Nape: Lowassa ameanza kufanya kampeni, yuko hatarini kuenguliwa

Nape: Lowassa ameanza kufanya kampeni, yuko hatarini kuenguliwa

10305958_609912092479625_6768162566209220271_n.jpg
 
Hila zinazofanywa na viongozi wa CCM dhidi ya Lowassa ni hujuma dhidi ya CCM.
 
Mimi siamini kama watu wamemtafuta, sipo tayari na itaweza kuamini hivyo. Ni watanzania gani wenye akili timamu wanaokubaliana na wewe kuwa "wananchi wameamua, waacheni" huku ni kupotoshana mchana kweupeeee.

Hao wameitwa...,
tena wamesafirishwa na wakalipwa. kama huamini jiulize ni kwa nini wanakula na kunywa huko, kwa nini hawakufanya hayo alipojiuzulu. Kwa nini hawakumfariji alipokumbwa na kashfa ya Richmond?

Huo ni uongo mkubwa, mbaya zaidi watu wasiofikiria wanaamini kuwa eti mashehe, maaskofu na wanafunzi wamemshawishi awanie urais. Kwani kaanza wiki iliyopita harakati hizo?, mbona tunafanya mambo locally?

Waje mashehe na maaskofu hapa watueleze kama kweli walienda bila kuitwa.

Tusipotoshane ktk hili.
Ahsante.

Mimi sio shabiki sanaa ila nafikiria inawezekana katika hayo makundi kuna wachache wanaanzisha msafara na wanaomba kampani kwa wenzao, wakati huohuo wanawasiliana na wasaidizi wa Lowasa kama yupo, akikubali wanaenda!!hata wewe kwako unaweza kuwa uliumwa au ulipata mtoto nk, watu wakitaka kuja kukuona watauliza kama wapo, na wewe utajua kuna wageni na unaweza hata ukaandaa soda na wali, hilo sidhani kama ni kosa na ndio kinachofanyika na wasaidizi wa Lowasa na yeye pia. Maandalizi yanafanyika kwa sababu anaambiwa kuna wageni kwako, yule ni kiongozi lazima taarifa zitumwe kwake na si kuzuka tu
 
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema kitendo cha mgombea mmoja anayepokea makundi ya watu ili wamshawishi kupiga kura huko Dodoma ni kuanza kampeni na yuko hatarini kuenguliwa.

Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa ndiye anayepokea makundi ya watu wakiwemo masheikh, maaskofu na wanafunzi wakimshawishi kugombea.

Akizungumza na radio VOA, Nape alisema: "Labda niweke vizuri hili, mtu yoyote anayekiuka kanuni hatapitishwa labda kamaa anakwenda kugombea kwa chama kingine.

"Kinachofanyika Dodoma cha watu kuchukuliwa na magari huku wengine wakiwa hawajui, halafu wakifika wanakuta viti vimeshapangwa na vyakula;halafu eti wanamshawishi kugombea, ni kukiuka kanuni na anaweza kuondolewa," alisema Nape.

Huyo nape laana ya mama yake inamsumbua na ndomana mpaka Leo jogoo haliwiki... Hatuwezi tukamsikiliza MTU ambae ni mwanaume hlf sio rijali.. Kinachofanyika Dodoma ni hisia na imani za watanzania kwa Edward Lowassa.. Hongera sana Lowassa
 
Mbona Deo filikunjombe naye kaanza kampeni alichangiwa pia.
Waache unafiki Lowasa kama Maji vile ukiyazuia yamejaa bora uyaache yatiririke.
Ila watu nyoro nyoro hawatakiwi hii nchi tena.
 
Lowasa atakuja kulia kama mwanake mjane aliyefiwa na mume anachofanya ni uvunjifu wa kanuni.

labda wewe,jk na nape ndio hamumtaki lowasa lkn sisi wanachama wengine wa ccm lowassa ndio chaguo letu,hata mvimbe mpasuke mtajijua wenyewe.
 
Nnatumai Nape anao ushahidi wa anayoyasema na kutuhumu watu. Kwamba watu wanaoenda dodoma wamelipwa na nani, kwa njia zipi na kwa sababu gani, la sivyo atakiaibisha chama kwa mara nyengine tena! Wananchi wameamua....acheni uzushi na uongo. Kwa nini mnawadhalilisha wananchi kiasi hiki? Waache kazi zao kwa kulipwa na kupewa chakula? Hivi wote walioonekana huko hawawezi kujinunulia chakula? Tena tunawaingiza mpaka viongozi wetu wa dini; maimamu na wachungaji!

Nnaungana na mtu wa Mungu mmoja aliyemtaka aokoke.....atubu na aokoke!!

Wewe nawe ni mmoja wao.msanii mkubwa wa sarakasi.
 
Hakuna kanuni iliyovunjwa kila kitu kiko sawa kama mbway na iwe mbwayyy
 
CCM itabomolewa na CCM wenyewe subiri uone muvi inayokuja.

ccm wakijajibu ujanja ujanja km ule waliowahi kumfanyia mrema au ule waliomfanyia samwel sitta juzi juzi nakuhakikishia wakijaribu tu kwa mheshimiwa Lowassa watasambaratika vibaya,mpaka dakika hii lowassa 2 ccm 0 halafu ni dakika ya 89.
 
Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi Nape Nauye ni wa kushitakiwa kamati kuu ya chama kwa kukivuruga chama kwa mambo mawili makubwa;

1. Matamshi mbalimbali ya kukidhalilisha chama na viongozi wa chama.
2. Kujenga makundi ndani ya chama kwa matamshi yake.

Hakuna siku haongei pumba lakini anaachwa tu, hadi baadhi ya wanachama na wasio wanachama kuamini ametumwa na viongozi wa juu wa chama.
 
Maneno yako yanaukweli lakini Lowassa hatalipa kisasi amekomaa Mungu akimjalia atawapuuza tuu

mkuu humjui vizuri lagwanan. unakumbuka mashishanga aliyekuwa mkuu wa mkoa wa morogoro? mwaka 1995 alikuwa akimshabikia sumaye hadharan huku akimnanga mkapa. unakumbuka kilichompata wakati mkapa alipoingia whitehouse? kama huna kumbukumbu sema nikukumbushe.
 
Nape hana hata chembe ya kosa afanyacho ni kuwakemea wanachama wanaobeza maagizo halali ya chama na kuwatahadharisha madhara yake.

Ukionywa usianze kampeni ukaanza basi unakemewa na kukumbushwa madhara ya ukaidi kwani mwana mkaidi hafaidi hadi Siku ya IDD!
 
Back
Top Bottom