Nape awavuruga Chadema Mbeya!

Nape awavuruga Chadema Mbeya!

Kimbelembele ni bidii ya kazi ndugu yangu, hii ndio kazi ya uenezi.

Kwahiyo Unasupport yeye kuweka hii Hoja Humu Ndani ya Jamii Forums? na kama ni NDIO kwanini asitumia Jina lake

Kamili kuna Ubaya Gani? naendelea kusema UONGOZI NI HEKIMA sio LELE MAMA
 
watu si wengi kwa sababu sera bali walijua nape anagawa hela na t-shirt na kofia na kama ilivyyo wanafunzi njaa yao nikali sana pia walipokea kadi ili kuwapiga changala macho Nape na chama chake
 
10.+Nape+akiwasili+mbeya.jpg
Naona hawa watoto wameamua kuvaa makoti ya baba zao.....embu cheki huyo wa kushoto wa kwanza...dah!!!1
 
Wanaenda kuuza utu wao, bumu halijatoka sasa wanakwenda kufuata elfu kumi kumi watakazo toa hao Magamba, wanafunzi wengine hawana misimamo.
 
Naona hawa watoto wameamua kuvaa makoti ya baba zao.....embu cheki huyo wa kushoto wa kwanza...dah!!!1

Haya makoti waliyaanda kwa ajili ya green guard ya Mbeya. Sasa wamekosa watu wa kuwa green guard wakayaweka store. Naona wameamua kuyatumia. Niamini mimi ni mmoja wa makada feki.
 
am huyu kijana ni noma alishawahi kuwaangusha rostam, lowasa na chenge akawavua magamba ndani ya siku 90 an akawashawishi wa tz kuvaa uzalendo na pia kuwakumbusha jinsi awamu ya nne ilivyoboresha maisha yao
Ndoto!! ndoto!! ndoto!! Rostama yuko wapi na mihela ya Kagoda 40bl. Chenge wa vijisenti yuko at large. Nepi ikiguswa kitu EL itaungua na yeye mwenyewe Amegwaya!! Amka NEPI ni mchumia tumbo tu!!
 
Mi namkubali si unaona!!
attachment.php





Hata mimi nakubali mkuu, na ungemsikia hapo ungedhani yupo na watu wengi sana kwani sauti anayoitoa utamuoneaa HURUMA.
 
....mkuu,natofautiana na ww kidogo,hapa kwny vyuo vikuu!mbeya kuna vyuo vikuu,mzumbe,teku nk.

You might be right, lakini walimu wa kwenda huko wanatoka wapi, ndio hao hao wa kubabaisha. Sawa hata watotot wangu wako kule wanasoma lakini unaona tofauti kabisa na mtu aliyetoka UDSM, MUHAS, SUA!!!!
 
hapo hakuna jipya, hao wanaoonekana ni wale akinamama wacheza ngoma na hao watoto wa shule tena hii kitu kwa hao watoto ni child abuse! watoto wanashindishwa kwenye jua then wanaambulia jero jero.
 
Halafu mbona mgambo watoto wameva mashati ya watu wazima? Ni yao kweli?
hafu hiyo ni child abuse, wanawashindisha watoto na njaa wanawapa jero jero! hafu hao akina mama na hao wanaume ni moja kati ya kikundi cha wacheza ngoma, hapo hamna kitu!
 
Wadau mimi ni mgeni natoka moshi ila mmenifurahisha jinsi mlivyomgundua huyo jamaa.tumechoshwa na magamba huku moshi kuna baadhi ya mitaa ukikatiza umevaa gamba unapigiwa ukunga kwamba ni mwizi na raia wakifika ni kipigo na kuvuliwa gamba
 
nape unalipenda GWANDA kuliko magamba wenzio HONGERA
 
HUYU dogo wa upande wa kushoto hilo gwanda kalivaa au limemvaa, wangemkodi fundi wa cdm awashonee
 
Ukumbini kwenyewe anakosema mtoa hoja ni hapa... amekosa sera anawachezesha kwaito mchana kweupe

562871_438918729462879_1642534746_n.jpg
 
Nape ndio kiboko yao. Silaha za maangamizi ziko pembeni, zimetulia tuli.

Ni kawaida ya nyoka kujivua gamba ili aweze kuwa kijana asambaze sumu yake ya ufisadi kwa kasi zaidi,nguvu zaidi na hari zaidi.Hata paka aliwahi kujitangaza ameokoka baada ya kuona hawapati panya,alidhoofika sana akidai amefunga na panya walirudisha imani kwake,kitokeo cha hapo wazazi wa panya waliowaruhusu watoto wao kucheza na paka,cha kushangaza watoto wale wa panya walizidi kupungua kwa kasi zaidi na afya ya paka kuimarika zaidi.Kamwe hatuto nasa kwa mtego huo
 
Kwa hili Chadema lazima tukubali CCM wanatupiga goli...Maana haiwezekani wakati wa Bunge viongozi wote wa chama wanakuwa Dodoma wakati CCM ndio inaanza mashambulizi yake. Hii ndio athari ya kuwa na viongozi wote wa chama ndani ya Bunge, maana Dr.Slaa hawezi kuifanya kazi hii peke yake.

Chadema, kwa ushauri wangu viongozi wa chama (Sekretariet) lazima iwe na viongozi ambao sii wabunge wala tunao wategemea kuongoza nchi isipokuwa ni viongozi wa Chama ktk kukijenga chama, haya ndio maandalizi ya chama ktk kuchukua madaraka na kuiongoza nchi.. Kama tunategemea kuwa na viongozi wa chama ndio viongozi wa nchi ni dhahiri na rahisi kujenga Udikteta..Nawakilisha
 
Hawa ndio wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Mbeya?


Bwana Nape,

Hivi hapa NANI ANAMDANGANYA NANI au kwa kimombo WHO IS FOOLING WHO????

Kwanza tumesikia ooh,sijui umati mkubwa,ooh sijui wanachama wapya 167,ooh sijui wanafunzi wa vyuo vikuu wamejazana kukupokea n.k. Sasa mimi nauliza uko wapi umati na wako wapi hao wanachama???

Tunakutaka ujitokeze utoe maelezo ya HIZI PICHA, kuwa hawa watoto ni wa vyuo gani,shule gani,au ni watoto wa mtaani?? Na kwanini WAMEVALISHWA SARE ZA CCM KUBWA(Oversize) KULIKO UMRI WAO???

Bwana Nape hebu jaribu kuwa mwungwana na uachane na hizi porojo za kijinga. Hapa utakuwa unajidanganya menyewe na hao wana magamba wenzio,basi. Kwa hali ya sasa hivi Watanzania hawadanganyiki kwa propaganda za kitoto kama hizi.

 
Nape ameingia Mbeya mchana huu, hakika nimeshangaa vijana wengi wa vyuo wamempokea na kwenda naye ukumbini ambako nako tumekuta watu wengi ajabu waliotambulishwa kama wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya juu Mbeya. Kagawa kadi mpya kwa wanachama wa CCM 167!!!Hivi bado kuna wapuuzi wanaojiita wasomi wanawasikiliza magamba jamani?? Wanachelewesha ukombozi wa nchi yetu! Sugu kamanda angalia umeingiliwa huKu!!

Habari kutoka Shinyanga zinasema uchaguzi wa S/mtaa matokeo CDM imeshinda mitaa 7 CCM imeshinda 4
 
Back
Top Bottom