OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
Ndo haya magamba tunahangaika nayo. Likitoka hili gamba kuu haya mengine hayatatusumbua
Kwani siku 90 hazijaisha?
Ndo haya magamba tunahangaika nayo. Likitoka hili gamba kuu haya mengine hayatatusumbua
Na Mungu ameshamkataa ndo maana anampa gonjwa la ajabu kiasi ambacho hata peni anasindwa kushikaWell said Mkuu.... Lowassa anaitajika kwa sana na kwa sasa hakuna wa kumzuia zaidi ya Mungu
Tunaendelea kuwachunguzaKwani siku 90 hazijaisha?
Hongereni CCM kwa kummaliza huyo mwizi
Tena sana Mkuu. Lowasa amejimaliza mwenyeweLowasa amekiuka taratibu nyingi sana za chama kwahiyo anatakiwa akutane na adhabu kali sana.
Hali isiyo ya kawaida amefikia kuudanganya summa kwamba yeye yuko mzima wa afya kwa kumuarika mpiga ampige picha akifanya mazoezi kitu ambacho kiliandaliwa huku wananchi wakijua kabisa kuwa hayuko sawa kiafya....hahahahaaa jamaa kapania kiukweli
Hahahaa naamini ww itakuaa miongoni mwa wale wanaojipanga foleni mkisubiri mfikiriwehivi mnakumbuka jk wakati anagombea ccm nape alisema jk ana ukimwi?na jk mpaka leo anadunda,ndicho hicho hicho kinachotokea kwa lowassa,jiandaeni kisaikolojia lowaasa ndiye rais ajaye
Unapotaja jina la lowasa taja pamoja na jina la shetani.Na Mungu ameshamkataa ndo maana anampa gonjwa la ajabu kiasi ambacho hata peni anasindwa kushika
napekapewa kazi na membe ya kumchafuwa lowasa kwa makubaqliano kwamba nape ataachiwa jimbo na membe,ridhiwani mama yake naye wanampotosha baba jk,membe amekuwa akimtumia riz kupeleka majungu kwa baba yake
Habari wapendwa.
Akihojiwa kupitia kituo cha Radio cha Clouds FM kwenye kipindi cha Power Breakfast juu ya makundi mbalimbali ya kijamii kumtaka Lowasa kutangaza nia yamkugombea nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2015, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Nape Moses Nnauye amesema kuwa kimsingi Lowasa ameonesha na ametangaza nia ya kugombea nafasi hiyo kwa muda mrefu na ndo maana chama kilimwadhibu kwa kuanza kampeni kabla ya wakati wake. Anasema kuwa kinachofanyika kwa sasa ni usanii na ulaghai wa kisiasa wa mwanasiasa huyo ambaye anausaka urais kwa udi na uvumba na kwamba kinachofanyika kwa sasa ni muendelezo wa kampeni za mapema zinazovunja kanuni na misingi ya chama.
Anasema kuwa si kweli kuwa makundi hayo ndiyo yanayomtaka Liwasa agombee bali watu hao wanaandaliwa na gharama zote zinalipwa na Lowasa ikiwa ni pamoja na nauli, malazi, chakula pamoja na fedha zinazotolewa kwa lengo la kugharamia uchukuaji wa fomu. Nape anaongeza kwa kusema kuwa wanazo taarifa kuwa makundi mbalimbali yanaendelea kuandaliwa ambayo yataenda Dodoma siku si nyingi. Anasema kuwa wakiwa Kilimanjaro, wamepata taarifa za baadhi ya watu walioombwa na Team Lowasa kwenda Dodoma. Ameyataka makundi hayo kuwa ni pamoja na Walemavu na Wafanya Biashara ndogo ndogo maarufu kama Wamachinga.
Akitoa ufafanuzi zaidi anasema kuwa nyumbani kwa Lowasa yamewekwa mahema na viti vya kutosha muda mrefu hata kabla ya kundi la kwanza kwenda. Anasema kuwa kama kweli wageni hao hawakutokana na jitihada zake Lowasa, maandalizi hayo ya nini? Kwa nini waitwe waandishi wa habari na pia maandalizi ya chakula cha wageni hao kufanyika hata kabla ya ujio wa wageni hao? Anahoji Nape Nnauye.
Kwa msingi huo, Nape anasema kuwa hatua ambayo amefikia Lowasa haivumiliki na kwamba mwanasiasa huyo amejiondoa mwenyewe kwenye kinyang'anyiro cha urais kwa Tiketi ya CCM labda kama jitihada zake zinalenga kugombea nafasi hiyo kupitia chama kingine ambacho Nape hakukibainisha.
My Take: Naamini kuwa Nape hakukurupuka kusema aliyosema na bila shaka amepata baraka za viongozi wake akiwemo Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana ambaye yupo naye sambamba kwenye ziara zake pamoja na Mwenyekiti, Jakaya Kikwete. Lowasa ujumbe ndio huo. Harakati zako ni sawa na mtu anayetwanga maji huku akitaraji kupata unga. Nakuhurumia sana
Nape anamuandama mtu mmoja ...Kiasi kwamba kila mtu anaona...,Kama Juzi ...Mbeya ...wanafunzi wamekutana kumtaka Mwandosya ( baba yake wa Kweli ) ..na Arusha wamekutana Huko kumtaka Profesa Muhongo ....
Inapokua imebaki miezi Sita tu kufanya uchaguzi kutaka Kubana tusimjue mgombea Ndio kuleteana WAGOMBEA wenye mambo mengi ya kificho ...infact ingetakiwa mgombea wa chama ajulikane mwaka mmoja kabla ..ili kuweza kutibu makundi kuelekea uchaguzi ...ingekuwa tunaye mgombea urais wa ccm ..toka mwaka Jana October ....hata yeye anapata wasaaa wa kuchangia kwenye Ilani ..Kama ana ya kwake na watu wanapata muda kumjua ..vema .
...hata wale waliokua washindani wanaoata muda wa KUSHUSHA hasira Za kushindwa ...na kurudisha uhusiano mwema na mgombea ...lakini hili la kutupa mgombea miezi mitatu kabla ..madhara yake ni makubwa especially uchaguzi highly contested Kama huu
LAKINI PIA TUJIULIZE MWENYEKITI WA CCM ALIPOTOA AGIZO PALE SONGEA KUWA KAMA KUNA WATU WANAMJUA MGOMBEA NA WANAONA ANAFAA BASI WAMFUATE WAMSHAWISHI...ALITEGEMEA WATAMFUATA WAPI KAMA SIIO KWENYE ANUANI YAKE IWE DAR ,DODOMA AU KIJIJINI .....
Mleta mada nimekutukana tusi baya sana.
Tatizo la Nape ni kuwa haaminiki sana, tayari ana mgombea wake kwapani, hebu afikirie Membe angefanyiwa hayo anayofanyiwa Lowassa angeweza kutamka hayo maneno? wao wakubali kuwa, Lowassa kawazidi mbinu za kisiasa, Ikulu haiji kwa kukaa nyumbani, lazima utafute namna ya kufika huko, kwani kanuni za CCM zinazuia watu kumshawishi mtu kwa kwenda kwake?
Lowassa na Nape ni nani aliyetangulia kujiunga na CCM na nani anayeijua vzr CCM? Nape hajui kusoma alama za nyakati...aliwahi kusema kuwa, Jakaya k. akishinda Urais atahama Nchi, lakini hadi leo bado yupo!!!!
Tunaendelea kuwachunguza
lowa jembe wananchi tumesha mkubali nape ninani?
Kosa la alieleta mada ni lipi? Mbona tunatoka nje ya maadili!!!!.