doing his best, sema tu ndiyo hivyo yupo katika dimbwi la waovu, linalomfanya na yeye aonekane muovu.
 
Hamia Chadema, wewe na jamaa zako
 
Back
Top Bottom