This is rather sad; hivi kweli tatizo la CCM ni NAPE. As a matter of fact Nape angepewa pongezi na kuungwa mkono na wana CCM wanaotaka mabadiliko ya kweli. Alichokifanya Nape hadharani hakijawahi kufanywa na kionogozi yeyote wa CCM. Wengi wa wale wanaojiita viongozi au wanajionesha kuwa niviongozi hawajawa na ujasiri wa kusimama na kuiita limau limau na chenza chenza! Tangu mwanzo wa sakata hili sikuwahi kusema lolote juu ya Nape lakini ukweli ni kuwa Nape amefanya kilichowashinda wengi na kama aliamua kuondoka kwenye vikao vyao pia ni uamuzi wa akili kwa sababu kwanini watu wakae mahali ambapo hawawezi kusimamia walichokisea. Kama watu wote wenye nguvu Tanzania wanakutanika kwenye chumba kimoja halafu wanashindwa kuchukua uamuzi ambao wanajua walipaswa kuukua bado wanaonekana wamefanya la maana?
Hivi kweli mnataka kusema ndani ya kundi zima la watu wa Kamati Kuu na NEC hakuna mtu aliyekuwa na uwezo wakujibu hoja zinazodaiwa kutolewa na Lowassa, really? Nape hata akijiuzulu kesho, atakuwa amejionesha kuwa amethubutu kufanya kilichomshinda fisi.