Kwa thinking hii hatutegemei CCM ituletee maendeleo yoyote. Tunaona hapa chama kinachoongoza serikali kikijivua nguo kuwa hakipo makini kiasi kwamba CDM inaweza ikafanya mauaji na kuachwa iendelee kuliangamiza taifa. Mawazo gani haya??
CDM haina silaha, Silaha zipo chini ya serikali, serikali inalipa mishahara polisi, polisi ndio wanaofyatua risasi, inawezekanaje tena CDM ndio waonekane wanaua??? Unamana hata kifo cha Mwangosi kimesababishwa na chadema??? Mbona hujaongelea Kifo cha Mwangosi?? au unataka kusema kifo hiki wewe hujakisikia???
Nyie watu mtakujaga kufa midomo wazi kwa usaliti mnaolifanyia taifa hili, mtasababisha vizazi vyenu vipate laana kwa kutetea matumbo yenu. Badala ya kuongelea hoja za msingi zinazolikumba taifa, mnatumia muda wenu kufanya siasa za kihuni na huyo jangiri. Hamuwezi kushinda vita hii coz we are determined to kick you out. Mtapasua makoo yenu ila hamtashinda.
Anatueleza eti Kinana kaenda Songea kudiscuss na Nchimbi namna ya kudhibiti maandamano ambayo CDM inatarajiwa kufanya. Uwe muwazi, Kinana kaenda Songea kufwatilia Meno ya Tembo toka Pori la Akiba la Selous hakuna kitu cha maana alichofwata zaidi ya deal zake za ujangiri. Aidha, huwezi sema kuwa umepata siri kuwa cdm wanampango wa kufanya maandamano. Hakuna siri hapo, kama maandamano yatafanyika ni dhahiri lazma waijulishe polisi intention yao, sasa hapo siri ni ipi???
Kama pumba hivi zinatoka kwa kiongoz wajuu kabisa wa chama tawala, watanzania wenzangu tusitegemee jipya. Haiwezekan kichwa kinachogenerate mawazo haya kiwe kinauwezo wa kugenerate mambo ya msingi.